Je!? Ni kweli kakobe alitaka kuvunja ndoa ya mtu singida?

Maneno yapi? kubali ukweli na ujirekebishe? usiwe kama Yuda isikari yote aliyekuwa miongoni mwa wale 12 waliokiri kuwa hakuna hata mmoja wa kumsaliti mwishoni akamsaliti.
ndani ya upentecoste kuna tatizo na wenye macho ya kiroho na kimwili wanajua hilo na ndiyo maana hata wachungaji wenyewe kwa wenyewe wanashambuliana, hata kushambuliana kuwa wengine wanajihusisha na ushirikina. Kakobe humshambulia rwakatare mara kwa mara, na wengine kama akina Katunzi kupitia wapo radio ndiyo usiseme ni matusi ya kejeli kwa watumishi wengine wapentekoste mbele kwa mbele.

Vipofu wa kiroho kama wewe ni vigumu kuliona na wanajivunia haya, ilimradi tu wanadai ni wapentekoste. Unaishia kuhukumu na kutukana watu! wewe una hadhi gani ya upentekoste? kwa sababu tu unasali kwa kakobe? Kumbuka Yesu alisema Haki yenu isipozidi haki ya mafarisayo mbinguni hamwingii. Hawa watumishi wapentecoste wanaojimbana kila siku, huo ndio wito wao?

ikiwa watumishi wanashambuliana hizi muda wa kujenga systems za uongozi na utawala ndani ya makanisa yao kushughulikia migogoro midogo mpaka wanakimbilia kwa waandishi watakuwa nao?
Wengi pengine hata wewe mmegeuza upentecoste kichaka kama si fimbo ya kuchapia wengine kwa kigezo cha repent na uokoke.Ni lazima kutoa boriti ndani ya jicho lako kabla ya kupiga kelele kuhusu kibanzi cha mwenzako.

Kumbuka Yesu alisema wengi watakuja watasema "Bwana Bwana...., naye atawajibu siwajui, ondokeni." Upentekoste wako isiwe fimbo ya kuhukumu na kutukana wengine na kujiona wewe ni bora zaidi ya wengine mbele za Mungu.

ndugu yangu, mimi wala sisali kwa kakobe, wala usihangaike kugesi vitu. pia, tusifike mbali. nimesema wewe si mpendecost kwasababu niliona umejiunga na wapinga kristo kushambulia ukristo, na hivyo utapata thawabu ya wapinga kristo. upentecost haumfikishi mtu mbinguni hata hivyo, na kwenye upentecost kuna madhehebu mengi..yote hayo ni taratibu tu za kuwafikisha watu kwenye njia sahihi wamwone Mungu wao wenyewe ibinafsi...si ticket toka kwenye dhehebu kuwa ndio ufike mbingini, pamoja na kwamba, si madhehebu yote yana system nzuri ya kumlisha mtu Neno la Mungu akamwona Mungu.

watu waliookoka wana hofu ya Mungu, watu waliookoka huwa hawakurupuki tu kumshambulia mtu hasa anayejihusisha na mambo ya Mungu, kwasababu kufanya hivyo ni kitu hatari kwao, ndio maana nikasema wewe sio mpentecost kwasababu niliona hauna hata hofu ya Mungu, siku maanisha kuwa wewe nim wenye dhambi sana la hasha, bali hauna tabia za kipentecost....ukimgusa mtumishi wa Mungu, unagusa mboni ya jicho la Mungu. hata tz kuna watumishi wa Mungu wengi sana, pamoja na kwamba unaona kama wanashambuliana wao kwa wao, haiwatoi kwenye fact kwamba bado ni watumishi wa Mungu. kukemeana katika wokovu ni kitu cha kawaida, na wachungaji si malaika. Paulo alimkemea Petro mbele za watu kabisa kwasababu petro aliteleza kidogo, na bado tu wote waliendelea kutumika mbele za Mungu. NI NANI ATAWAHUKUMU WATEULE WA MUNGU? MUNGU NDIYE MWENYE KUWAHUKUMU, na si mwanadamu...ukifanya hivyo utakula jeuri yako.

