Nilikuwa nasoma mtandaoni leo gazeti moja la kiingereza lililoandika habari ya jinsi fedha zilizotarajiwa kufufua kiwanda cha nguo cha Urafiki lakini zikaliwa na wajanja!!
Pia habari kama hizo hizo zimeeleza jinsi viwanda vyetu vilivyobinafsishwa kugeuzwa maghala na huku waliouziwa mpaka sasa wengine hawajamaliza kuvilipia kama vile kiwanda cha madawa Moshi na Moproco Morogoro.
Sasa msomaji mmoja ameandika comment baada ya habari hizi kwenye hilo gazeti kuwa eti wanasiasa wa Tanzania ni wezi na wabadhilifi wa mali za umma kuliko aliyekuwa mtawala wa Zaire Mobutu Sese Seko na yule wa Phillipines Marcos na familia yake.
Je ni kuwa kweli hawa watawala wetu wametuibia mpaka wakawa na utajili wa namna hiyo?
Pia habari kama hizo hizo zimeeleza jinsi viwanda vyetu vilivyobinafsishwa kugeuzwa maghala na huku waliouziwa mpaka sasa wengine hawajamaliza kuvilipia kama vile kiwanda cha madawa Moshi na Moproco Morogoro.
Sasa msomaji mmoja ameandika comment baada ya habari hizi kwenye hilo gazeti kuwa eti wanasiasa wa Tanzania ni wezi na wabadhilifi wa mali za umma kuliko aliyekuwa mtawala wa Zaire Mobutu Sese Seko na yule wa Phillipines Marcos na familia yake.
Je ni kuwa kweli hawa watawala wetu wametuibia mpaka wakawa na utajili wa namna hiyo?