Je, naweza kupata Laptop nzuri kwa budget ya laki nane?

Core ni kma procoessor iliyopo ndani ya CPU. Hizi core ndio zinafanya hzo instructions zinazohitajika kurun program flan. Nguvu ya core inakuwa determined kwa kupima Instructions per cycle (IPC), hii ni idadi ya maelekezo core yako inaweza fanya kwa mzunguko mmoja wa CPU (mzunguko mmoja wa CPU clock speed). IPC ndio muhim sana, core mbili tofaut kutoka processor mbili tofaut zinaweza kuwa na clock speed sawa (mf 1GHz) ila moja ikawa na 2000IPC na nyingine ikawa na 1000IPC ile ya 2000 IPC ndio yenye nguvu. Lakini kumbuka kuwa clock speed bado ni muhimu, kma CPU zote ni za class moja na generation sawa ile yenye clock speed kubwa ndio itakuwa na nguvu zaidi.

Sasa je ni kitu gani kinachangia core/processor kuwa na IPC kubwa kuliko nyingine?

Cha kwanza ni number ya transistors, kila processor ina transistors ndani yake ambazo ndio zinarun hzo instructions. Core moja inaweza kuwa na transistors nyingi kuliko nyingine. Yenye transistor nyingi itakua na IPC kubwa.

Pili ni size ya core hyo. Core kubwa inamaanisha kuwa inaweza beba transistors na nodes nyingi zaidi. Ndio maana zile Xeon processors za kwenye servers zinakuwa na core zenye nguvu sana

Kingine pia ni kwamba fabrication method (njia inayotumika kutengeneza processor) inachangia uwepo wa transistors na nodes nyingi. Kma ukicheki kwenye processor specification utakuta hchi kitu kimenadikwa: 10nm or 7nm or 5nm. Hichi ni kipimo cha udogo wa components (transistors and nodes) zilizopoa kwenye processor. Uwepo wa components ndogo inawezesha kuweka transistors and nodes nyingi kwenye processor yako na kupandisha IPC kwa kila core.

Pia processor zenye clock speed ndogo zinaweza kuwa na IPC kubwa sababu ya joto linalotengezwa. Processor zenye clock speed kubwa zinatengeza joto jingi na hii inalimit ufanyaji kazi wa transistors hvyo kuwa na IPC ndogo. Ila ukiwa na clock speed ndogo unaweza pandisha IPC yako sababu joto sio jingi sana. Ndio maana unakuta 10th gen i3 yenye clock speed ya 1.4ghz inaikalisha 3rd gen i7 yenye clock speed ya 2.7ghz kwenye single core performance.

Ukitaka details zaidi soma hizi sehemu mbil:

1.

2. Instructions per cycle - Wikipedia

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwa uzoefu wako... Hp na dell zote zikiwa generation ya 9-10 hipi itakuwa bora sifa zikiwa zinafanana
 
Mkuu kwa uzoefu wako... Hp na dell zote zikiwa generation ya 9-10 hipi itakuwa bora sifa zikiwa zinafanana
Inategemea. Haijalishi company inategemea model hyo ya laptop inaweza kuhandle na kushusha temperature za CPU. Kma laptop ina cooling mbaya performance yake lazima ipingue (au wao wenyewe wanapunguza). Kma laptop zote ni slim jua hazitaweza fikia uwezo halisi wa hyo CPU sababu slim laptops hazina cooling nzuri. Hyo tofaut za laptop zilizo kwenye class moja usiziwaze sana sababu ni ndogo tu. Ila uwe unapitia review za sites kma Notebook check au Anandtech ndio huwa wanaelezea vizuri performance za CPUs katika device mbali mbali
 
Inategemea. Haijalishi company inategemea model hyo ya laptop inaweza kuhandle na kushusha temperature za CPU. Kma laptop ina cooling mbaya performance yake lazima ipingue (au wao wenyewe wanapunguza). Kma laptop zote ni slim jua hazitaweza fikia uwezo halisi wa hyo CPU sababu slim laptops hazina cooling nzuri. Hyo tofaut za laptop zilizo kwenye class moja usiziwaze sana sababu ni ndogo tu. Ila uwe unapitia review za sites kma Notebook check au Anandtech ndio huwa wanaelezea vizuri performance za CPUs katika device mbali mbali
Nimekusoma mkuu mi nataka utofauti kati ya laptop ya hp na dell..maana nimekuta core i3 zinazofanana sifa ila ni dell ma hp... Sasa inanipa ugumu wa kuchagua
 
Dell Latitude 5491 (hii ni around 700k to 800k)
Thinkpad T470 (hii ni around 800k)
Thinkpad T460 (hii ni around 700k)
HP ProBook 450 G5 (hii inaendaga mpk 1M)
HP ProBook 840 G3 (hii ni around 900k)

Hizi ni baadhi ambazo nimeziona madukani hapa karibuni. Ila kwa program za 3D unaweza pata tafuta hata laptop ya 5th or 6th gen yenye dedicated graphics za Nvidia or AMD.

Mm kuna jamaa yangu anatumia hzo software kwenye Thinkpad T440p yenye Nvidia graphics na anasema kwake iko vizuri tu ila hii ni PC kubwa kidogo sio hzo slim na alichukua kwa 600k.

Pia hzo nilizotaja hapo ni bei za refurbished nzuri sio bei za mpya na uhakikishe ni ya 8GB RAM or 16GB sio chini ya hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
For sure..
 
Nimekusoma mkuu mi nataka utofauti kati ya laptop ya hp na dell..maana nimekuta core i3 zinazofanana sifa ila ni dell ma hp... Sasa inanipa ugumu wa kuchagua
Hapo unatakiwa kujua jina full la hyo CPU. Kwa mfani core i3-9100. Ukijua jina kamili la CPU zilizopo kwenye laptop hzo mbili ndio utajua ipi ni bora kuliko nyingine. Alaf kwenye laptop sio unaangalia tu CPU, kuna vitu vingine vya kuangalia pia. Mfano; backlit keyboard, display resolution and quality, battery capacity, speaker quality, n.k.

Unaweza kuta HP ina core i5 8350U na Dell ina core i7 8550u. Hii Dell itakua na uwezo uliozidi wa HP ila sio sana lakini unakuta hyo HP ina display ya IPS ya 1080p na baklit keyboard na good quality speakers kuliko hyo Dell. Sasa hapa kutokana na kazi unayotaka kufanya na hyo laptop unaweza kuta hyo HP ni bora zaidi sababu ina display nzuri na backlit keyboard wakati bado ina uwezo mzuri tu.
 
Hapo unatakiwa kujua jina full la hyo CPU. Kwa mfani core i3-9100. Ukijua jina kamili la CPU zilizopo kwenye laptop hzo mbili ndio utajua ipi ni bora kuliko nyingine. Alaf kwenye laptop sio unaangalia tu CPU, kuna vitu vingine vya kuangalia pia. Mfano; backlit keyboard, display resolution and quality, battery capacity, speaker quality, n.k.

Unaweza kuta HP ina core i5 8350U na Dell ina core i7 8550u. Hii Dell itakua na uwezo uliozidi wa HP ila sio sana lakini unakuta hyo HP ina display ya IPS ya 1080p na baklit keyboard na good quality speakers kuliko hyo Dell. Sasa hapa kutokana na kazi unayotaka kufanya na hyo laptop unaweza kuta hyo HP ni bora zaidi sababu ina display nzuri na backlit keyboard wakati bado ina uwezo mzuri tu.
Ok ngoja nikatest la mentali... Nikipigwa fresh.

Kupotea njia ndio kuijua njia
 
Hapo unatakiwa kujua jina full la hyo CPU. Kwa mfani core i3-9100. Ukijua jina kamili la CPU zilizopo kwenye laptop hzo mbili ndio utajua ipi ni bora kuliko nyingine. Alaf kwenye laptop sio unaangalia tu CPU, kuna vitu vingine vya kuangalia pia. Mfano; backlit keyboard, display resolution and quality, battery capacity, speaker quality, n.k.

Unaweza kuta HP ina core i5 8350U na Dell ina core i7 8550u. Hii Dell itakua na uwezo uliozidi wa HP ila sio sana lakini unakuta hyo HP ina display ya IPS ya 1080p na baklit keyboard na good quality speakers kuliko hyo Dell. Sasa hapa kutokana na kazi unayotaka kufanya na hyo laptop unaweza kuta hyo HP ni bora zaidi sababu ina display nzuri na backlit keyboard wakati bado ina uwezo mzuri tu.
Mkuuu maelezo yako ni mazuri sana ila kwa Mimi nisie na uzoefu was PC naomba nisha uri moja kwa moja nichukue PC ya aina gani na yenye specification zipi ambayo itanifaaa na nitaitumia kwa kazi za ki handisi,,bajeti isizidi 1.5M
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom