Je, ni kweli 3,000,000/= ni kubwa kwa kulipia Mahari tu?

Lugumgya

JF-Expert Member
Dec 10, 2019
629
1,997
Ilikuwa juzi mida ya saa 2 usiku nikapokea simu kutoka kwa Mdogo wangu, akiniuuliza swali hilo! Yaani M 3 si kama nanunua? Why all that amount? Nahisi hawataki labda nimuoe! Au nimchukue bila kutoa chochote and the girl is ready! Kaka hivi kweli jamani? M.3? Anaendelea kulalamika! Baada ya malalamiko yake nikamwambia Mdogo wangu sikiliza!

Unampenda? Unamuelewa? Yuko tayari kwa ajili yako? Uko tayari ajili yake? Yote alinijibu ndiyo! Una uhakika na hisia zenu, au ni mihemko? Nina hakika brother! Huo uhakika umeupataje? Hujawahi kupendana na mtu Kama mlivyopendana na huyu afu Mwisho wa siku mkaachana? Iliwahi kutokea!

Alivyoondoka uliumia au hukuumia? Niliumia! Ulikuwa umeshamtolea Mahari kiasi gani? Nilikuwa sijamtolea! Kwanini uliumia? Nilikuwa nampenda!

Mdogo Wangu, kutoa mahari hata kama ni elfu 10 au 500 au Milioni 3 si kununua ni utaratibu tuliyoukuta! Hata mama alitolewa ng' ombe 12, miaka ya 80 ambayo ni thamani kubwa kuliko hiyo Milioni 3 yako! Milioni 3 is just fair for a wife! Siyo nyingi Mdogo wangu! Labda Kama hauna! Kama ndo waliyokubaliana na wajumbe uliyowatuma, haina shida.

Brother hapana, mtu mwenyew hana kazi atakuwa anategemea kila kitu kutoka kwangu! Nikacheka kidogo! Kazi anazo sema aliyemwajili atakuwa hamlipi Mshahara! Atafua, atapika, atanyoosha nguo zenu, atadeki, atasimamia malezi na makuzi ya Watoto, atatandika kitanda, atakuhudumia ukiugua, atawahudumia ndugu zako, atakupa sex ambayo wengine wanaitolea hadi magari ( japo zipo na za bure) nk. Ukiajili mtu akufanyie hayo yote miezi kadhaa tu, hiyo Milioni 3 itakuwa imeisha, na bado utakuwa huna mke! Yeye atafanya hizo kazi bure kabisa! Hutalazimika kumtumia nauli Pamoja na ya kutolea ili muonane! Hivyo, hiyo itakuwa ni Shukrani tu kwa wazazi, ni vibaya tu kwamba jamii iliweka utaratibu wa wazazi wa mke kujipangia Shukrani! Lakini kwangu M 3 kwa ajili ya mke is just okay!

Nikaendelea, Mdogo wangu, unakumbuka jinsi Mzee wetu alivyoamua kwenda kutafuta akatuacha Mimi Kaka yenu na mama? Unakumbuka jinsi mama alivyosimama imara kusimamia elimu yetu? Hakuwa na kazi ya ofisini lkn alikuwa na akili na Nguvu! Kama huyo mke wako mtarajiwa ana akili na Nguvu basi M.3 si kitu! Unakumbuka mama alivyofanya vibarua, mkawa mnaniletea unga na shilingi elfu 3 kila mwezi kule shule ya Sekondari kijijini Nyangalagata? Unakumbuka mama alivyowaongoza? Labda ndo maana baba alitoa Ng'ombe 12, aliiona thamani yake! Na wew Kama umeiona hiyo thamani, nitakuunga mkono! Lakini kama huioni thamani hiyo kwake, then M.3 unaporwa bila kupigwa ngeta! Ni Kama kibaka anachukua hiyo hela yako mbele ya Simon Nyankoro Sirro au Alphonce Mabeyo!

Akasema brother naona Kama yuko vizuri! Nikamwambia sawa Mdogo wangu! Kama yuko vizuri, haina shida!

Mdogo wangu mwanamke ni mtu muhimu Sana katika katika maisha yetu na Ustawi wa familia yoyote ile. Kwa hiyo kumlinganisha na kitu Kama M. 3 ni kumkosea heshima! Hiyo kazi inayokufanya uwe na uwezo wa kulipia M .3 imetokana na usimamizi wa mama, baba angeona Ng'ombe 12 ni wengi kwa ajili ya mama, mm na wew labda tusingekuwa na hali tuliyonayo leo! Lakini mama ndo alituombea, alitumia Nguvu zake kutosomesha, akasimamia maadali yetu, akawa mshauri wetu na mfariji wetu Mkuu! Hadi Leo tukienda kijijini kwetu napo panaonekena! Wew unaona M.3 zina thamani kubwa kuliko majukumu ya mwanamke katika familia!?

