Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,477
- 30,130
Kutokana na mienendo ya kisiasa inavyokwenfa nchini kwetu, kuna tetesi kuwa watawala wetu wako mbioni kurejesha mfumo wa chama kimoja
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 3(1) inatamka kuwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itaendeshwa katika mfumo wa kidemokrasia na ni ya mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu
Ukifuatilia matukio kadhaa nchini kwa siku za karibuni, ni dhahiri kuwa watawala wetu wamepania kuitejesha nchi yetu kwenye mfumo wa chama kimoja
Mikakati kadhaa inaendelea nchi nzima nyuma ya pazia
Mkakati mmjawapo muhimu sana uliofanyika hivi karibuni ni kuwakata "makali" wapinzani, katika uchaguzi wa setikali za mitaa wasichukue hata mitaa mmoja nchi nzima!
Mkakati mwingine ni kivipunguzia vyama vya upinzani nguvu ili kuwezesha mambo ya watawala yapite bila kipingamizi chochote
Tumeona dalili za awali kabisa za watawala wetu katika kutimiza azma yao dhalimu katika uchaguzi wa serikali za mitaa ulioisha hivi karibuni, ambapo wagombea wa vyama vya upinzani zaidi ya asilimia 95, yalikatwa na wasimamizi wa uchaguzi huo, ambapo ni makada kindakindaki wa CCM, kwa madai kuwa wamekosea kujaza fomu za kuombea uongozi huo na wasimamizi wa uchaguzi kuzikimbia ofisi zao!
Wakati wenzao wa CCM wakidaiwa kuwa wagombea wao ni "malaika" ambapo wagombea wao wote asilimia 100, wamejaza kwa usahihi mkubwa na hivyo kufanya wagombea wao, wapite bila kupingwa!
Hivi karibuni tulimsikia Rais Magufuli akihoji iweje yeye apewe mamlaka ya kuteua na asipewe mamlaka ya kutengua ndani ya Katiba ya nchi??
Ni jambo linaloeleweka kuwa kuna baadhi ya nafasi ambazo kutokana na unyeti wake, Rais amepewa mamlaka ya kuteua, lakini amenyimwa uwezo wa kutengua
Miongoni ya nafasi hizo ni ya CAG na Majaji wa mahakama kuu
Inaonekana hiyo kupewa nafasi ya kuteua bila kupewa uwezo wa kutengua, ndiko kunakomkera na kumkosesha usingizi Rais wetu
Basi ni dhahiri kuwa watawala wetu wanafanya mipango nyuma ya pazia kutaka kuirekebisha Katiba ya nchi yetu, ili kufanya usiwepo ukomo wa Rais kukaa madarakani
Tunaamini pia kwa yale tuliyoyaona kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, ni "trailer" tu na ni dhahiri kuwa picha kamili tutaiona kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 3(1) inatamka kuwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itaendeshwa katika mfumo wa kidemokrasia na ni ya mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu
Ukifuatilia matukio kadhaa nchini kwa siku za karibuni, ni dhahiri kuwa watawala wetu wamepania kuitejesha nchi yetu kwenye mfumo wa chama kimoja
Mikakati kadhaa inaendelea nchi nzima nyuma ya pazia
Mkakati mmjawapo muhimu sana uliofanyika hivi karibuni ni kuwakata "makali" wapinzani, katika uchaguzi wa setikali za mitaa wasichukue hata mitaa mmoja nchi nzima!
Mkakati mwingine ni kivipunguzia vyama vya upinzani nguvu ili kuwezesha mambo ya watawala yapite bila kipingamizi chochote
Tumeona dalili za awali kabisa za watawala wetu katika kutimiza azma yao dhalimu katika uchaguzi wa serikali za mitaa ulioisha hivi karibuni, ambapo wagombea wa vyama vya upinzani zaidi ya asilimia 95, yalikatwa na wasimamizi wa uchaguzi huo, ambapo ni makada kindakindaki wa CCM, kwa madai kuwa wamekosea kujaza fomu za kuombea uongozi huo na wasimamizi wa uchaguzi kuzikimbia ofisi zao!
Wakati wenzao wa CCM wakidaiwa kuwa wagombea wao ni "malaika" ambapo wagombea wao wote asilimia 100, wamejaza kwa usahihi mkubwa na hivyo kufanya wagombea wao, wapite bila kupingwa!
Hivi karibuni tulimsikia Rais Magufuli akihoji iweje yeye apewe mamlaka ya kuteua na asipewe mamlaka ya kutengua ndani ya Katiba ya nchi??
Ni jambo linaloeleweka kuwa kuna baadhi ya nafasi ambazo kutokana na unyeti wake, Rais amepewa mamlaka ya kuteua, lakini amenyimwa uwezo wa kutengua
Miongoni ya nafasi hizo ni ya CAG na Majaji wa mahakama kuu
Inaonekana hiyo kupewa nafasi ya kuteua bila kupewa uwezo wa kutengua, ndiko kunakomkera na kumkosesha usingizi Rais wetu
Basi ni dhahiri kuwa watawala wetu wanafanya mipango nyuma ya pazia kutaka kuirekebisha Katiba ya nchi yetu, ili kufanya usiwepo ukomo wa Rais kukaa madarakani
Tunaamini pia kwa yale tuliyoyaona kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, ni "trailer" tu na ni dhahiri kuwa picha kamili tutaiona kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020