Miriam dada yake Musa pamoja na wengine, walijiunga kwenye kikundi wakamshambulia Musa kuwa kwanini amemuoa mwanamke methiopia/kushi/seba,....kilichotokea, haijalishi kama walikuwa sahihi au la, Mungu alishuka kwa hasira, AKAMPIGA MIRIAMU KWA UKOMA, ilibidi Musa aanze kumwomba mungu upya ili amponye tena.

Ndugu yangu, watumishi wote wa Mungu huwa wanatukanwa na kusinginziwa mambo mengi, Yesu mwenyewe alitukanwa na kusingiziwa, ni vita tu vya shetani, ila mwishoni huwa inakuja kugundulika kuwa walikuwa wanaonewa tu pamoja na kwamba wamesharushiwa matope hadi wamechoka....usikurupuke tu kuanza kushambulia, huwezi kujua kakobe au mtumishi yeyote wa Mungu yuko kwenye vita ipi katika ulimwengu wa roho wa hapo tz...in order for you to be safe, tulia kimya, mwombe Mungu awasaidie watumishi wa Mungu kwenye vita, au pale walipovunjika moyo au kuteleza, ili wasimame na kazi ya Mungu iendelee...HAUNA HATA SAUTI YA KUWAHUKUMU WATUMISHI WA MUNGU. ushauri wangu ndio huo..unaweza kuendelea kurusha mawe yako...lakini nakuhakikishia, utaona matunda yake siku moja na utakuwa wa kwanza kwenda kuwambia watu waache ulichokuwa unakifanya. Mungu akusaidie, na wote.

by the way, watu wawili tu wameshikilia bango jambo hili....na mko biased sana!
 
uyo mdad katumika tu na watu.asi unajua dini ni km siasa T thats umwaribie uyu upate wew.
i dnt blv t i knw km alisema alisema ktk ground nzurio bt dada kaamua kuiconvert t n use per her nid for certain reason
m nt his follower bt i dnt blv if he can comments on such eveil act
achen kumzushia bwana
ata km aumwamina au aumpend bt haina haja ya kumzushia
uyu dada sjui kaadiwa nini na kina nan bt yeye anajua
aache dhambi ela aliyopewa itamwangamiza mwenyewe
si utu wala ukristu ausemi ivo
na km uyo dadA KM angekuwa mkristu wa kweli aka mlokole as she claims to b asingetumia njia hii ya magazeti na kufanya publicity ya ukweli juu ya ajambo liwalo lolote ambalo wametofautiana na kakobe angutumia njia za kikristu ambazo nio dplomatic byu nature na si za ki shabiki km ambazo katumia .kuna wazee wa kanisa n a like amabao wangeweza kusolve i mambo bt habari ya kuita press confrence kwa kweli nimempa doubt kubwa sana
kuna kitu anachotafuta uyu si ayo aliyoenda kushtaki
atubu cz mapepo 77 yamemganda na aende akajiunge na chadema au cuf au ccm naona she got elements of POLITICS.

DADA tafuta njia ingine bt ntoke vp ya namna i isnt gud 4u :closed_2: hauna tofauti na yuda kwa dinari 30 hahahahaha pole
 
Utawala wenye misingi ya fitina hufika mahali ukajifitinisha wenyewe. Hapo ndipo wenye macho wanapoweza kumtambua mtu amevaa nguo ya rangi gani. Kamuulize Mwaitege namna ya kumtambua mtu aliye rohoni. Sio kwa mn'ao wake na maneno yenye utata kila saa, sio kwa mbwembwe zake na udhibiti wa watu wengine. Lakini chumvi ikishaharibika, itiwe nini ili ikolee?

