Je, ni kampuni ipi inaongoza kwa huduma bora za kuagiza magari ya nje hapa Tanzania

Mr. MTUI

JF-Expert Member
Feb 18, 2013
8,130
8,329
Wajuzi tafadhali mtuambie nataka kufanya uwamuzi,

Nafahamu kuna kampuni kadhaa za uagizaji magari hapa nchini zikiwemo Beforward, autocom Japan, Sbt n.k. Naomba wajuzi mtuambie kampuni ipi ni nzuri ukiitumia katika kuagiza magari.

Tafadhali lenga katika nyanja zifuatazo kama una experience mbaya ni vyema pia ukatuambia.
1. Huduma bora kwa wateja/ customer service
2. Uharaka wa kufika kwa magari.
3. Bei nafuu
4. Uhakika na usalama wa transactions.
5. Magari yenye quality nzuri.
 
Mbona uzi umekimbiwa?
Habari Mr. Mtui, ikiwa utakua na amani, unaweza kunitumia Mimi (ecarstanzania) japo ni kampuni changa na inayo chipukia.


Sitaki kujiongelea zaidi na hata kuhusu vigezo ulivyoweka maana naweza kuonekana najifagilia, ila naomba nifanye kwa vitendo nawe utanipa "maksi"


Karibu!
 
Nimewahi kuagiza gari kupitia Beforward mwaka 2015 , walinihudumia vizuri kiasi fulani, ila bei nilikuja kugundua kuwa wamenipiga nilipolinganisha na kampuni zingine kwa gari husika.
 
Msisahau Instagram pia, wana service nzuri sana ya kuuza magari yaliyochakaa ya washikaji. Mtu kanunua gari miaka 10 iliyopita kwa milioni 4, anaiuza kwa milioni 6 ili apate faida wakati gari limechoka kishenzi. Wabongo kwa biashara uchwara, kwa kweli hawajambo.
Na mm nmeliona pia..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom