Kasimba G
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 3,428
- 2,609
Imetokea bahati mbaya saana asilimia kubwa ya wahusika wa utekwaji na uteswaji hata kuuliwa ni watu wa origin ya Mbeya. Kihistoria watu wa Mbeya haswa wanyakyusa na wandali hawakutawaliwa na wakoloni kama ilivyo kwa wamasai, wachaga, nk. Sababu kubwa ni kwamba wazungu walikuwa wanaogopa makabila ya watu wakali, wakorofi, waelevu na wenye hasira saana, ndio maana kuna baadhi ya nchi kama ethiopia ilishindikana kutawaliwa na wakoloni!
Kwa huku kwetu Tanzania kama nchi kuna baadhi ya sehemu walizo tawaliwa na kuwanyenyekea wazungu na waarabu, lakini sehemu nyingine ilikuwa ngumu kwa sababu ya misimamo hasi ya jumuia husika.
Kwa wanaofuatilia mambo ya nchi yetu, wakati wa uhuru, na mala tuu baada ya uhuru, matukio mbalimbali yalishawahi kuwakuta haswa wanyakyusa, kama kihistoria inajulikana wasomi wakati wa uhuru walikuwa wachache na walikuwa kama tunu ya taifa, lakini, kuna ukoo wa Mwanjisi waliwapoteza wapendwa wao wakati huo, mpaka leo hii haijurikani waliko tangu miaka hiyo ya sitini!
Bahati mbaya pia imewafuatilia mpaka leo hii, matukio kama Mwakyembe, Mwandosya, Mwangosi, Ulimboka, Mwangosi na sasa la Kibanda, Woote hao ni wa asili ya mbeya na bahati mbaya wa kutoka kabila hilohilo la mwanyakyusa "watata wa wakolomi" je ni kwa bahati mbaya au historia inalifuatilia kabila hili ambalo wazungu waliamini kuwa wanajifanya waelevu na wakorofi? Au mamlaka wanalijua hili na wanafuata mkondo wa imani ya wakoloni? Je ni kweli watu wa jamii hii ni wakorofi?
Kistoria pia wanyakyusa walikuwa wajanja wasiopenda vita, mfano mkubwa ni vita kati ya mwanyakyusa na wamalila, waliamua kumuoza binti yao kwa wamalila ili mradi wasipigane vita! Kiufupi walikuwa waelevu kama wazungu walivyowachukulia.
Je serikali wana siri gani na watu wa jaaamii hii? au ni bahati mbaya?
Kwa huku kwetu Tanzania kama nchi kuna baadhi ya sehemu walizo tawaliwa na kuwanyenyekea wazungu na waarabu, lakini sehemu nyingine ilikuwa ngumu kwa sababu ya misimamo hasi ya jumuia husika.
Kwa wanaofuatilia mambo ya nchi yetu, wakati wa uhuru, na mala tuu baada ya uhuru, matukio mbalimbali yalishawahi kuwakuta haswa wanyakyusa, kama kihistoria inajulikana wasomi wakati wa uhuru walikuwa wachache na walikuwa kama tunu ya taifa, lakini, kuna ukoo wa Mwanjisi waliwapoteza wapendwa wao wakati huo, mpaka leo hii haijurikani waliko tangu miaka hiyo ya sitini!
Bahati mbaya pia imewafuatilia mpaka leo hii, matukio kama Mwakyembe, Mwandosya, Mwangosi, Ulimboka, Mwangosi na sasa la Kibanda, Woote hao ni wa asili ya mbeya na bahati mbaya wa kutoka kabila hilohilo la mwanyakyusa "watata wa wakolomi" je ni kwa bahati mbaya au historia inalifuatilia kabila hili ambalo wazungu waliamini kuwa wanajifanya waelevu na wakorofi? Au mamlaka wanalijua hili na wanafuata mkondo wa imani ya wakoloni? Je ni kweli watu wa jamii hii ni wakorofi?
Kistoria pia wanyakyusa walikuwa wajanja wasiopenda vita, mfano mkubwa ni vita kati ya mwanyakyusa na wamalila, waliamua kumuoza binti yao kwa wamalila ili mradi wasipigane vita! Kiufupi walikuwa waelevu kama wazungu walivyowachukulia.
Je serikali wana siri gani na watu wa jaaamii hii? au ni bahati mbaya?