Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,830
- 976
Salamu kwenu,
Kumekuwa na kelele nyingi kuwa ndege zetu hazina maana yoyote kwa mwananchi wa kawaida. Watu wanaenda mbali zaidi kuhoji ikiwa flyovers za Dar es Salaam zina umuhimu wowote kwa watanzania waishio vijijini, mikoani huko.
Ukiangalia hizi hoja, unapata picha mbili. Ya kwanza ni kuwa ni kweli hawajui umuhimu wake na picha ya pili ni kuwa wanajua ila wameamua kupotosha. Picha zote mbili zinao wahusika, yaani wapo wasiojua na wapo wanaojua ila wameamua kupotosha. Kwa faida ya wote tuchambue kama ifuatavyo:
Utangulizi
Kujenga uchumi imara sio kazi rahisi. Ni kazi inayohitaji weledi na uwekezaji janja (smart investment) pamoja na mazingira wezeshi kiuchumi. Kufikia uchumi mzuri sio kazi ya muda mfupi ingawa matokeo chanya yanaweza kuonekana ndani ya muda mfupi Kama miaka mitano hivi. Haya yanakuwa ni viashiria kuwa tupo kwenye mstari sahihi (right track).
Kwanini watu huona kuwa flyovers na ndege haziwasaidii chochote?
Wanadamu tuna asili flani ya ubinafsi. Unataka uone wewe Kama wewe umefaidikaje. Aidha ukiacha ubinafsi, Ni kweli kuwa kwa macho ya kawaida, mfanyakazi atataka kuona mshahara mnono, mkulima atataka pembejeo, barabara ya uhakika ya kusafirisha mazao yake na soko la uhakika. Mwanafunzi atataka elimu Bora, vifaa vya kujifunzia na mazingira bora ya kujisomea. Watu wanataka huduma bora za afya kwa kuwa na vituo vya afya karibu yao, hospitali nzuri zenye vifaa na wataalamu wa kutosha. Hivyo matarajio yao Ni hivyo vitu kutimizea, na kwa hakika hivyo ndivyo serikali inapaswa kufanya.
Kwanini flyovers na ndege ni muhimu kwa watanzania wote hata kwa wale waishio nje ya Dar es Salaam na vijijini?
1. Flyovers
Dar es Salaam ni mji wa kibiashara na ndio mji wenye watu wengi zaidi Tanzania. Dar es Salaam ndio mji iliko hospitali ya taifa. Kila siku maelfu ya magari huongia Dar es Salaam kuleta wafanyabiashara wa ndani na nje, wagonjwa walioshindikana huko mikoani, watalii hasa wa ndani na bidhaa za mashambani.
Unapokuwa na msongamano mkubwa barabarani ni kuwa unapoteza muda mrefu kupeleka bidhaa sokoni, mgonjwa hospitalini na kuwahi kazini kwaajili ya kuwahudumia watanzania. Unapoondoa kero hiyo unakuwa hujamsaidia tuu mtu aishiye Dar Bali umemsaidia mkulima aliyeleta mazao yake manzese au kariakoo aharikishe biashara yake, mgonjwa aliyetoka mkoani kuwahi hospitali na mfanyakazi kuwahi kazini. Hapa utaokoa gharama za mafuta, muda na maisha ya mgonjwa. Pia utaongeza vivutio vya utalii na kupendezesha mji.
Ndege
Ndege zinarahisha usafiri wa ndani ya nchi. Unafika popote nchini ndani ya muda mfupi. Bibi akiumwa na kuzidiwa kule ikungi, mnachangishana anaenda sehemu ndege inapotua, huyoo anawahishwa hospitalini.
Uwepo wa usafiri wa ndani was uhakika unawafahya watalii waongezeke na hivyo Kukuza pato la taifa. Kuwa na ndege yenu (national carrier) inayofanya safari za nje inachangia sana kuongeza pato la taifa kwani watalii watalipa nauli jwa fedha za kigeni ambazo zitaingia Tanzania na watalipa fedha za kigeni wanapoingia hapa kufanya utalii. Hiyo itakuza ajira nchini kwa waongoza watalii, madereva, wenye hoteli, migahawa na orodha inaendelea.
Mazingira hayo yanatengeneza kipato cha uhakika ambacho kitakuwezesha kulipa watumishi mishahara mizuri zaidi, kujenga shule nyingi zaidi zenye ubora, hospitali zenye ubora zaidi, kutoa ruzuku kwa wakulima na orodha inaendelea.
Hongera Rais Magufuli kwa kufanya uwekezaji janja, hongera CCM, hongera Tanzania. Msioelewa sasa muelewe Rais anaposema tuko kwenye right track anamaanisha Nini.
Unaweza kuona nimetaja punje tuu ya mambo yaliyofanyika yenye lengo la kutufikisha mbali kiuchumi.
