Je, ni ipi picha inayofanana na Yesu Kristo Mnazareti?

Yesu hakuwahi kupiga picha
Wakati ule kulikiwa na utaalam wa kuchora picha ya mtu; nafikiri katika makabrasha ya kumbukumbu lazima kuna picha halisi ya Yesu ( iliyochorwa).
Hatuna uhakika kama Yesu alikuwa mtu mweupe ama Mweusi, kweli technologia kipindi kile ilikuwa bado mno.
 
Uongo tu watu wa dini ili kutengeneza kipato kama wale wanaozungusha misaraba na sanamu la uongo ati ni Yesu wakichangisha mamilioni ya pesa kwa kuwahadaa waumini eti sanamu likifika ndani kwako unapata mibaraka
imani yako ndiyo itakayo kuponya
 
Swalo la kipumbavu kabisa. Enzi za Yesu hakukuwa na Camera. Hamna hata picha moja inayofanana na Yesu maana hakuwahi piga picha. Usiwe unauliza stupid questions

Kumekuwepo mitazamo kinzani ya miaka mingi juu ya muonekano halisi wa Yesu Kristo, Mnazareti, Masihi na Mwana wa Mungu (katika perspective ya kikristo).
Kutokana na Yesu kuzaliwa katika enzi za ustaarabu wa Kigiriki na Utawala wa Roma, machapisho ya Biblia na maisha ya Yesu Kristo, yalikuwa katika mitazamo ya Kizungu zaidi na siyo Kiyahudi kutokana na Dini hiyo mpya ya Kikristo kuenea kwa kasi katika Nchi za Uturuki, Ugiriki na Roma kwenye Karne ya Kwanza AD, licha ya Dini hiyo kudharaulika kwa Wayahudi.
Wakristo wengi wamekuwa wakidhani kuwa, muonekano wa Yesu kwenye Sinema ndio wa kwake, ama picha zinazomwonyesha akiwa na uso mzuri wa kizungu (nywele laini ndefu za brown na blue eyes). Hata hivyo, sura hiyo siyo yake kwani, Wayahudi wa zamani hawakuwa na sura za namna hiyo. Halafu tukumbuke kuwa, zamani ilikuwa haiwezekani mwanaume kuwa handsome Kama picha ya Yesu Kristo kutokana na ugumu wa mazingira ya wakati huo.

View attachment 805874
View attachment 805876
View attachment 805873W

Mimi nakubaliana wazi na picha hii ya chini kwani picha za kwenye sinema zinazomwonyesha akiwa kama mzungu zaidi kuliko Myahudi.
 
Mimi nakubaliana wazi na picha hii ya chini kwani picha za kwenye sinema zinazomwonyesha akiwa kama mzungu zaidi kuliko Myahudi.
Swali ulilojiuliza, na wengine pia wamewahi kujiuliza.

Kuna hii makala ya BBC inajaribu nayo kutoa mwanga zaidi: https://www.bbc.com/swahili/habari/2015/12/151224_how_did_jesus_looked_like

Pia kupitia maandiko ya kwenye biblia, waweza pata mwanga zaidi:

Sura na umbo:

Yesu alikuwa Muyahudi na bila shaka aliriti umbo la kiyahudi kutoka kwa mama yake. (Waebrania 7:14) Inawezekana sura na umbo lake havikuwa tofauti kabisa na watu wengine. Wakati fulani alifikia kusafiri kwa siri kutoka Galilaya mupaka Yerusalemu bila hata watu kumutambua. (Yohana 7:10, 11) Na inaonekana kwamba hata kati ya mitume wake, hakuwa na umbo lenye kuwa tofauti sana nao. Kumbuka kwamba, Yuda Iskariote alipaswa kumutambulisha kwenye kikundi cha watu wenye walikamata Yesu.—Mathayo 26:47-49.

Urefu wa nywele:
Inawezekana Yesu hakuwa na nywele ndefu, kwa sababu Biblia inasema kwamba “nywele ndefu, ni aibu [kwa mwanaume].”—1 Wakorintho 11:14.