Japo si lazima utoe hela ndo afanye hayo, hata bure tu anaweza kufanya, washukuru wazazi wake kwa hicho walichoona wanastahili afu mjenge familia katika Imani na upendo! Niko Pamoja na wewe Mdogo wangu! Tarajia kheri!

Je, nimemshauri vibaya? Kama nyie ndo mngekuw kwenye nafasi yangu mngesemaje? M.3 ni nyingi kwa ajili ya mahari ya Mwanamke?

Lugumya!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Million tatu unanunua nini?huyo aliyeambiwa mahari kiasi hiko kimaisha amejijenga kwa kiasi gani?ana nyumba miradi kadhaa itakayomfanya aweze ku-survive vyema na huyo mke anayetoa mahari kubwa hivyo kumuowa?

Maana itakuwa kituko kama atajikaza atoe hiyo pesa kisha achukue mke wakaishi kwenye chumba cha kupanga na kurudi kumtumikia mwajiri wake,ktk watakaoanza kumcheka ndugu wa mke pia wapo tena ndo watakaokuwa wa kwanza kumdharau

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Nimeshashuhudia hv karibuni ndoa km 4, na zote mahari ni milioni 3 na kuendelea na wanatoa vzr kiroho safi kabisa.

Haumnunui yule mtu lkn ni kitu ambacho tumekikuta ktk jamii zetu km shukrani kwa kulelewa huyo binti mpk umri huo na ukamuona ukataka kumuoa. Mana anayoenda kukufanyia ni bora sana.

Mtu muelewa na anazo anatoa tu. Wanaolia lia ndo hao wasiojiweza na hawana uelewa huyo binti mpk anamuona na kumtamani bs ametunzwa na kulelewa vzr na wazazi wake. Atoe achukue mke huyo aache kusita sita.
 
Vijana wengi wa sasa wanahitaji kaka kama wewe.
Mimi ni mwanamke na nilitolewa mahari.
Ilikua juu kidg ya hiyo 3m japo sikupenda ila ni utamaduni...Sikupenda kwasababu naona saa nyingine ni kama kumkomoa "bwana harusi" kwasababu mbali na mahari anajukumu kubwa la kugharamikia harusi despite kwamba anapata michango. Harusi ina gharama
Ila mahari kubwa pia itafanya mtu amthamini na kumpenda mkewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ningemwambia waongezee zingine 7 angalau maana hata wewe unakiri kuwa binti yao yuko vizuri.
Na usiache kuwashukuru kila upatapo nafasi.
 
Wew ungeshauri afanyeje Kaka! Hapa tunasaidiana mawazo! Wew Kama hujaoa hukiambiwa hivyo, ukiwa hujajenga na unamtumikia mwajiri wako utafanyaje? Pia ahsante kwa maswali yako fikirishi!
Million tatu unanunua nini?huyo aliyeambiwa mahari kiasi hiko kimaisha amejijenga kwa kiasi gani?ana nyumba miradi kadhaa itakayomfanya aweze ku-survive vyema na huyo mke anayetoa mahari kubwa hivyo kumuowa?

Maana itakuwa kituko kama atajikaza atoe hiyo pesa kisha achukue mke wakaishi kwenye chumba cha kupanga na kurudi kumtumikia mwajiri wake,ktk watakaoanza kumcheka ndugu wa mke pia wapo tena ndo watakaokuwa wa kwanza kumdharau

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati nataka kuoa nkamwambia mchumba wangu nataka kuja kutoa mahali kwenu.
Nikamwambia hela nliyonayo haizidi laki 5, kwahiyo wapange kabisa ndugu zako na uwaeleze hali halisi.

Na nikampa msimamo kwamba wakipanga hela zaidi ya hii niliyonayo mimi sitatoa na itabidi tuachane, sasa wewe kama hutaki nikuoe zubaa

Kesho yake alimpigia babaake mdogo akamweleza huku analia, babaake akamwambia mwambie aje tu haina shida.

Tulipoenda wakakomaa eti tutoe milioni 2. Mimi nikamwambia mshenga wangu tuondokeni. Tulipoanza kuondoka acha binti aangue kilio.

