Je nani anamiliki maisha yako? Who own your life?

Nxt Millionaire

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
406
89
Yawezekana likaonekana ni swali la kizushi au la kipuuzi pengine ni lakitoto hivi, lakini wakati mwingine maswali ya kitoto yanakuwaga na maana hasa ukichukua muda kidogo kuyatafakali pamoja na upuuzi wake au utoto wake na labda unaweza kuona mantiki, na yapo pia maswali yakijinga na kitoto ambayo yaliwai shindwa jibiwa na hao wanaojiita wakubwa.

Sina hakika umepata picha gani au mantiki katika swali hili, vyovyote iwavyo labda kusaidia katika kupata jibu, jiulize maswali haya:-

- Una uhuru kiasi gani kwenda utakako?
- Una uhuru kiasi gani kufanya kazi utakayo na muda uutakao?
- Je una uhuru kiasi gani kujichagulia watu wa kufanya nao kazi?
- Na je nini kitatokea kwa kazi au biashara yako iwapo utasafiri muda mrefu? kama mwaka hivi.


Majibu ya maswali haya yaweza kutofautiana kati mtu mmoja na mwingine lakini ndio pia yatakuonesha kuwa nani mmiliki wa maisha yako.

Labda nikushirikishe kisa kimoja kilichowai kunipata wakati nikiwa mwajiriwa.
Wakati mmoja katika ajira yangu ya MWISHO (ndio ya mwisho sababu sitarajii kuajiriwa tena labda kuajiri) ilitokea kwamba nimefanya kazi zaidi ya miezi miwili mfululizo hakuna jumapili wala sikukuu na kila siku kurudi home ni usiku na bila malipo yoyote ya ziada, nilikuwa nimechoka sana ata akili zilikuwa zimechoka, nikajikuta nachukia kila mtu bila sababu, siku mmoja nikaomba kwa bosi ili nipumzike japo siku mbili, alikubali shingo upande.

Siku mbili zile nikapata na dharura kifamilia ikabidi niende Morogoro, sikuwa na sababu kuomba ruhusa sababu nina off! lakini kumbe sivyo baada ya siku mbili nikaenda kazini katika maongezi hapa na pale nikasema nilikwenda Moro, we! ilikuwa kosa, nililimwa memo na HR kupitia kwa bosi wangu wa karibu, kisa! kwanini nimeondoka nje ya Dar bila ruhusa ya ofisi, ama! nikamaka si nilipewa siku 2 za mapumziko baada ya kutumika zaidi ya miezi 2 bila mapumziko? tatizo si mapumziko bali ni kuondoka kituo cha kazi bila ruhusa ya mwajiri, yaani utakiwi kwenda hata Kibaha kwa ni nje ya kituo cha kazi, nilichoka kwa kweli.

Ndipo nilijua kumbe mi sina tofauti na mfungwa, japo mi ni mfungwa wa hiari, fikilia umefanya kazi zaidi ya miezi miwili bila mapumziko wala jumapili na bila malipo yoyote ya nyongeza, unapata off ya kulazimisha ktk off hiyo unapata dharura unarudi ofisini unalimwa memo?? ni maisha gani haya? tangu siku hiyo niliweka azimio kuwa lazima nitafute uhuru wangu, wa kipato, afya na maisha pia.


Watu wengi sana wako katika maisha ya namna hii, waajiriwa au wanaojiajiri na baadhi ya wafanyabiashara pia, yaani wengi wanaishi na wako huru lakini wana minyororo isiyoonekana na ambayo hawako tayari kuachana nayo kwa sababu nyingi tu lakini zaidi labda kwa kuwa hawajui la kufanya au ni waoga wa kufanya maamuzi magumu kwa manufaa ya baadaye.



Iwapo uwezi kufanyakazi namna utakavyo, uwezi kufanya kazi ama kupumzika muda uutakao au uwezi kuchagua utakaye kufanya nae kazi, uwezi kusafiri utakapo kwa muda utakao, je waweza sema ni wewe au mtu mwingine anamiliki maisha yako?

“Today’s workers understand that it doesn’t matter how much money you earn if you never get to see your spouse or children, or if you sacrifice your health for your work” by Paul Zane Pilzer, a world-renowned economist, multi millionaire entrepreneur, college professor and author.

Je wewe ni Mmoja wa Today’s workers? huko tayari kufanya maamuzi magumu na muhimu kwa maisha yako?
Huko tayari kujiunga na sekta inayokuwa kwa kasi ya ajabu? kwa mujibu wa Profesa wa Uchumi duniani Paul Zane Pilzer, Sekta hii imekuwa kwa kasi ya ajabu sana katika kipindi cha miaka 20 iliyopita na kuongezeka kwa asilimia 91 katia miaka kumi tu. ikiwa na watu wapatao milioni 70 dunia nzima, leo hii ni sekta ya dola billioni 100.


Doors of opportunity don’t open they unlock: its up to you to turn the knob” Lily Taylor

Do you want to work when you want, how you want and with whom you want? if the answer is YES! then TURN THE KNOB HERE. , but if NO then ignore this.
 