Ndevu: Yesu alikuwa na ndevu. Alifuata sheria ya Wayahudi yenye ilikataza wanaume ‘kuharibu ncha ya ndevu zao.’ (Mambo ya Walawi 19:27; Wagalatia 4:4) Pia, Biblia inaeleza kuhusu ndevu za Yesu katika unabii wenye kuzungumuzia mateso yake.— Isaya 50:6.

Mwili:
Maelezo yote yanaonyesha kwamba Yesu alikuwa na nguvu. Wakati wa utumishi wake, alisafiri kilometre nyingi. (Mathayo 9:35) Mara mbili alisafisha hekalu la Wayahudi akipindua meza za wabadilisha-feza, na mara moja alifukuza inje wanyama kwa kutumia fimbo. (Luka 19:45, 46; Yohana 2:14, 15) Kitabu Cyclopedia cha McClintock na Strong kinasema hivi: “Maelezo yote ya injili yanaonyesha [Yesu] akiwa na afya nzuri na nguvu nyingi za kimwili.”—Buku la IV, ukurasa wa 884.

Ishara za uso:
Yesu alikuwa mwenye shauku na mwenye huruma, na bila shaka hilo lilionekana kupitia ishara za uso wake. (Mathayo 11:28, 29) Watu wa namna zote walimutafuta ili kupata kitulizo na musaada. (Luka 5:12, 13; 7:37, 38) Hata watoto walijisikia muzuri kuwa pamoja naye.—Mathayo 19:13-15; Marko 9:35-37.

Mawazo ya uongo kuhusu sura na umbo la Yesu

Wazo la uongo:
Watu fulani wanasema kwamba Yesu alikuwa wa kizazi cha Waafrika kwa sababu kitabu cha Ufunuo kinafananisha nywele zake na sufu (ao, manyoya ya kondoo) na miguu yake na “shaba inapowaka.”—Ufunuo 1:14, 15.

Ukweli wa mambo:
Kitabu cha Ufunuo kinatolewa “kwa njia ya ishara.” (Ufunuo 1:1) Maelezo kuhusu nywele na miguu ya Yesu ni maneno ya mufano yenye kuonyesha sifa zake kisha ufufuo wake, haiko maelezo kuhusu sura na umbo lake wakati alikuwa katika dunia. Wakati inasema kwamba “kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji,” Ufunuo 1:14 inatumia rangi kuwa ulinganifu, hapana umbo la nywele. Hilo linaonyesha hekima yake yenye kutokana na miaka yake. (Ufunuo 3:14) Andiko hili halilinganishe umbo la nywele za Yesu na sufu na halilinganishe pia umbo la nywele zake na teluji.
Miguu ya Yesu ilionekana “kama shaba safi inapowaka katika tanuru.” (Ufunuo 1:15) Pia, sura yake ilikuwa “kama jua linapoangaza katika nguvu zake.” (Ufunuo 1:16) Kwa kuwa hakuna watu wenye kuwa na rangi ya ngozi yenye kupatana na maelezo hayo, maono hayo yanapaswa kuwa ya mufano, na yanaonyesha Yesu mwenye kufufuliwa kama mutu “anayekaa katika nuru isiyoweza kufikiwa.”—1 Timotheo 6:16.


Chanzo: https://www.jw.org/swc/mafundisho-ya-biblia/maulizo/yesu-alifanana-namna-gani/
 
Yesu hajawahi kupiga wala kuacha picha wala haitaji aaminiwe kwa kuonwa sura. Imani inatosha kabisa Kuona matendo yake makuu katika maisha yako huku ukingoja kumuona Mubashara siku akija.

Picha zote za anayesadikiwa Yesu ni za Uongo au kwa lugha rafiki ni kielelezo tu.
Yesu alimzawadia Mt. Veronica kitambaa chenye sura yake mwenyewe
 
Hivi Yesu alikuwepo au ni mchongo ili watu waishi kwa amani? Siamini kama Mungu wa kweli ana mtoto wa kumtoa kafara. Sasa binadamu atoe kafara na Mungu atoe kafara, inaingia akilini kweli! Naamini Mungu mwenye uwezo na huruma hawezi kufanya hivyo. Mimi bado namtafuta Mungu wa kweli kupitia imani yangu ya jadi.
 
Ebu tuelewane hapa kwamba
Hizo Ni picha za yesu au ni picha za muigiza filamu za yesu
 
Back
Top Bottom