Wakatuita tukaongea ongea wakasema tutoe milion 1.2, tukawambia sawa tukawapa ile laki 5 hizo zilizo baki ntawapa nikifisha utajiri kama wa Billget, na afterall mahali huwa haiishi.

Binti ana nafasi kubwa sana ya kukomaa ili utoe mahali kidogo maana ile siyo bidhaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante kwa busara zako hizi Mkuu! Baadhi ya Comments ni nitakuwa namsukumia! Aone jinsi waungwana wanavyonena juu ya hiyo ishu yake!
Nimeshashuhudia hv karibuni ndoa km 4, na zote mahari ni milioni 3 na kuendelea na wanatoa vzr kiroho safi kabisa. Haumnunui yule mtu lkn ni kitu ambacho tumekikuta ktk jamii zetu km shukrani kwa kulelewa huyo binti mpk umri huo na ukamuona ukataka kumuoa. Mana anayoenda kukufanyia ni bora sana. Mtu muelewa na anazo anatoa tu. Wanaolia lia ndo hao wasiojiweza na hawana uelewa huyo binti mpk anamuona na kumtamani bs ametunzwa na kulelewa vzr na wazazi wake. Atoe achukue mke huyo aache kusita sita.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeshashuhudia hv karibuni ndoa km 4, na zote mahari ni milioni 3 na kuendelea na wanatoa vzr kiroho safi kabisa. Haumnunui yule mtu lkn ni kitu ambacho tumekikuta ktk jamii zetu km shukrani kwa kulelewa huyo binti mpk umri huo na ukamuona ukataka kumuoa. Mana anayoenda kukufanyia ni bora sana. Mtu muelewa na anazo anatoa tu. Wanaolia lia ndo hao wasiojiweza na hawana uelewa huyo binti mpk anamuona na kumtamani bs ametunzwa na kulelewa vzr na wazazi wake. Atoe achukue mke huyo aache kusita sita.
Kwa taarifa yako ni kwamba wenye vihele hele mpaka ile mahali inakuwa kubwa wala siyo wazazi ila utakuta ni mashangazi na wajomba, na ndio huwa wanakula ile hela
Huku wazazi wakiambulia kitu kidogo tu. Chunguza utaona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa ahsante! Japo wapo ambao hawajatoa hata kumi ila wanawapenda wake zao kushinda waliotoa mamilioni
Vijana wengi wa sasa wanahitaji kaka kama wewe.
Mimi ni mwanamke na nilitolewa mahari.
Ilikua juu kidg ya hiyo 3m japo sikupenda ila ni utamaduni...Sikupenda kwasababu naona saa nyingine ni kama kumkomoa "bwana harusi" kwasababu mbali na mahari anajukumu kubwa la kugharamikia harusi despite kwamba anapata michango. Harusi ina gharama
Ila mahari kubwa pia itafanya mtu amthamini na kumpenda mkewe

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ili inabidi tuliingize kwenye Customary law na ile Sheria ya ndoa! Maana hata sisi mpaka tunafikia hatua hii Kuna watu wamehusika! Ikibid twende kihindi!
Mwanaume anaeamua kumuoa huyo msichana nae wazazi wake walipwe kwani amepunguza gharama ya maisha nyumbani kwa msichana . Kwa kifupi mahari zitoke pande mbili .

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Aisee kamilisha deni Mkuu!
Wakati nataka kuoa nkamwambia mchumba wangu nataka kuja kutoa mahali kwenu.
Nikamwambia hela nliyonayo haizidi laki 5, kwahiyo wapange kabisa ndugu zako na uwaeleze hali halisi.

Na nikampa msimamo kwamba wakipanga hela zaidi ya hii niliyonayo mimi sitatoa na itabidi tuachane, sasa wewe kama hutaki nikuoe zubaa

Kesho yake alimpigia babaake mdogo akamweleza huku analia, babaake akamwambia mwambie aje tu haina shida.

Tulipoenda wakakomaa eti tutoe milioni 2. Mimi nikamwambia mshenga wangu tuondokeni. Tulipoanza kuondoka acha binti aangue kilio.

Wakatuita tukaongea ongea wakasema tutoe milion 1.2, tukawambia sawa tukawapa ile laki 5 hizo zilizo baki ntawapa nikifisha utajiri kama wa Billget, na afterall mahali huwa haiishi.

Binti ana nafasi kubwa sana ya kukomaa ili utoe mahali kidogo maana ile siyo bidhaa

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom