Je ni halali mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa kulipwa mshahara na serikali?

ungonella wa ukweli

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
4,210
555
Wanabodi heshima kwenu. Kama mnavyojua wanabodi hapa jf,wakuu wa wilaya ni wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ya ccm,na pia wakuu wa mikoa ni wajumbe wa kamati ya siasa ya ccm ya mikoa. Vilevile mkuu wa mkoa ni mwakilishi wa rais katika mkoa. Pia na mkuu wa wilaya ni mwakilisha wa rais wilayani.kama mtakumbuka matamshi yaliyotolewa na viongozi wa ccm hivi karibuni kuwa wakuu wa wilaya wahakikishe viongozi wa kisiasa wanaotoa matamshi ya kumtukana ama kumkashifu rais wakamatwe.pia mtakumbuka la mkuu wa wilaya kule mwanza kuagiza kukamatwa kwa wabunge wa mwanza. Kwa mtiririko huo unadhani ni halali kulipwa mshahara na serikali ambayo inakusanya kodi kutoka kwa wananchi wote?
 
wanafanyiaga mavikao yao kwenye kumbi za se3rikali bure,chakula bure,bili kwa serikali..me hate dis country man
 
Wanabodi heshima kwenu. Kama mnavyojua wanabodi hapa jf,wakuu wa wilaya ni wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ya ccm,na pia wakuu wa mikoa ni wajumbe wa kamati ya siasa ya ccm ya mikoa. Vilevile mkuu wa mkoa ni mwakilishi wa rais katika mkoa. Pia na mkuu wa wilaya ni mwakilisha wa rais wilayani.kama mtakumbuka matamshi yaliyotolewa na viongozi wa ccm hivi karibuni kuwa wakuu wa wilaya wahakikishe viongozi wa kisiasa wanaotoa matamshi ya kumtukana ama kumkashifu rais wakamatwe.pia mtakumbuka la mkuu wa wilaya kule mwanza kuagiza kukamatwa kwa wabunge wa mwanza. Kwa mtiririko huo unadhani ni halali kulipwa mshahara na serikali ambayo inakusanya kodi kutoka kwa wananchi wote?

Wakuu wa mikoa na wilaya ni civil servants kwa hiyo wanalipwa na sirikali. Kutumika kwao ni tatizo lingine ambalo katiba mpya inatakiwa iliweke sawa.
While at it, ningependekeza regional structure iondolewe tubakie na wilaya - madaraka wilayani yawe mikononi mwa waliopigiwa kura. Watendaji wilayani wawe chini ya waliochaguliwa na wananchi.
 
Back
Top Bottom