Fuatilia
Ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere
Ujenzi wa barabara
Uwekezaji kwenye madini
Ununuzi wa meli na vivuko
#2020 kura yangu kwa John
Kumekuwa na kelele nyingi kuwa ndege zetu hazina maana yoyote kwa mwananchi wa kawaida. Watu wanaenda mbali zaidi kuhoji ikiwa flyovers za Dar es Salaam zina umuhimu wowote kwa watanzania waishio vijijini, mikoani huko.
Ukiangalia hizi hoja, unapata picha mbili. Ya kwanza ni kuwa ni kweli hawajui umuhimu wake na picha ya pili ni kuwa wanajua ila wameamua kupotosha. Picha zote mbili zinao wahusika, yaani wapo wasiojua na wapo wanaojua ila wameamua kupotosha. Kwa faida ya wote tuchambue kama ifuatavyo:
Utangulizi
Kujenga uchumi imara sio kazi rahisi. Ni kazi inayohitaji weledi na uwekezaji janja (smart investment) pamoja na mazingira wezeshi kiuchumi. Kufikia uchumi mzuri sio kazi ya muda mfupi ingawa matokeo chanya yanaweza kuonekana ndani ya muda mfupi Kama miaka mitano hivi. Haya yanakuwa ni viashiria kuwa tupo kwenye mstari sahihi (right track).
Kwanini watu huona kuwa flyovers na ndege haziwasaidii chochote?
Wanadamu tuna asili flani ya ubinafsi. Unataka uone wewe Kama wewe umefaidikaje. Aidha ukiacha ubinafsi, Ni kweli kuwa kwa macho ya kawaida, mfanyakazi atataka kuona mshahara mnono, mkulima atataka pembejeo, barabara ya uhakika ya kusafirisha mazao yake na soko la uhakika. Mwanafunzi atataka elimu Bora, vifaa vya kujifunzia na mazingira bora ya kujisomea. Watu wanataka huduma bora za afya kwa kuwa na vituo vya afya karibu yao, hospitali nzuri zenye vifaa na wataalamu wa kutosha. Hivyo matarajio yao Ni hivyo vitu kutimizea, na kwa hakika hivyo ndivyo serikali inapaswa kufanya.
Kwanini flyovers na ndege ni muhimu kwa watanzania wote hata kwa wale waishio nje ya Dar es Salaam na vijijini?
1. Flyovers
Dar es Salaam ni mji wa kibiashara na ndio mji wenye watu wengi zaidi Tanzania. Dar es Salaam ndio mji iliko hospitali ya taifa. Kila siku maelfu ya magari huongia Dar es Salaam kuleta wafanyabiashara wa ndani na nje, wagonjwa walioshindikana huko mikoani, watalii hasa wa ndani na bidhaa za mashambani.
Unapokuwa na msongamano mkubwa barabarani ni kuwa unapoteza muda mrefu kupeleka bidhaa sokoni, mgonjwa hospitalini na kuwahi kazini kwaajili ya kuwahudumia watanzania. Unapoondoa kero hiyo unakuwa hujamsaidia tuu mtu aishiye Dar Bali umemsaidia mkulima aliyeleta mazao yake manzese au kariakoo aharikishe biashara yake, mgonjwa aliyetoka mkoani kuwahi hospitali na mfanyakazi kuwahi kazini. Hapa utaokoa gharama za mafuta, muda na maisha ya mgonjwa. Pia utaongeza vivutio vya utalii na kupendezesha mji.
Ndege
Ndege zinarahisha usafiri wa ndani ya nchi. Unafika popote nchini ndani ya muda mfupi. Bibi akiumwa na kuzidiwa kule ikungi, mnachangishana anaenda sehemu ndege inapotua, huyoo anawahishwa hospitalini.
Uwepo wa usafiri wa ndani was uhakika unawafahya watalii waongezeke na hivyo Kukuza pato la taifa. Kuwa na ndege yenu (national carrier) inayofanya safari za nje inachangia sana kuongeza pato la taifa kwani watalii watalipa nauli jwa fedha za kigeni ambazo zitaingia Tanzania na watalipa fedha za kigeni wanapoingia hapa kufanya utalii. Hiyo itakuza ajira nchini kwa waongoza watalii, madereva, wenye hoteli, migahawa na orodha inaendelea.
Mazingira hayo yanatengeneza kipato cha uhakika ambacho kitakuwezesha kulipa watumishi mishahara mizuri zaidi, kujenga shule nyingi zaidi zenye ubora, hospitali zenye ubora zaidi, kutoa ruzuku kwa wakulima na orodha inaendelea.
Hongera Rais Magufuli kwa kufanya uwekezaji janja, hongera CCM, hongera Tanzania. Msioelewa sasa muelewe Rais anaposema tuko kwenye right track anamaanisha Nini.
Unaweza kuona nimetaja punje tuu ya mambo yaliyofanyika yenye lengo la kutufikisha mbali kiuchumi.
Fuatilia
Ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere
Ujenzi wa barabara
Uwekezaji kwenye madini
Ununuzi wa meli na vivuko
#2020 kura yangu kwa John