Mlenge
R I P
- Oct 31, 2006
- 2,125
- 2,291
Je ni Kweli madaktari wanapojua mgonjwa atakufa humficha na kuwaambia ndugu zake tu?
Pana tetesi huzisikia kwamba madaktari wanapotambua mgonjwa atafariki, au ana tatizo kubwa sana kuliko mgonjwa mwenyewe anavyoelewa, basi huwaita ndugu wa karibu wa mgonjwa huyo na kuwaambia "prognosis" mbaya ya ndugu yao, ikiwa ni kifo au tatizo kubwa la kiafya, huku wakimficha mgonjwa mwenyewe. Je, ni kweli?
Ni kwa nini? Kama ni kweli, haikiuki haki za mgonjwa kudhibiti taarifa zake binafsi? Nini kitatokea madaktari wakimwambia mgonjwa, "hutoboi", kama watatumia Kiswahili cha siku hizi, ili mgonjwa aweze kuweka mambo yake sawa akijua fika 'hatoboi', badala ya kubakia na matumaini hewa?
Wengine hudai kwamba mgonjwa akiambiwa ukweli, ndio atakufa kwa kihoro; hata uwezekano mdogo wa kupona utapotea, na kadhalika. Ndivyo ilivyo? Mbona nchi za mbali mgonjwa huambiwa ukweli bila kificho "hautoboi" miezi sita ijayo, na mgonjwa ndio huamua nani amuambie, nani amuache?
Ingekuwa wewe unaumwa kiasi kwamba madaktari wanajua "hutoboi". Ungependa wakuambie au wakufiche?
Ingekuwa ndugu yako anaumwa kiasi kwamba madaktari wanajua "hatoboi". Ungependa wakuambie wewe huku wakimficha mgonjwa au wakufiche wewe na kumwambia mgonjwa?
Pana tetesi huzisikia kwamba madaktari wanapotambua mgonjwa atafariki, au ana tatizo kubwa sana kuliko mgonjwa mwenyewe anavyoelewa, basi huwaita ndugu wa karibu wa mgonjwa huyo na kuwaambia "prognosis" mbaya ya ndugu yao, ikiwa ni kifo au tatizo kubwa la kiafya, huku wakimficha mgonjwa mwenyewe. Je, ni kweli?
Ni kwa nini? Kama ni kweli, haikiuki haki za mgonjwa kudhibiti taarifa zake binafsi? Nini kitatokea madaktari wakimwambia mgonjwa, "hutoboi", kama watatumia Kiswahili cha siku hizi, ili mgonjwa aweze kuweka mambo yake sawa akijua fika 'hatoboi', badala ya kubakia na matumaini hewa?
Wengine hudai kwamba mgonjwa akiambiwa ukweli, ndio atakufa kwa kihoro; hata uwezekano mdogo wa kupona utapotea, na kadhalika. Ndivyo ilivyo? Mbona nchi za mbali mgonjwa huambiwa ukweli bila kificho "hautoboi" miezi sita ijayo, na mgonjwa ndio huamua nani amuambie, nani amuache?
Ingekuwa wewe unaumwa kiasi kwamba madaktari wanajua "hutoboi". Ungependa wakuambie au wakufiche?
Ingekuwa ndugu yako anaumwa kiasi kwamba madaktari wanajua "hatoboi". Ungependa wakuambie wewe huku wakimficha mgonjwa au wakufiche wewe na kumwambia mgonjwa?