Je, nauli zinazotozwa na watu wa Daladala wa Jiji la Dar es Salaam ni sahihi kwa mujibu wa SUMATRA /LATRA au ni abiria kukosa uelewa?

Msurunje

JF-Expert Member
Oct 21, 2019
219
342
Habarini za Jumapili ndugu wa JF,

Nina imani tunaendelea kupambana na athari za ugonjwa wa korona ambao athari zake zimekuwa kubwa sana kiuchumi kuliko kiafya hasa katika jamii yetu ya Kitanzania/Kiafrika.

Nije kwenye mada yangu moja kwa moja. Kumekuwa na utaratibu wenye mkanganyiko kwa watu wa daladala hasa wa jiji la dar es salaam katika utozaji wa nauli. Makondakta wamekuwa wakitoza nauli kubwa kwa kuliko kiwango kilichowekwa na mamlaka kwa kisingizio cha vituo badala ya umbali hivyo muda mwingine kuleta mzozo kwa abiria ambao wanajua utaratibu wa mpangilio wa nauli zilizowekwa na mamlaka husika.

Hapa naweka mpangilio wa nauli kulingana na umbali kwa mujibu wa Sumatra /Latra.

Umbali -- Nauli
0.1-15km 400-450
15-20km 500-600
20-25km 600-750

Sasa natumia ruti ya Gongo la Mboto kama mfano.

Kutoka G/Mboto - Makumbusho =22km
G/mboto - Buguruni =12km
G/mboto - Ubungo =19km
Vingunguti - Buguruni =2.4km
Vingunguti - Tabata Reli =4.5km.

Kitu kinacholeta mkanganyiko ni kwamba ukipanda gari kutoka gongo la mboto mpaka buguruni ambapo ni 12 km nauli ni sh 400 lakini ukipandia gari Vingunguti na ukashuka tabata reli ambapo ni 4.5 km kondakta anakwambia nauli ni sh 500 tena anakwambia nauli ya 400 mwisho ni buguruni bila kujali umepandia wapi.

Lakini ukikagua tiketi zao zimeandikwa nauli kwa baadhi ya vituo na umbali na hali hii ya kuandika nauli za vituo badala ya umbali ipo jiji dsm kwa kiasi kikubwa kuliko majiji mengine.

Sasa je, nauli zinazotozwa na watu wa daladala wa jiji la Dar es Salaam kwa kuzingatia vituo badala ya umbali ni sahihi kwa mujibu wa mamlaka husika au ni abiria kutokuwa na uelewa kuwa nauli inalipwa kulingana na umbali na siyo vituo au ni makondakta kutokujua kuwa wanapaswa kumtoza abiria nauli kulingana na umbali na siyo vituo?

Wakuu naomba tupeane elimu juu ya hili.
 
Nakuongezea.

1. Gongolamboto - Masaki 45 km. Nauli 600

Completely unfair
 
Nakuongezea.

1. Gongolamboto - Masaki 45 km. Nauli 600

Completely unfair
Sio kweli mkuu, gongo la Mboto - masaki ni 25 km lkn pia nauli za ndani ya mji huwa zinahesabiwa mwisho km 25 kwa ikizidi hapo ni uchaguzi wako wewe mwenyewe kuendelea na hiyo ruti au la. Mfano wa huo umbali uliyouweka ni kutoka Chanika.
 
Nielewe mkuu. Nimepima kwa gari yangu mwenyewe. Banana mpaka pale Macho ni 36 km. Iweje kuwe na 25 km Gongolamboto mpaka Masaki? Juzi nimehakiki kwa uber nikapata the same. Siwezi kuweka screen shot ya uber kwa sababu ina details nyingi binafsi. Anhalaia google map thr unipe jibu
Sio kweli mkuu, gongo la Mboto - masaki ni 25 km lkn pia nauli za ndani ya mji huwa zinahesabiwa mwisho km 25 kwa ikizidi hapo ni uchaguzi wako wewe mwenyewe kuendelea na hiyo ruti au la. Mfano wa huo umbali uliyouweka ni kutoka Chanika.
 
