Je, ni kwanini malori yanafurika Zambia highway ilihali TAZARA cape gauge railway ipo?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,059
40,723
Leo nilikuwa naelekea Kigamboni kupitia daraja la Nyerere, baada ya kuvuka nilipita ile njia ya kushoto inayopitia jeshini, kabla sijaingia kwenye kile kipande cha lami hapo katikati kulikuwa na malori ya mafuta (fuel tankers) takriban 350 yamepaki yakisubiri kupakia mafuta kwa ajili ya kusafirisha sehemu mbalimbali mikoani na hata nje ya nchi.

Sasa nikajiuliza, baada ya hii SGR itakayogharimu kiasi cha jasho la walipa kodi bilioni elfu saba (bilioni 7,000) za kitanzania, yaani bilioni ziwe 100, alafu ziwe mara 10 yake, alafu ziwe mara saba. (7,000,000,000,000/=) kukamilika si itabidi haya maelfu kwa maelfu ya malori yanayosafirisha mafuta kwenda mikoa mbalimbali nchini pamoja na nchi za nje yapaki au yatafute shughuli mbadala kama kubeba maji safi, au hata kupakua/kunyonya vyoo vilivyo jaa, au hata kukata screpa, au hata kuuza tu.

Sasa kwakua wamiliki wa hivi vituo vya mafuta (waarabu koko) ndani na nje ya nchicndio hawa hawa wanaomiliki haya malori, je, watakubali kupaki malori yao kwa hiari yao halafu waende kutumia SGR? Mfano labda lori lake linalopeleka mafuta Mwanza lisafiri tupu hadi Dodoma kusubiri treni ya SGR ikifika ndio wafaulishe halafu ndio apeleke hayo nafuta hadi Mwanza (double handling), je, atakubali kwa hiari yake kuacha kutumia malori yake na badala yake atumia SGR?

Kuna uzi ulikuwepo hapa na niliuliza swali hili bila kupewa majibu. JE, NI KWANINI MALORI YANAFURIKA ZAMBIA HIGHWAY ILIHALI TAZARA CAPE GAUGE RAILWAY IPO? JE, NI KWANINI WAFANYABIASHARA WANAIKWEPA? NA JE, NINI KITABADILIKA KIASI HAWA HAWA WAFANYABIASHARA WASIIKWEPE SGR?

 
Trilioni saba ndio zinateketea hivi hivi huku watz wenye akili timamu wakichekelea tu.
If you spread costs of Bil 7000/100yrs you will get Bil 70 per year!
If you spread Mil 70,000/1000 km = Mil 70 per km/yr which is equivalent to 70mil per Km/12 months =5.2milion/km/month which is equivalent to Tsh 170,000 per Km/ day.
This is the cost of constructing SGR per km per yr/ month/ day as per simple estimation.
I leave u to calculate benefit per day, month or year.
 
Nilisoma mahali wakati ulaya wanaanza kutengeneza magari, hofu za usalama, kupoteza ajira, gharama, kumaliza madini chuma zilikuwa zimesambaa sambamba na mipango na maandamo kuzuia isiendelee.
Ni kawaida kuogopa mabadiliko.

Hili la SGR si jipya. Mtoa mada anajaribu kuturudisha tuone tulijikwaa wapi. Wakati reli hizi zilizopo zilikuwa zinajengwa changamoto kubwa ilikuwa barabara. Kusafirisha mizigo kwa njia ya barabara ilikuwa hatari na gharama.Huduma za reli kwa uhakika wa soko ziligeuka ukiritimba na kero. Polepole usalama ukaanza kushuka. Leo, barabara nzuri na usalama si tatizo watu wakachagua barabara, reli zikabaki kwa maskini na watalii.

Na sasa kuna watu wengi wanatengeneza mamilioni kwa biashara hii. Wako wengi walioajiriwa huko.
Serikali inaweza ikatoa mwelekeo kama itakuwa tayari kuwatosa wafadhili wao kuweka sera wezeshi kwa reli au kuweka usafiri wa reli kuwa bora na nafuu kuvutia wateja.

Anko anaweza, tatizo hata fuata taratibu za sera kwa hiyo akiondoka mambo yatakuwa yale yale. Hapa wamarekani ndo walipotupiga bao, ingawaje nao wanapata marais wa hizi style lakini si rahisi kubadilisha kila kitu na ndio maana JFK alianzisha mradi wa NASA kwenda mwezini ila walienda yeye akiwa tayari karudisha namba.
 
