Je ni halali waziri huyu kumtupia zigo hili waziri mkuu kwa dhambi yake mwenyewe!

MELODY

Member
Apr 6, 2012
23
11
Waziri wa Ujenzi Ndugu John Pombe Magufuli akihojiwa na waandishi kuhusu kutumia siasa chafu za kibaguzi kwenye kampeni mbalimbali kukibeba CCM alikwepa kujibu hoja ya dhambi yake na kumsukumia waziri mkuu Mizengo Pinda baada ya waziri mkuu kuulizwa kwenye maswali ya hapo kwa papo bungeni. Miongoni mwa kauli za kibaguzi (siasa chafu) ni kwamba serikali haitapeleka maendeleo wakichagua upinzani katika maeneo husika. Huku ni kuvunja katiba na kinyume na taratibu. Magufuli akihojiwa alijibu "Sina la kujibu na kama ni suala la tuhuma hizo kamuulize Waziri mkuu kwani ndiye aliyeulizwa. Sasa unataka nini kwangu"Mwanachi april 14/2012.
Je Pinda ndo amekuwa katibu au msemaji wa Magufuli? Magufuli kushindwa kujibu hoja ni dalili za kufilisika kisiasa?
 
Mie nadhani ni bora abebe zigo lake mwenyewe.Kumtupia Pinda asidhani amepona,bora angejitetea hata kwa kujibu fyongo sababu aliyatamka mwenyewe.Anataka kutuaminisha kwamba alitumwa na Pinda kuyasema.Lakini pamoja na yote imekuwa tabia ya wabunge wa magamba kuwatisha wananchi kuwa wakichagua upinzani maeneo husika hayato pelekewa maendeleo.Wajue kuwa wananchi wanauelewa mwingi kwa masuala yanayo wahusu,na wanacho kifanya magamba kinazidi kuwadidimiza.
 
Na si Magufuli tu aliyejichanganya kuhusu tuhuma hizo,wengine ni Marry Nagu(Waziri wa viwanda) na Naibu waziri wa ardhi(Kilaza aitwae Ole medeye)
 
Back
Top Bottom