BIG Banned
JF-Expert Member
- May 4, 2012
- 262
- 71
Nilimaliza chuo miaka kadhaa iliyopita na sasa ni mhadhiri chuo kimoja hapa TZ. Ukweli ni kwamba GPA nzuri (ambayo sasa mi naiita mbaya!) ndio iliyonifanya nishawishiwe na kushawishika kubaki hapo nilipo!, Nikapata nafasi ya kwenda kusoma masters then PhD kwa takriban miaka kama 6 hivi. Tulipomaliza Undergrad kama kawaida watu/classmates tulitawanyika kila mtu kutafuta maisha kwa namna yake. Sasa kwahiyo miaka sita niliyopoteza kwa kusoma, wenzangu walibaki nchini wengine walipata kazi serikalini, wengine kampuni binafsi ambapo huko ni watu wenye vyeo na experience nzuri sana. Ukiachana na hayo ukweli ni kwamba wenzangu wapo mbali sana kimaisha kiasi kwamba nahisi mimi kama vile nilipotea au ile GPA niliyopata ndio iliniponza ingawa kwa wakati ule nilijihisi mi ndio mwenye bahati, lakini naona ni tofauti kabisa hasa nikijilinganisha na wenzangu na hiyo miiaka sita nimefanya maendeleo gani, wenzangu wana mengi sana ambayo mi ndio nafikiria kuanza.
Mbaya zaidi uhadhiri haulipi kabisa, yani ni kutegemea mshahara tu!. Na nikiangalia masenior wangu (Professors etc) hawana maendeleo yoyote, wanalia na njaa tu, wapo wanahangaika na vibiasharabiashara vidogo ambavyo kweli vinachangia kwa wahadhiri wengi kutojiandaa vizuri wanapoingia madarasani kufundisha. Maisha na heshima ya mwalimu wa chuo ni vitu viwili tofauti kabisa (sivyo vile watu wanavyofikiria)!.
Kweli uwalimu ni wito!, lakini kama hauridhiki na unachokipata na hauwezi kujikwamua na maisha magumu na majukumu ambayo unayo kila siku, kweli uwezekano wa kufunza tu ilimradi siku ziende utakuwepo tu miaka yote, sababu utakuwa unatumia muda mwingi kufanya madili mengine nje na kazi ya kufundisha.
Je ni Kweli GPA kubwa iliniponza!! Niache hii kazi nitafute nyingine!!.
Mbaya zaidi uhadhiri haulipi kabisa, yani ni kutegemea mshahara tu!. Na nikiangalia masenior wangu (Professors etc) hawana maendeleo yoyote, wanalia na njaa tu, wapo wanahangaika na vibiasharabiashara vidogo ambavyo kweli vinachangia kwa wahadhiri wengi kutojiandaa vizuri wanapoingia madarasani kufundisha. Maisha na heshima ya mwalimu wa chuo ni vitu viwili tofauti kabisa (sivyo vile watu wanavyofikiria)!.
Kweli uwalimu ni wito!, lakini kama hauridhiki na unachokipata na hauwezi kujikwamua na maisha magumu na majukumu ambayo unayo kila siku, kweli uwezekano wa kufunza tu ilimradi siku ziende utakuwepo tu miaka yote, sababu utakuwa unatumia muda mwingi kufanya madili mengine nje na kazi ya kufundisha.
Je ni Kweli GPA kubwa iliniponza!! Niache hii kazi nitafute nyingine!!.