Nilisoma mahali wakati ulaya wanaanza kutengeneza magari, hofu za usalama, kupoteza ajira, gharama, kumaliza madini chuma zilikuwa zimesambaa sambamba na mipango na maandamo kuzuia isiendelee.
Ni kawaida kuogopa mabadiliko.

Hili la SGR si jipya. Mtoa mada anajaribu kuturudisha tuone tulijikwaa wapi. Wakati reli hizi zilizopo zilikuwa zinajengwa changamoto kubwa ilikuwa barabara. Kusafirisha mizigo kwa njia ya barabara ilikuwa hatari na gharama.Huduma za reli kwa uhakika wa soko ziligeuka ukiritimba na kero. Polepole usalama ukaanza kushuka. Leo, barabara nzuri na usalama si tatizo watu wakachagua barabara, reli zikabaki kwa maskini na watalii.

Na sasa kuna watu wengi wanatengeneza mamilioni kwa biashara hii. Wako wengi walioajiriwa huko.
Serikali inaweza ikatoa mwelekeo kama itakuwa tayari kuwatosa wafadhili wao kuweka sera wezeshi kwa reli au kuweka usafiri wa reli kuwa bora na nafuu kuvutia wateja.

Anko anaweza, tatizo hata fuata taratibu za sera kwa hiyo akiondoka mambo yatakuwa yale yale. Hapa wamarekani ndo walipotupiga bao, ingawaje nao wanapata marais wa hizi style lakini si rahisi kubadilisha kila kitu na ndio maana JFK alianzisha mradi wa NASA kwenda mwezini ila walienda yeye akiwa tayari karudisha namba.
Mchango mzuri sana, thanks. Sasa kama barabara kua nzuri na usalama kuimarika barabarani kunafanya wafanya biashara kuchagua barabara badala ya reli, nini kitakachobadilika sasa kitakachofanya wachague SGR badala ya barabara? Mtaondoa usalama barabarani? Mtaharibu barabara ili wahamie SGR?
 
Mchango mzuri sana, thanks. Sasa kama barabara kua nzuri na usalama kuimarika barabarani kunafanya wafanya biashara kuchagua barabara badala ya reli, nini kitakachobadilika sasa kitakachofanya wachague SGR badala ya barabara? Mtaondoa usalama barabarani? Mtaharibu barabara ili wahamie SGR?
Hakuna uharibifu wowote utatokea, zaidi ya discouraging those old means of transportation through expensive tax whilst minimising the sgr costs.
Plenty routes not connected to sgr consumes oil and the rate of consumption will forever enlarge.
So be a lit more great thinker, surely Jf has become home of nyumbus
 
ukiondoa chuki moyoni utapata jibu kirahisi sana. hakuna mfanya biashara atatumia njia yenye gharama kubwa ikiwa yenye nafuu ipo hata kama ni magari yake inakua anajiongezea gharama.
nakubaliana na wewe kua uchukuzi wa treni ni bora kwa masafa marefu mfano mafuta kutoka depo mpaka depo gharama inaweza kuwa < 50% ya gharama za malori pia chukulia uharibufu wa mazingira na barabara unaofanywa na malori. Lakini uongozi mbaya umefanya hizi reli za tazara na reli ya kati karibu zife na hazitoi huduma ipasavyo
 
Hakuna uharibifu wowote utatokea, zaidi ya discouraging those old means of transportation through expensive tax whilst minimising the sgr costs.
Plenty routes not connected to sgr consumes oil and the rate of consumption will forever enlarge.
So be a lit more great thinker, surely Jf has become home of nyumbus
Ni kwanini hayo hayafanyiki sasa hivi kwa case ya TAZARA? i.e " discouraging old means of tranport through expensive tax whilst minimizing the TAZARA costs"?
 
ukiondoa chuki moyoni utapata jibu kirahisi sana. hakuna mfanya biashara atatumia njia yenye gharama kubwa ikiwa yenye nafuu ipo hata kama ni magari yake inakua anajiongezea gharama.
nakubaliana na wewe kua uchukuzi wa treni ni bora kwa masafa marefu mfano mafuta kutoka depo mpaka depo gharama inaweza kuwa < 50% ya gharama za malori pia chukulia uharibufu wa mazingira na barabara unaofanywa na malori. Lakini uongozi mbaya umefanya hizi reli za tazara na reli ya kati karibu zife na hazitoi huduma ipasavyo
Kwahiyo uongozi mbaya wa TAZARA ndio unafanya wafanyabiashara waikwepe TAZARA CGR na kutumia barabara? Fafanua ni kipi ambacho uongozi mzuri wa SGR ya Dodoma utafanya ambacho huu uongozi 'mbovu' wa TAZARA CGR haufanyi.
 