Hebu nenda Iringa uangalie kando ya barara, kuna makaburi yamepakwa chokaa yanang'aa sana, hurudiwa kupakwa chokaa kila mara hata ukiwa gizani utayaona. Je, ina maana waliomo mle ndani ni watu hai? Sio ajabu wanaopaka chokaa makaburi yale hawana uwezo wa kujipatia hata milo mitatu kwa siku, imani zao zimeelekezwa kwenye kile wanachokifanya. Yeyote aendaye kinyume nao ni adui yao. Kwa nini Luther alianzisha Kanisa la Kilutheri wakati yeye alikuwa Padre mwenye kuaminika sana na Papa wake? Ukitaka kuona jinsi rhumba linavyochakatwa ingia ndani uwaone wanaocheza live. Usiamini stori wanazotoa waliohudhuria mle ndani, kwani habari ya mkono wa tatu haitakuwa na uzito sawa na unachokiona wewe mwenyewe.

Kwani kuna mtu anayo nguvu ya kuelezea maovu yake? Mungu amemjalia binadamu kujihami katika kujieleza ili kujisafishia sura machoni pao wanaomsikiliza. Nani ni mjinga hata akusimulie jinsi anavyovaa nguo yake ya ndani iliyochakaa kwa kukosa matunzo mema? Mtu hupiga mswaki kwa bidii meno yake ya mbele ili akitabasamu watu wammpongeze na apate sifa, lakini ni nani mwenye uhalali wa kujua sababu ya mtu kukosa meno meno ya nyuma hata akashindwa kutafuna chips dume?

Aliyezoea kula vitu laini unamwonea kumpa bisi. Siri ya maiti aijuaye ni mwosha, lakini je, mwosha anaijua siri yote ya maiti? Mungu huangalia moyo wa binadamu na wala sio maumbile ya mtu. Kama hujaijenga nyumba huna haki ya kuikosoa isipokuwa umeambiwa hatua zote za ujenzi huo nawe ukawa mtaalam wa uwezo huo. Kwa nini mtazamaji mpira ajifanye kujua kuliko mchezaji uwanjani?

Imani ya mtu na iheshimiwe, kama ndoa za watu zinavyoheshimiwa. Kuikosoa imani ya mtu ni zaidi ya kukosoa ndoa ya jirani yako. Kuishi jirani na mwenzio sio warrant ya kufahamu jinsi maisha ya wanandoa majirani zako yalivyo. Kila wakati kumbuka mwanangu, unachokijua juu ya mwenzako ni kidofgo kuliko kilele cha pua ya kiboko unayoiona mtoni, mengi sana huwezi kuyajua. Yapo mambo mengine ambayo misahafu inatuambia kwamba hata mkeo wa kifuani pako hapaswi kuyajua.

Mungu aonaye sirini na awajaze kila mmoja wetu, hekima kifuani pake ili ajue namna ya kutafakari na kuwatoa kasoro wenzie, kwani machoni pa Mungu wanadamu wote wamepotea, wameoza wote pia. SI unajua mwizi hapendi kuibiwa? ANayefanya ujambazi kamwe hakubali kufanyiwa ujambazi. Unafikiri mbakaji anapenda kubakwa? Ujue tunaelekea ukingoni, mtakatifu na aendelee kuwa mtakatifu, mwovu na aendelee kuwa mwovu zaidi, siku yake ikifika, ikakuwa kama Paulo ambaye hakuwahi kufikiri atakuwa mkristo, achilia mbali kuwa kiongozi na mwalimu wa ukristo huo. Aliongoka akienda kutimiza haki ya kuwamaliza wakristo, akaishia kuwa mkristo yeye mwenyewe hata kabla hajafika mwisho wa safari yake.

Mambo mengine tumwachie Roho Mtakatifu, tusije tukajikuta tunamkufuru hata tusisameheke milele. SI wajua dhambi kubwa kuliko yote ni kumkufuru Yeye? Kama mtu anasema anafanya kazi ya Mungu, mwombee aifanye kwa usahihi wa Mungu aliyemtuma, kama waona anaenda ndivyo sivyo mwonye. Asipoonyeka hata mbele ya wenye kuenenda kiroho watatu, mwachieni na msahauni, Mungu atajua njia mwafaka kumrekebisha, kwani asiyesikia la mkuu si huvunjika guu lake mwenyewe?
 
Hawa wote ni manabii wa giza, wengi wao huishia kuwa wauwaji. Kibwetere,David Koresh, Jim Jones, etc, walianza kama watumishi wa Mungu na walikuwa wakitumia mkono wa chuma kuwanyamazisha waumini wao.

Wanaanza kama Mesiah, wana wa brain-wash waumini (mfano kulinda kanisa wiki kadhaaa)... matokeo yake kifo...
 
1099_show_image_xlarge.jpg

Killer Cults: The Men Who Would Be Gods
Coming Soon




Motivation of the Guru: his desire for power and ambition to become master of his own warped world.

All sects function in a similar manner. Organised as a totalitarian system, a sect is like a miniature dictatorship, using the classic weapons of propaganda and repression. This series reveals, for the first time, the implacable techniques that Gurus use to seduce, condition and train their believers, leading them towards suicidal or murderous violence.

Taking four of its most notorious examples: The Order of the Solar Temple, The Aum, The Branch Davidians and The People’s Temple, this series explores the initiation of innocents into sects, the internal organisation and structure of the sects, the psychological portraits of their leaders and the sect’s final apocalypse.
 
Khe!! Kuna mnyukano hapa. Mpaka haijulikani nani ni nani. Kumbukeni kuwa maneno mazuri humtoa tembo shambani.
 
Hawa wote ni manabii wa giza, wengi wao huishia kuwa wauwaji. Kibwetere,David Koresh, Jim Jones, etc, walianza kama watumishi wa Mungu na walikuwa wakitumia mkono wa chuma kuwanyamazisha waumini wao.

Wanaanza kama Mesiah, wana wa brain-wash waumini (mfano kulinda kanisa wiki kadhaaa)... matokeo yake kifo...

Hapana hawa ni watumishi wa MUNGU wa kwedli, usisahau kuwa na wao ni wanadamu kama mimi na wewe, wanahitaji sana maombi yetu ili waweze kuenenda katika njia ifaayo, wasihukumiwe, Kumbuka Mungu hutumia wanadamu katika kufanikisha matakwa yake kwa binadamu wengine, Kila mtu anayomapungufu yake ndiyo maana yesu alikufa kwa ajili yetu sote ili katika yeye tuwe na uzima tele.Wakati wewe unawaangalia katika namna tofauti MUNGU anawaangalia katika kutimiza kazi yake.
Kumbuka: Bwana alisema, amlaaniye Israel naye amelaaniwa, Ambarikiye naye ubarikiwa.
 
Mkuu, hata mimi nashangaa, KOKOBE IS A PROBLEM TO HIS OWN ESTABLISHMENT. huwa ni mwepesi sana kuita waandishi wa hapari ikiwa anakuwa kinyume na wengine. Inapokuwa issue inamhusu yeye huwa anadai niko kwenye maombi.

After all he is businessman like anybody else. The only difference is he uses word Bible as his capital and Ignorant Tanzanians as money minting goods. Simple
 
ndugu yangu, mimi wala sisali kwa kakobe, wala usihangaike kugesi vitu. pia, tusifike mbali. nimesema wewe si mpendecost kwasababu niliona umejiunga na wapinga kristo kushambulia ukristo, na hivyo utapata thawabu ya wapinga kristo. upentecost haumfikishi mtu mbinguni hata hivyo, na kwenye upentecost kuna madhehebu mengi..yote hayo ni taratibu tu za kuwafikisha watu kwenye njia sahihi wamwone Mungu wao wenyewe ibinafsi...si ticket toka kwenye dhehebu kuwa ndio ufike mbingini, pamoja na kwamba, si madhehebu yote yana system nzuri ya kumlisha mtu Neno la Mungu akamwona Mungu.

watu waliookoka wana hofu ya Mungu, watu waliookoka huwa hawakurupuki tu kumshambulia mtu hasa anayejihusisha na mambo ya Mungu, kwasababu kufanya hivyo ni kitu hatari kwao, ndio maana nikasema wewe sio mpentecost kwasababu niliona hauna hata hofu ya Mungu, siku maanisha kuwa wewe nim wenye dhambi sana la hasha, bali hauna tabia za kipentecost....ukimgusa mtumishi wa Mungu, unagusa mboni ya jicho la Mungu. hata tz kuna watumishi wa Mungu wengi sana, pamoja na kwamba unaona kama wanashambuliana wao kwa wao, haiwatoi kwenye fact kwamba bado ni watumishi wa Mungu. kukemeana katika wokovu ni kitu cha kawaida, na wachungaji si malaika. Paulo alimkemea Petro mbele za watu kabisa kwasababu petro aliteleza kidogo, na bado tu wote waliendelea kutumika mbele za Mungu. NI NANI ATAWAHUKUMU WATEULE WA MUNGU? MUNGU NDIYE MWENYE KUWAHUKUMU, na si mwanadamu...ukifanya hivyo utakula jeuri yako.

Miriam dada yake Musa pamoja na wengine, walijiunga kwenye kikundi wakamshambulia Musa kuwa kwanini amemuoa mwanamke methiopia/kushi/seba,....kilichotokea, haijalishi kama walikuwa sahihi au la, Mungu alishuka kwa hasira, AKAMPIGA MIRIAMU KWA UKOMA, ilibidi Musa aanze kumwomba mungu upya ili amponye tena.

Ndugu yangu, watumishi wote wa Mungu huwa wanatukanwa na kusinginziwa mambo mengi, Yesu mwenyewe alitukanwa na kusingiziwa, ni vita tu vya shetani, ila mwishoni huwa inakuja kugundulika kuwa walikuwa wanaonewa tu pamoja na kwamba wamesharushiwa matope hadi wamechoka....usikurupuke tu kuanza kushambulia, huwezi kujua kakobe au mtumishi yeyote wa Mungu yuko kwenye vita ipi katika ulimwengu wa roho wa hapo tz...in order for you to be safe, tulia kimya, mwombe Mungu awasaidie watumishi wa Mungu kwenye vita, au pale walipovunjika moyo au kuteleza, ili wasimame na kazi ya Mungu iendelee...HAUNA HATA SAUTI YA KUWAHUKUMU WATUMISHI WA MUNGU. ushauri wangu ndio huo..unaweza kuendelea kurusha mawe yako...lakini nakuhakikishia, utaona matunda yake siku moja na utakuwa wa kwanza kwenda kuwambia watu waache ulichokuwa unakifanya. Mungu akusaidie, na wote.

by the way, watu wawili tu wameshikilia bango jambo hili....na mko biased sana!

Unamaanisha Lumbe Akijitambulisha kwako kwamba yeye ni Mtumishi wa Mungu Utafuta kauli zako zote Dhidi yake? Kwa maana Kwa mujibu wako, kitu Muhimu ni kujitambulisha tu kwa maneno na maandiko ya kwenye biblia bila kujali matendo yako!!!. Si ndivyo?
 
Ndugu yangu, watumishi wote wa Mungu huwa wanatukanwa na kusinginziwa mambo mengi, Yesu mwenyewe alitukanwa na kusingiziwa, ni vita tu vya shetani, ila mwishoni huwa inakuja kugundulika kuwa walikuwa wanaonewa tu pamoja na kwamba wamesharushiwa matope hadi wamechoka....usikurupuke tu kuanza kushambulia, huwezi kujua kakobe au mtumishi yeyote wa Mungu yuko kwenye vita ipi katika ulimwengu wa roho wa hapo tz...in order for you to be safe, tulia kimya, mwombe Mungu awasaidie watumishi wa Mungu kwenye vita, au pale walipovunjika moyo au kuteleza, ili wasimame na kazi ya Mungu iendelee...!

Maneno mazito sana haya.
 
Mambo mengine tumwachie Roho Mtakatifu, tusije tukajikuta tunamkufuru hata tusisameheke milele. SI wajua dhambi kubwa kuliko yote ni kumkufuru Yeye? Kama mtu anasema anafanya kazi ya Mungu, mwombee aifanye kwa usahihi wa Mungu aliyemtuma, kama waona anaenda ndivyo sivyo mwonye. Asipoonyeka hata mbele ya wenye kuenenda kiroho watatu, mwachieni na msahauni, Mungu atajua njia mwafaka kumrekebisha, kwani asiyesikia la mkuu si huvunjika guu lake mwenyewe?

Aksante.
 
KAKOBE ALIPULIWA - NA HERRIETH BENNY WA GAZETI LA MTANZANIA




MUUMINI wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), la Askofu Mkuu Zachary Kakobe, ameibuka na kutoa siri nzito kuhusu Kanisa hilo.

Mtoa siri huyo ni Mchungaji Monicah Mtasingwa, ambaye pamoja na mambo mengine, ameeleza ubabe, ukiukwaji wa haki za binadamu na adha za maisha zinazowafanya wachungaji na waumini wa Kanisa waishi kwa shida.

Mtasingwa alitoa siri za Askofu Mkuu Kakobe jana alipozungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jijini Dar es Salaam.

Alisema miongoni mwa adha walizoonja kwa kuwapo kwao kwa Kakobe ni kuuza mali zao zote kwa ajili ya kuanzisha tawi la Kanisa hilo, lakini wameishia kupokwa kila kitu.

Alisema Askofu Mkuu Kakobe anatumia vitisho kuwakandamiza wachungaji wake wasijiendeleze kielimu huku akiwambia kuwa yeyote atakayekiuka sheria zake atakufa.

Kitu kingine ni kwamba wachungaji na waumini wanazuiwa kushirikiana na watu wa madhehebu mengine kwa madai kwamba ni wazinzi na makahaba.

Mtasingwa alisimulia jinsi yeye na mumewe walivyoweza kuingia katika Kanisa hilo, na kufikia hatua ya kwenda kuanzisha tawi Nzega.

"Wakati huo mume wangu alikuwa mfanyakazi wa benki, mimi nilikuwa nimemaliza kidato cha sita Msalato mkoani Dodoma, tulipofika huko tulianza kuishi maisha ya kimasikini, hata hivyo tuliweza kujenga kanisa na makazi yetu ambayo hivi sasa yamechukuliwa.

"Niliamua kujiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa siri ambako nilisoma sayansi ya jamii ili niwe mchungaji mwenye uelewa, lakini Askofu Kakobe aliposikia alisema mimi ni fisadi, akanitenga na mume wangu wa ndoa.

"Hata hivyo, mume wangu baadaye alijutia kosa, nilirudi Nzega, Askofu Kakobe aliposikia hivyo alimfukuza kazi na kutunyang'anya kila tulichokuwa nacho," alisema Mtasingwa.

Alisema Askofu Mkuu Kakobe hajawahi kuwapa Katiba waumini waione, hali iliyomfanya yeye Mtasingwa aitafute kwa udi na uvumba.

Alisema alifanikiwa kuipata na kubaini kuwa wanatakiwa kusoma ili kupambana na mafisadi.

"Ninamuomba Askofu Kakobe aache kutoa vitisho juu ya familia yetu, usalama wetu wa maisha kule Nzega ni mdogo kwani hata polisi nao hawajalichukulia uzito pamoja na kutoa taarifa," alisema.

Aliwaonya Wakristo kuacha kutangatanga makanisani kwa kudhani kuwa wanamtafuta Mungu, kwani wanaweza kukutana na mateso kama yaliyowapata.

"Wakristo simamieni wokovu, ni wewe siyo kanisa, simama ulipo usiondoke, Kakobe hata vyeti vya ndoa hatoi kutokana na ukandamizaji alionao, amebeba madaraka yote yeye mwenyewe, Kanisa limekuwa ni asasi ya kujinufaisha mwenyewe, anapoulizwa kuhusu jambo anasema hakuna kuhoji hoji," alisema.

Hii si mara ya kwanza kwa waliokuwa waumini wa Aksofu Kakobe kujitokeza hadharani kuanika udhaifu na dhuluma ndani ya Kanisa hilo.

Juhudi za kumpata Askofu Mkuu Kakobe kuzungumzia tuhuma hizi mpya zilishindikana. Muda wote simu yake ya mkononi ilipopigwa haikupokewa.

Source: Nyimbozadini.blogspot.com
 
KAKOBE ALIPULIWA - NA HERRIETH BENNY WA GAZETI LA MTANZANIA




MUUMINI wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), la Askofu Mkuu Zachary Kakobe, ameibuka na kutoa siri nzito kuhusu Kanisa hilo.

-------------------------------------

Alisema Askofu Mkuu Kakobe anatumia vitisho kuwakandamiza wachungaji wake wasijiendeleze kielimu huku akiwambia kuwa yeyote atakayekiuka sheria zake atakufa.

Kitu kingine ni kwamba wachungaji na waumini wanazuiwa kushirikiana na watu wa madhehebu mengine kwa madai kwamba ni wazinzi na makahaba.-------------


Source: Nyimbozadini.blogspot.com

This is what all other cult leaders do, when they find that their powers are dimishing they resort to killing. Many have killed followers who defect and sometimes have caused mass killings such as those witnessed in The Gate of Paradise, The Davidians, and the recent Kibwetele killings in Uganda.....
 
KAKOBE ALIPULIWA - NA HERRIETH BENNY WA GAZETI LA MTANZANIA




MUUMINI wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), la Askofu Mkuu Zachary Kakobe, ameibuka na kutoa siri nzito kuhusu Kanisa hilo.

Mtoa siri huyo ni Mchungaji Monicah Mtasingwa, ambaye pamoja na mambo mengine, ameeleza ubabe, ukiukwaji wa haki za binadamu na adha za maisha zinazowafanya wachungaji na waumini wa Kanisa waishi kwa shida.

Mtasingwa alitoa siri za Askofu Mkuu Kakobe jana alipozungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jijini Dar es Salaam.

Alisema miongoni mwa adha walizoonja kwa kuwapo kwao kwa Kakobe ni kuuza mali zao zote kwa ajili ya kuanzisha tawi la Kanisa hilo, lakini wameishia kupokwa kila kitu.

Alisema Askofu Mkuu Kakobe anatumia vitisho kuwakandamiza wachungaji wake wasijiendeleze kielimu huku akiwambia kuwa yeyote atakayekiuka sheria zake atakufa.

Kitu kingine ni kwamba wachungaji na waumini wanazuiwa kushirikiana na watu wa madhehebu mengine kwa madai kwamba ni wazinzi na makahaba.

Mtasingwa alisimulia jinsi yeye na mumewe walivyoweza kuingia katika Kanisa hilo, na kufikia hatua ya kwenda kuanzisha tawi Nzega.

"Wakati huo mume wangu alikuwa mfanyakazi wa benki, mimi nilikuwa nimemaliza kidato cha sita Msalato mkoani Dodoma, tulipofika huko tulianza kuishi maisha ya kimasikini, hata hivyo tuliweza kujenga kanisa na makazi yetu ambayo hivi sasa yamechukuliwa.

"Niliamua kujiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa siri ambako nilisoma sayansi ya jamii ili niwe mchungaji mwenye uelewa, lakini Askofu Kakobe aliposikia alisema mimi ni fisadi, akanitenga na mume wangu wa ndoa.

"Hata hivyo, mume wangu baadaye alijutia kosa, nilirudi Nzega, Askofu Kakobe aliposikia hivyo alimfukuza kazi na kutunyang'anya kila tulichokuwa nacho," alisema Mtasingwa.

Alisema Askofu Mkuu Kakobe hajawahi kuwapa Katiba waumini waione, hali iliyomfanya yeye Mtasingwa aitafute kwa udi na uvumba.

Alisema alifanikiwa kuipata na kubaini kuwa wanatakiwa kusoma ili kupambana na mafisadi.

"Ninamuomba Askofu Kakobe aache kutoa vitisho juu ya familia yetu, usalama wetu wa maisha kule Nzega ni mdogo kwani hata polisi nao hawajalichukulia uzito pamoja na kutoa taarifa," alisema.

Aliwaonya Wakristo kuacha kutangatanga makanisani kwa kudhani kuwa wanamtafuta Mungu, kwani wanaweza kukutana na mateso kama yaliyowapata.

"Wakristo simamieni wokovu, ni wewe siyo kanisa, simama ulipo usiondoke, Kakobe hata vyeti vya ndoa hatoi kutokana na ukandamizaji alionao, amebeba madaraka yote yeye mwenyewe, Kanisa limekuwa ni asasi ya kujinufaisha mwenyewe, anapoulizwa kuhusu jambo anasema hakuna kuhoji hoji," alisema.

Hii si mara ya kwanza kwa waliokuwa waumini wa Aksofu Kakobe kujitokeza hadharani kuanika udhaifu na dhuluma ndani ya Kanisa hilo.

Juhudi za kumpata Askofu Mkuu Kakobe kuzungumzia tuhuma hizi mpya zilishindikana. Muda wote simu yake ya mkononi ilipopigwa haikupokewa.

Source: Nyimbozadini.blogspot.com
Vyema sana kaka Jambazi
 
Hakuna awezaye kuthibitisha kwa pande mbili, Kama kakobe aliitenda kweli hii Familia Ajauye ni Mungu na sisi Wanadamu hatuwezi kufanya chochote, vile vile kama huyu mama amepika Majungu vile vile ajuaye ni yeye familia yake na Mungu na Malipo yake ayajua yeye awezaye kuona hata Sirini
 
Duh? Hizi ni tuhuma nzito ambazo zinapaswa kutolewa kauli na aliyetuhumuwa. kakobe ni mtumishi na kiongozi katika jamii ya watanzania, tunamwomba asijifiche kwa hili kama mtu asie na jina ndani ya jamii. Ajitokeze na kusafisha mazingira, kwani kweli ndio kitu pekee kinachoweza kumweka mtu huru.
 
Nawashauri waandishi wa habari wayasikilize mafundisho yote ya Askofu Kakobe kuhusu masuala ya ndoa na kisha wayachapishe kwenye magazeti ili kila mtanzania asome na kuhukumu. Mimi namjua vema Askofu Kakobe. Yeye anafundisha masomo bora kabisa ya ndoa. Watu wengi wanaosumbuliwa na dhambi ya uzinzi hawapendi kumsikiliza Kakobe ili wapone na kuokolewa. Namshauri huyo mchungaji kama ana madai ya kweli afungue kesi mahakamani, kuliko kumchafua mtumishi wa Mungu bila sababu ya maana. WAchungaji wa Full Gospel Bible Fellowship, wanawekwa katika utumishi kwa utaratibu maalum, huyu mwanamke alikuwa mchungaji kwa utaratibu gani wakati ana matatizo ya ndoa?
 
Wachungaji wengi wa makanisa ya kilokole huwa wanatabia ya kukamata watu ufahamu afu yeye ndo anaendesha maisha ya MTU huyo akijakujigundua akatafuta kujitoa huwawanaishia vita. Mfano leta mshahara wote , ile gari yako nipe bwana amesema, KIWANJA chako tufungue tawi la kanisa. Yani sijui wakoje ndomana unawakuta Ni matajiri sana afu waumini wao Ni masikini wa kutupwa. Afu wala hawajali Mimi imenikuta kwa Mme wangu wamkamata ufaham vizuri
 
Wachungaji wengi wa makanisa ya kilokole huwa wanatabia ya kukamata watu ufahamu afu yeye ndo anaendesha maisha ya MTU huyo akijakujigundua akatafuta kujitoa huwawanaishia vita. Mfano leta mshahara wote , ile gari yako nipe bwana amesema, KIWANJA chako tufungue tawi la kanisa. Yani sijui wakoje ndomana unawakuta Ni matajiri sana afu waumini wao Ni masikini wa kutupwa. Afu wala hawajali Mimi imenikuta kwa Mme wangu wamkamata ufaham vizuri
Hiyo mbinu mfuu iliandaliwa na CCM kupitia TBC lakini ikashindwa kama waasi wa Burundi
 
Back
Top Bottom