Muda mwingine hizo routi zinakuwa na bei ndogo kweli, Mfano mchana ukiwa Buguruni kwenda Ubungo nauli 300 panda asubuhi uwone bei inaongezeka.
 
Tatizo la LATRA ambao wamechukua nafasi ya SUMATRA wamekuwa ni watu wa kukaa ofisini, hizi nauli zingekuwa wazi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kila kwenye gari kuna jedwali la nauli kuhusu tiketi huwa zinachapishwa na mwenye bus kwa hiyo anajiandikia anavyotaka iwe
 
Acha ujuaji na kulialia, umaskini kitu kibaya sana... kama umepungukiwa hiyo ‘mia’ ongea tu na konda atakuelewa.
 
Nielewe mkuu. Nimepima kwa gari yangu mwenyewe. Banana mpaka pale Macho ni 36 km. Iweje kuwe na 25 km Gongolamboto mpaka Masaki? Juzi nimehakiki kwa uber nikapata the same. Siwezi kuweka screen shot ya uber kwa sababu ina details nyingi binafsi. Anhalaia google map thr unipe jibu
Nimetumia mpaka msaada wa Google map mkuu ili kuwa na uhakika zaidi lbd na wewe unaweza angalia ili uthibitishe lkn according to Google maps g/Mboto to masaki =25 km & chanika to masaki =44km
 
LATRA wanaingilia vitu 2 kwenye upangaji wa nauli ,uwingi wa abiria katika ruti utakayopangiwa na umbali wa ruti utakayoenda.
Mfano ruti ya mbagala makumbusho nauli ni 600 ila wao wanangalia kuwa ukitoka mbaghala mpaka ufike karume au boma ,utakuwa umeshusha na kupandisha abiria wengi tu,mpaka ufike kawe au makumbusho utakuwa umefanya biashara nzuri tu,na kweli mnaweza mkatoka mbaghala kufika karume karibu robo 3 ya abiria ,uwa wameshuka pale .
 
Acha ujuaji na kulialia, umaskini kitu kibaya sana... kama umepungukiwa hiyo ‘mia’ ongea tu na konda atakuelewa.
Sio ujuaji wala kulia ila kiongozi ila utaonekana mvivu wa kufikiri kutozwa nauli ya sh 400 kwenye 12km alafu utozwe sh 500 kwenye 4.5km ukaona ni sawa.
 
Google map inapima straight line kaka, ndio sababu unapata kiloneta hizo 25. Ukiendesha gari hufuati straight line, unafuata barabara. Kama una muda just drive that way, utakuja ku edit post hapa. Anzia Gomz, pitia Chang'ombe, Karume, Ilala Boma, Kigogo, Magomeni, Morocco, Oysterbay Police, Macho mpaka Masaki. Sio 25 km hio
Nimetumia mpaka msaada wa Google map mkuu ili kuwa na uhakika zaidi lbd na wewe unaweza angalia ili uthibitishe lkn according to Google maps g/Mboto to masaki =25 km & chanika to masaki =44km
 
Tatizo la LATRA ambao wamechukua nafasi ya SUMATRA wamekuwa ni watu wa kukaa ofisini, hizi nauli zingekuwa wazi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kila kwenye gari kuna jedwali la nauli kuhusu tiketi huwa zinachapishwa na mwenye bus kwa hiyo anajiandikia anavyotaka iwe
Si kweli LATRA wanafanya kazi changamoto kubwa nadhani ni kwa abiria nao kujua nafasi yao
Si kila unapotokea ukiukwaji kunakuwepo mtu wa LATRA
 
Si kweli LATRA wanafanya kazi changamoto kubwa nadhani ni kwa abiria nao kujua nafasi yao
Si kila unapotokea ukiukwaji kunakuwepo mtu wa LATRA
unawatetea bure siku zote madaladala yanakamatwa na traffic kwa kukiuka sheria za barabarani umeshawahi kusikia LATRA wamewaadhibu madaladala kwa kukiuka sheria au hata ukiingia kwenye website yao kuna mwongozo wa nauli za daladala au kuna namba ya kutoa taarifa pale daladala zinapovunja sheria
 
Back
Top Bottom