Na kwa ukimya huu, na kwa kutokujua kwanini wafanyabiashara wanaikwepa TAZARA, basi nina hakika baada ya SGR kukamilika, wafanyabiashara wataendelea kuikwepa SGR kama wanavyoikwepa TAZARA na bado hatutakuwa na la kufanya zaidi ya kulalamikia haya
1.) Uongozi mbovu cc: Percival
2.) Usalama na ubora wa barabara cc:double R
 
Leo nilikuwa naelekea Kigamboni kupitia daraja la Nyerere, baada ya kuvuka nilipita ile njia ya kushoto inayopitia jeshini, kabla sijaingia kwenye kile kipande cha lami hapo katikati kulikuwa na malori ya mafuta (fuel tankers) takriban 350 yamepaki yakisubiri kupakia mafuta kwa ajili ya kusafirisha sehemu mbalimbali mikoani na hata nje ya nchi.

Sasa nikajiuliza, baada ya hii SGR itakayogharimu kiasi cha jasho la walipa kodi bilioni elfu saba (bilioni 7,000) za kitanzania, yaani bilioni ziwe 100, alafu ziwe mara 10 yake, alafu ziwe mara saba. (7,000,000,000,000/=) kukamilika si itabidi haya maelfu kwa maelfu ya malori yanayosafirisha mafuta kwenda mikoa mbalimbali nchini pamoja na nchi za nje yapaki au yatafute shughuli mbadala kama kubeba maji safi, au hata kupakua/kunyonya vyoo vilivyo jaa, au hata kukata screpa, au hata kuuza tu.

Sasa kwakua wamiliki wa hivi vituo vya mafuta (waarabu koko) ndani na nje ya nchicndio hawa hawa wanaomiliki haya malori, je, watakubali kupaki malori yao kwa hiari yao halafu waende kutumia SGR? Mfano labda lori lake linalopeleka mafuta Mwanza lisafiri tupu hadi Dodoma kusubiri treni ya SGR ikifika ndio wafaulishe halafu ndio apeleke hayo nafuta hadi Mwanza (double handling), je, atakubali kwa hiari yake kuacha kutumia malori yake na badala yake atumia SGR?

Kuna uzi ulikuwepo hapa na niliuliza swali hili bila kupewa majibu. JE, NI KWANINI MALORI YANAFURIKA ZAMBIA HIGHWAY ILIHALI TAZARA CAPE GAUGE RAILWAY IPO? JE, NI KWANINI WAFANYABIASHARA WANAIKWEPA? NA JE, NINI KITABADILIKA KIASI HAWA HAWA WAFANYABIASHARA WASIIKWEPE SGR?
Hapa nilivyokuelewa ni kwamba hakuna sababu ya kutumia mabilion na mabilioni kwa sababu ya kujenga reli
Wakati reli tu ambayo ipo haitumiki ipasavyo
Sasa swali je kwani reli ni kwaajili ya kubeba tu mafuta??
 
Hapa nilivyokuelewa ni kwamba hakuna sababu ya kutumia mabilion na mabilioni kwa sababu ya kujenga reli
Wakati reli tu ambayo ipo haitumiki ipasavyo
Sasa swali je kwani reli ni kwaajili ya kubeba tu mafuta??
Kwani ni nani amesema kwamba malori yanayofurika Zambia highway ni ya mafuta tu? Nimetolea mfano malori ya mafuta ila malorry ya macontainer yanayofurika Zambia highway ni mengi kuliko ya mafuta. Nimetolea mfano tu. Na ndio maana swali limesema 'malori', na sio 'malori ya mafuta'. Pia sijasema hakuna haja ya kujenga nyingine wakati iliyopo haitumiki,infact sisemi bali nauliza hivi;
NI KWANINI MALORI YANAFURIKA ZAMBIA HIGHWAY ILIHALI TAZARA CAPE GAUGE RAILWAY IPO? JE, NI KWANINI WAFANYABIASHARA WANAIKWEPA? NA JE, NINI KITABADILIKA KIASI HAWA HAWA WAFANYABIASHARA WASIIKWEPE SGR?

JIKITE KWENYE SWALI.
 
Back
Top Bottom