MAMESHO
JF-Expert Member
- Jul 5, 2011
- 1,366
- 1,622
Naandika ujumbe huu kwa niaba ya dada mmoja anaitwa Joan, alinunua kiwanja kutoka kwa rafiki yake miaka ya nyuma na kupewa hati ya kijiji ambapo aliweka mashahidi watatu.
Aliyemuuzia kiwanja alisafiri kwenda njje ya nje ambako ameolewa na anaishi huko kwa sasa. Joan akaanza kujenga nyumba ya vyumba viwili katika kiwanja chake cha 20 x 20. Baada ya nyumba kufika dirishani kajitokeza mtu kasema kiwanja ni chake naye alinunua kwa huyo huyo aliyemuuzia.
Akamwambia kashtaki popote na ujenzi uliofanya nitakulipa, cha ajabu anaendelea na ujenzi katika nyumba ile na ana mpango wa kurasimisha ile ardhi kupitia serikali ya kijiji.
Amekuwa akitoa majibu ya dharau na kusisitiza kama Joan ana haki aende mahakamani. Hapa namUombea msaada wa kisheria ni hatua gani afuate ili kupata haki yake. Kutokana na kipato chake hawezi kumudu gharama za mwanasheria kwa sasa, lakini naamini akipata ushauri ataufanyia kazi na nitakuwa natoa mrejesho wa kinachoendelea.
Natanguliza shukrani za dhati.
Aliyemuuzia kiwanja alisafiri kwenda njje ya nje ambako ameolewa na anaishi huko kwa sasa. Joan akaanza kujenga nyumba ya vyumba viwili katika kiwanja chake cha 20 x 20. Baada ya nyumba kufika dirishani kajitokeza mtu kasema kiwanja ni chake naye alinunua kwa huyo huyo aliyemuuzia.
Akamwambia kashtaki popote na ujenzi uliofanya nitakulipa, cha ajabu anaendelea na ujenzi katika nyumba ile na ana mpango wa kurasimisha ile ardhi kupitia serikali ya kijiji.
Amekuwa akitoa majibu ya dharau na kusisitiza kama Joan ana haki aende mahakamani. Hapa namUombea msaada wa kisheria ni hatua gani afuate ili kupata haki yake. Kutokana na kipato chake hawezi kumudu gharama za mwanasheria kwa sasa, lakini naamini akipata ushauri ataufanyia kazi na nitakuwa natoa mrejesho wa kinachoendelea.
Natanguliza shukrani za dhati.