Kuna jambo linaendelea nchini ambalo nafikiri wengi wetu hatufahamu lakini ukitazama kwa jicho la tatu la kisiasa utakubaliana na mimi kwamba pengine ni hujuma dhidi ya Rais Samia kwa sababu ili jambo lolote litokee lazima liwe na sababu.
Matukio haya machache yanatoa taswira ni kwa jinsi gani Rais samia anaweza kuwa anahujumiwa;
1. MATUKIO YA MOTO
Siku chache baada ya Samia kukalia kiti cha urais kuliibuka matukio ya moto ikiwemo kuungua kwa soko kubwa la kibiashara la kariakoo pamoja na shule. Matukio hayo ya mato yalitokea kwa kufuatana kwa mfululizo mara ghafla yakapotea hadi wa leo hakuna kisa cha moto kingine kilichoripotiwa.
Katika nyanja ya kisiasa naweza kugawa matukio haya ya moto katika taswira mbili;
(i)yalilenga kumjaribu Rais Samia kuona amejipangaje, kujua tabia yake, kupima uwezo wake na kujua reaction zake endapo atajua kama anahujumiwa.
(ii) yalikuwa yanalenga kumdhoofisha Rais samia kwamba ameshindwa kulinda usalama wa raia na mali zao hivyo hatoshi kuendelea kukalia kiti cha urais kama amiri jeshi mkuu.
2. TUKIO LA DAKTARI KUSHINDWA KUHUTUBIA MDAHALO WA CHANJO YA UVIKO-19
Kwangu naliona lile tukio kama issue ambayo ilikuwa planned kuanzia kwa daktari mwenyewe na wahusika ambao sauti zao zinasikika kwenye ile video clip. Kwanini nasema ni planned?
(i) kama kweli yule daktari alikuwa ana matatizo ya kiafya angeomba hudhuru na kutolewa kwenye orodha ya wachangia mada haraka iwezekanavyo lakini haikuwa hivyo. Lakini pia tujiulize, siku zote serikali imekuwa ikiandaa midahalo mikubwa, ukichilia mbali kigugumizi hatujawahi kusikia mtu ameshindwa kuhutubia na kuanguka chini, iweje kwenye mdahalo wa chanjo ya uviko-19 ambayo imekuwa na mapokeo na mtazamo tofauti miongoni mwa watu ndipo linajitokeza hili tena likirushwa live kwenye television ya taifa?
(ii) ukitazama ile video clip ya tukio kuna sauti zinasikika zikisema "alikuwa amechanjwa" na nyingine ikisema "hakikisha hii video haisambai kwa watu". Kama ni kweli yule daktari alishindwa kufanya mdahalo kwa matatizo ya kiafya kwanini wahusika ambao sauti zao zinasikika kwenye ile video clip hawakusema tatizo lingine kama vile uchovu n.k lakini walikimbilia moja kwa moja kuhusianisha hilo tukio na chanjo ya uviko-19?
Je, ni nani aliyerusha hiyo video ambayo walikuwa wameambizana isisambae kwa watu?
Ukijiuliza hayo maswali ndipo unagundua kwamba lile tukio lilikuwa planned na lengo hasa ni kudhoofisha zoezi la utoaji chanjo ambalo limeratibiwa na Rais mwenyewe. Vile vile walilenga kuaminisha wananchi kwamba chanjo zina madhara ila serikali inaficha ndio maana kwenye clip mmoja wao anasikika kwa sauti akisema video isisambae wakati wangeweza kukatisha kipindi pasipo kurekodi sauti zao.
3. TUKIO LA WIZARA YA KILIMO KUCHAPISHA MAUDHUI YASIYOFAA
Jana kwenye ukarasa wa mtandao wa twitter wa wizara ya kilimo kulichapishwa maudhui yasiyohusiana na mambo ya wizara ambapo iliwekwa picha ya binti mrembo akitakiwa heri ya siku yake ya kuzaliwa.
