flagship
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 1,641
- 1,188
Ni muda mrefu kumekuwa na harakati za mabaharia wa Tanzania kupitia jumuiya yao Tanzania Seafarers Community lakini mafanikio yamekuwa ni ndoto.Lengo hasa la mabaharia ni kutambuliwa rasmi na serikali kisha kupatiwa ajira katika bandari mbalimbali.Madai ya mabaharia ni kuwa wamekamilisha kila kitu na wamepitia hatua zote lakini bado hawajapewa nafasi zaidi ya kupigwa danadana.Je kunaweza kukawa na maslahi binafsi ya wanasiasa katika jambo hili kwa kuwa sheria itawapa nguvu mabaharia kushika sehemu nyeti?