Je, ni kwanini Waafrika hatukemei uvunjifu wa amani na fujo za Kidemokrasia zinazoendelea sasa Marekani?

Hivi kinachofanywa na Utawala wa Rais Trump Fujo na Ukatili wa Kidemokrasia huku Kwetu Afrika hatuyaoni? Kwanini tumelinyamazia hili la sasa?
Wao walikwisha mchukulia hatua, alichokifanya, kwetu ingekuwa ni amri ya Rais!
Twitter nayo imemfungia kabisakabisa akaunti yake! Huku mtandao ungezimwa ili tusishutumu!
 
Pamoja na "MATAGA" wa marekani kuandamana wakitaka bwana "TRUMP" asalie madarakani pamoja na kushindwa, ila hujasikia IGP wakule akisema watapigwa kipigo cha mbwa koko, makamo wa raisi Mike Pence yani mama Samia Suluhu Wakule kasema "MATAGA" hao wanaiaibisha MAREKANI.
Ccm na vibaraka wenu mna la kujifunza.
Kule polisi huwa Hawaii matamko wanapiga na kuua tu si umeona waluvyopiga na kuwa bila kutoa tamko?
 
Kuna mtaalamu mmoja ambaye amefanya utafiti wa miaka kumi anaezea kuwa LIBERAL DEMOCRACY ni ndoto ya binadamu yeyote lakini ni ndoto ambayo haiwezi kufikiwa.

Na sababu anazotowa ni kuwa kwa kila binadamu kufanya kinacho mpendeza bila kumkwaza mwenzako ni kutengeneza fujo ambayo bado dawa yake hajapatikana.

Unapo amua kufanya ulicho kichagua, hapo ndipo mwanzo wa kumkwaza mwenzako. Sio rahisi ukipendacho wewe kikapendwa na wenzako, vile vile na wao. Kwa hiyo anashauri dunia izungumzie na kutekeleza democracy tuu na sio democracy huria ya wote( liberal democracy ).
 
Kama urusi ilianguka na kugawika vipande vipande na hizo za marekani nazo ni dalili tosha za ukaskazini na ukusini wa tanzania.
 
Kuna tofauti kubwa kati ya maandamano ya CHADEMA na Yale ya wafuasi binafsi wa trump
 
watetezi wa demokrasia wakina lissu na amsterdam nasubiri watoe tamko la kuwawekea vikwazo vya kiuchumi marekani
Marekani haiwezi wekewa vikwazo,huoni ilivyoshughulika na upambavu waTrump kumwonyesha kuwa yeye siyo Marekani bali Marekani ni wananchi umevurunda nenda kasimamie biashara zako siyo sisi Wamarekani.
 
Kuna mtaalamu mmoja ambaye amefanya utafiti wa miaka kumi anaezea kuwa LIBERAL DEMOCRACY ni ndoto ya binadamu yeyote lakini ni ndoto ambayo haiwezi kufikiwa.

Na sababu anazotowa ni kuwa kwa kila binadamu kufanya kinacho mpendeza bila kumkwaza mwenzako ni kutengeneza fujo ambayo bado dawa yake hajapatikana.

Unapo amua kufanya ulicho kichagua, hapo ndipo mwanzo wa kumkwaza mwenzako. Sio rahisi ukipendacho wewe kikapendwa na wenzako, vile vile na wao. Kwa hiyo anashauri dunia izungumzie na kutekeleza democracy tuu na sio democracy huria ya wote( liberal democracy ).
Hiyo ni sahihi;

Binafsi naona kwa nature ya mwanadamu ni vigumu Sana kupractice democracy,

Yaani kumuacha mtu ajiamulie tu mambo yake itazua taharuki.
 
Hivi kinachofanywa na Utawala wa Rais Trump Fujo na Ukatili wa Kidemokrasia huku Kwetu Afrika hatuyaoni? Kwanini tumelinyamazia hili la sasa?

US ina taasisi imara za kuweza kufutilia mbali huo uhuni.
 
Hivi kinachofanywa na Utawala wa Rais Trump Fujo na Ukatili wa Kidemokrasia huku Kwetu Afrika hatuyaoni? Kwanini tumelinyamazia hili la sasa?
Acha ujinga wewe, Uganda wametawanyika wangapi in maana unathamini USA kuliko hapa jirani?
 
tufanye kama sisi tumeshindwa kukemea kwa sababu hatujui demokrasia, je nyie watetezi wa demokrasia kweli mko wapi kukemea uovu unaofanyika kule, wapi wakina amsterdam, wapi kina lissu, wakina sarungi wako wapi kukemea????? nadhan jibu mnalo, hapa ndo pale tunapowaimbia upinzani hii nchi ni makapuku akilini nadhan kinaeleweka sasa
Aliyetaka kuchezea demokrasia kadhibitiwa, sasa wapinzani wakemee nini? Hapa kuna kelele maana ccm ndio kaibaka demokrasia na kaweza kujitangaza kibabe, ndio maana kuna kelele.
 
Hivi kinachofanywa na Utawala wa Rais Trump Fujo na Ukatili wa Kidemokrasia huku Kwetu Afrika hatuyaoni? Kwanini tumelinyamazia hili la sasa?
Taratibu za kidemokrasia zilizowekwa ndani ya katiba ya Marekani zitamuondoa bila shida. "No need for external intervention".
 
Aliyetaka kuchezea demokrasia kadhibitiwa, sasa wapinzani wakemee nini? Hapa kuna kelele maana ccm ndio kaibaka demokrasia na kaweza kujitangaza kibabe, ndio maana kuna kelele.

hatimae wakaondoka sehem ambapo hakuna demokrasia wakaenda sehem ambapo kuna demokrasia wakiwa na viapo vya kutetea demokrasia kokote duniani, ukianza na yule mbabu na mke wake lissu, nadhan walisema tanzania wawekewe vikwazo vya uchumi sasa ni zam ya marekani kuwekewa vikwazo vya uchumi
 
hatimae wakaondoka sehem ambapo hakuna demokrasia wakaenda sehem ambapo kuna demokrasia wakiwa na viapo vya kutetea demokrasia kokote duniani, ukianza na yule mbabu na mke wake lissu, nadhan walisema tanzania wawekewe vikwazo vya uchumi sasa ni zam ya marekani kuwekewa vikwazo vya uchumi
Itawekewa na magufuri labdda.
 
vp wale mabinti wawili wa belgium wanaojiita wasemaji wa dunia, si ndo wako concerned sana na demokrasia ya hii dunia ama hiki kikombe kiwaepuke
Marekani haiwezi wekewa vikwazo,huoni ilivyoshughulika na upambavu waTrump kumwonyesha kuwa yeye siyo Marekani bali Marekani ni wananchi umevurunda nenda kasimamie biashara zako siyo sisi Wamarekani.
 
vp wale mabinti wawili wa belgium wanaojiita wasemaji wa dunia, si ndo wako concerned sana na demokrasia ya hii dunia ama hiki kikombe kiwaepuke
Hakuna binti pale labda wewe unataka uolewe nao ushamba na ujinga vitakutesa sana.
 
Back
Top Bottom