Japo wizara ilijitokeza na kusema kwamba account hiyo ilidukuliwa lakini pia kwa jicho la tatu inaweza kuwa ni tukio la kupangwa ili kuwaaminisha watu kwamba serikali ya Rais Samia haiko serious kwenye mambo ya msingi na kwamba inaendesha mambo yake hovyo hovyo bila mpangilio kama hilo la kutakiana birthday kwenye ukurasa wa serikali.
Watu wanaweza kujiuliza kwanini nasema Rais Samia anahujumiwa?
Ukweli ni huu,
(i) Ndani ya CCM kuna genge ambalo limejipanga kuhakikisha Rais Samia ana kwama na hafanyi jambo lolote la maana la kuwagusa wanchi katika kipindi hiki cha miaka minne. Kwa kifupi asiache alama yoyote ya kukumbukwa na watu katika uongozi wake.
(ii) genge hilo hilo limejipanga kumtengenezea chuki na kumpunguzia hali ya kukubalika kwa wananchi na itakapofika 2025 asipate kibali cha kuwania kiti cha urais ili waweke mtu wao wanayemtaka.
Nini Rais Samia afanye kujinasua katika matego haya anayotegewa?
Rais samia anatakiwa afanye mambo makuu yafuatayo;
(i) Achague watu makini wa kumshauri na ajiepushe na waliokuwa washauri wa mtangulizi wake kwani ndio wanaendesha genge la kumkwamisha.
(ii) Rais samia apenyeze mashushu (informers) wake mitaani na kwenye taasisi zote za kiserikali ambao ni royal kwake ili wamsaidie kudhibiti matukio na kukusanya taarifa za wanaopanga kumkwamisha au kumhujumu. Hata Rais magufuli pia alifanya hivyo baada ya kuona hali ni tete. Hii itamsaidia Rais Samia kutumia muda mwingi kuwaletea wananchi maendeleo kuliko ilivyo sasa kwa sababu kila jema atakalopanga atakwamishwa tu.
(iii) Rais samia afanye mabadiliko kidogo kwenye baraza la mawaziri kwa kuweka mawaziri wenye nia ya dhati na serikali yake ya kuwaletea wananchi maendeleo sio wenye uchu wa madaraka na wafuasi wa mtangulizi wake kwani ndio wanaongoza genge la kumkwamisha.
Matukio haya machache yanatoa taswira ni kwa jinsi gani Rais samia anaweza kuwa anahujumiwa;
1. MATUKIO YA MOTO
Siku chache baada ya Samia kukalia kiti cha urais kuliibuka matukio ya moto ikiwemo kuungua kwa soko kubwa la kibiashara la kariakoo pamoja na shule. Matukio hayo ya mato yalitokea kwa kufuatana kwa mfululizo mara ghafla yakapotea hadi wa leo hakuna kisa cha moto kingine kilichoripotiwa.
Katika nyanja ya kisiasa naweza kugawa matukio haya ya moto katika taswira mbili;
(i)yalilenga kumjaribu Rais Samia kuona amejipangaje, kujua tabia yake, kupima uwezo wake na kujua reaction zake endapo atajua kama anahujumiwa.
(ii) yalikuwa yanalenga kumdhoofisha Rais samia kwamba ameshindwa kulinda usalama wa raia na mali zao hivyo hatoshi kuendelea kukalia kiti cha urais kama amiri jeshi mkuu.
2. TUKIO LA DAKTARI KUSHINDWA KUHUTUBIA MDAHALO WA CHANJO YA UVIKO-19
Kwangu naliona lile tukio kama issue ambayo ilikuwa planned kuanzia kwa daktari mwenyewe na wahusika ambao sauti zao zinasikika kwenye ile video clip. Kwanini nasema ni planned?
(i) kama kweli yule daktari alikuwa ana matatizo ya kiafya angeomba hudhuru na kutolewa kwenye orodha ya wachangia mada haraka iwezekanavyo lakini haikuwa hivyo. Lakini pia tujiulize, siku zote serikali imekuwa ikiandaa midahalo mikubwa, ukichilia mbali kigugumizi hatujawahi kusikia mtu ameshindwa kuhutubia na kuanguka chini, iweje kwenye mdahalo wa chanjo ya uviko-19 ambayo imekuwa na mapokeo na mtazamo tofauti miongoni mwa watu ndipo linajitokeza hili tena likirushwa live kwenye television ya taifa?
(ii) ukitazama ile video clip ya tukio kuna sauti zinasikika zikisema "alikuwa amechanjwa" na nyingine ikisema "hakikisha hii video haisambai kwa watu". Kama ni kweli yule daktari alishindwa kufanya mdahalo kwa matatizo ya kiafya kwanini wahusika ambao sauti zao zinasikika kwenye ile video clip hawakusema tatizo lingine kama vile uchovu n.k lakini walikimbilia moja kwa moja kuhusianisha hilo tukio na chanjo ya uviko-19?
Je, ni nani aliyerusha hiyo video ambayo walikuwa wameambizana isisambae kwa watu?
Ukijiuliza hayo maswali ndipo unagundua kwamba lile tukio lilikuwa planned na lengo hasa ni kudhoofisha zoezi la utoaji chanjo ambalo limeratibiwa na Rais mwenyewe. Vile vile walilenga kuaminisha wananchi kwamba chanjo zina madhara ila serikali inaficha ndio maana kwenye clip mmoja wao anasikika kwa sauti akisema video isisambae wakati wangeweza kukatisha kipindi pasipo kurekodi sauti zao.
3. TUKIO LA WIZARA YA KILIMO KUCHAPISHA MAUDHUI YASIYOFAA
Jana kwenye ukarasa wa mtandao wa twitter wa wizara ya kilimo kulichapishwa maudhui yasiyohusiana na mambo ya wizara ambapo iliwekwa picha ya binti mrembo akitakiwa heri ya siku yake ya kuzaliwa.
Japo wizara ilijitokeza na kusema kwamba account hiyo ilidukuliwa lakini pia kwa jicho la tatu inaweza kuwa ni tukio la kupangwa ili kuwaaminisha watu kwamba serikali ya Rais Samia haiko serious kwenye mambo ya msingi na kwamba inaendesha mambo yake hovyo hovyo bila mpangilio kama hilo la kutakiana birthday kwenye ukurasa wa serikali.
Watu wanaweza kujiuliza kwanini nasema Rais Samia anahujumiwa?
Ukweli ni huu,
(i) Ndani ya CCM kuna genge ambalo limejipanga kuhakikisha Rais Samia ana kwama na hafanyi jambo lolote la maana la kuwagusa wanchi katika kipindi hiki cha miaka minne. Kwa kifupi asiache alama yoyote ya kukumbukwa na watu katika uongozi wake.
(ii) genge hilo hilo limejipanga kumtengenezea chuki na kumpunguzia hali ya kukubalika kwa wananchi na itakapofika 2025 asipate kibali cha kuwania kiti cha urais ili waweke mtu wao wanayemtaka.
Nini Rais Samia afanye kujinasua katika matego haya anayotegewa?
Rais samia anatakiwa afanye mambo makuu yafuatayo;
(i) Achague watu makini wa kumshauri na ajiepushe na waliokuwa washauri wa mtangulizi wake kwani ndio wanaendesha genge la kumkwamisha.
(ii) Rais samia apenyeze mashushu (informers) wake mitaani na kwenye taasisi zote za kiserikali ambao ni royal kwake ili wamsaidie kudhibiti matukio na kukusanya taarifa za wanaopanga kumkwamisha au kumhujumu. Hata Rais magufuli pia alifanya hivyo baada ya kuona hali ni tete. Hii itamsaidia Rais Samia kutumia muda mwingi kuwaletea wananchi maendeleo kuliko ilivyo sasa kwa sababu kila jema atakalopanga atakwamishwa tu.
(iii) Rais samia afanye mabadiliko kidogo kwenye baraza la mawaziri kwa kuweka mawaziri wenye nia ya dhati na serikali yake ya kuwaletea wananchi maendeleo sio wenye uchu wa madaraka na wafuasi wa mtangulizi wake kwani ndio wanaongoza genge la kumkwamisha.