Je naweza kupata mkopo bank kwa kutumia business plan?

Mimi nimetoka leo tu huko bank, baada ya kuonana na mtu wa bank idara ya mikopo

MAZUNGUMZO YAKAWA HIVI

Me: Nahitaji kukopa pesa nifanyie biashara nina dhamana kiwanja.
Banker : una biashara?
Me: Ndio
Banker:biashara gani?
Me: Video Library
Banker: Ina leseni ya biashara
Me: hapana
Banker: Tunakopesha kwa mtu mwenye biashara ambayo tiali inafanya kazi ina leseni na account ya bank ambayo inazungusha pesa zake za biashara humo, naongeza trend yake inaonekana.
Me : Kazi njema

Nikatoka huyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iyo biashara yenyewe zugazuga tu yakupata shingi 500/= yakujiungia bando lakuja kusumbuana na mng'ato humu.

Sent using Jamii Forums mobile app


Lakini juzi nilipoongea na ww ...🤔🤔 huna mpango kbs wa kuhama jiji ww...yaan unatamani mafanikio lakini hutak kutok kwenye comfort zone...!
Kuna face na sound unaona kbs huyu yuko tayari muda na popote pale!😉😉
 
Ukiwa n idea plus una hati y kiwanja au nyumba unapewa mkopo

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiwanja kinatumika kama dhamana baada ya kuwa na biashara yenye leseni na ambayo ina mzunguko wa fedha.
Hicho kiwanja lazima kiwe kwenye eneo potential nacho kiwe na hati au nyumba.
Mikopo inatolewa kwa ajili ya kuendeleza biashara sio kuanzia biashara.
 
Back
Top Bottom