Mkuu kuna watu wako addicted to work. Akitoka kazini late hour anasalimia then laptop. hana cha jmos wala J2 hao naona hawatakuewewa sana ila mimi nimekusona mkuu. Nakubaliana sana na busara zako, tufike mahali tusiwe watumwa wa hizi kazi hadi mtu anapata magonjwa ya ajabu ajabu wakati wenye makampuni yao wanajitajirisha na kuneemeka.
 
wengine mume wengine mke wengine ajira wengine shule ila mimi mmmmh! mungu tu
 
Yawezekana likaonekana ni swali la kizushi au la kipuuzi pengine ni lakitoto hivi, lakini wakati mwingine maswali ya kitoto yanakuwaga na maana hasa ukichukua muda kidogo kuyatafakali pamoja na upuuzi wake au utoto wake na labda unaweza kuona mantiki, na yapo pia maswali yakijinga na kitoto ambayo yaliwai shindwa jibiwa na hao wanaojiita wakubwa.

Sina hakika umepata picha gani au mantiki katika swali hili, vyovyote iwavyo labda kusaidia katika kupata jibu, jiulize maswali haya:-

- Una uhuru kiasi gani kwenda utakako?
- Una uhuru kiasi gani kufanya kazi utakayo na muda uutakao?
- Je una uhuru kiasi gani kujichagulia watu wa kufanya nao kazi?
- Na je nini kitatokea kwa kazi au biashara yako iwapo utasafiri muda mrefu? kama mwaka hivi.


Majibu ya maswali haya yaweza kutofautiana kati mtu mmoja na mwingine lakini ndio pia yatakuonesha kuwa nani mmiliki wa maisha yako.

Labda nikushirikishe kisa kimoja kilichowai kunipata wakati nikiwa mwajiriwa.
Wakati mmoja katika ajira yangu ya MWISHO (ndio ya mwisho sababu sitarajii kuajiriwa tena labda kuajiri) ilitokea kwamba nimefanya kazi zaidi ya miezi miwili mfululizo hakuna jumapili wala sikukuu na kila siku kurudi home ni usiku na bila malipo yoyote ya ziada, nilikuwa nimechoka sana ata akili zilikuwa zimechoka, nikajikuta nachukia kila mtu bila sababu, siku mmoja nikaomba kwa bosi ili nipumzike japo siku mbili, alikubali shingo upande.

Siku mbili zile nikapata na dharura kifamilia ikabidi niende Morogoro, sikuwa na sababu kuomba ruhusa sababu nina off! lakini kumbe sivyo baada ya siku mbili nikaenda kazini katika maongezi hapa na pale nikasema nilikwenda Moro, we! ilikuwa kosa, nililimwa memo na HR kupitia kwa bosi wangu wa karibu, kisa! kwanini nimeondoka nje ya Dar bila ruhusa ya ofisi, ama! nikamaka si nilipewa siku 2 za mapumziko baada ya kutumika zaidi ya miezi 2 bila mapumziko? tatizo si mapumziko bali ni kuondoka kituo cha kazi bila ruhusa ya mwajiri, yaani utakiwi kwenda hata Kibaha kwa ni nje ya kituo cha kazi, nilichoka kwa kweli.

Ndipo nilijua kumbe mi sina tofauti na mfungwa, japo mi ni mfungwa wa hiari, fikilia umefanya kazi zaidi ya miezi miwili bila mapumziko wala jumapili na bila malipo yoyote ya nyongeza, unapata off ya kulazimisha ktk off hiyo unapata dharura unarudi ofisini unalimwa memo?? ni maisha gani haya? tangu siku hiyo niliweka azimio kuwa lazima nitafute uhuru wangu, wa kipato, afya na maisha pia.


Watu wengi sana wako katika maisha ya namna hii, waajiriwa au wanaojiajiri na baadhi ya wafanyabiashara pia, yaani wengi wanaishi na wako huru lakini wana minyororo isiyoonekana na ambayo hawako tayari kuachana nayo kwa sababu nyingi tu lakini zaidi labda kwa kuwa hawajui la kufanya au ni waoga wa kufanya maamuzi magumu kwa manufaa ya baadaye.



Iwapo uwezi kufanyakazi namna utakavyo, uwezi kufanya kazi ama kupumzika muda uutakao au uwezi kuchagua utakaye kufanya nae kazi, uwezi kusafiri utakapo kwa muda utakao, je waweza sema ni wewe au mtu mwingine anamiliki maisha yako?

"Today's workers understand that it doesn't matter how much money you earn if you never get to see your spouse or children, or if you sacrifice your health for your work" by Paul Zane Pilzer, a world-renowned economist, multi millionaire entrepreneur, college professor and author.

Je wewe ni Mmoja wa Today's workers? huko tayari kufanya maamuzi magumu na muhimu kwa maisha yako?
Huko tayari kujiunga na sekta inayokuwa kwa kasi ya ajabu? kwa mujibu wa Profesa wa Uchumi duniani Paul Zane Pilzer, Sekta hii imekuwa kwa kasi ya ajabu sana katika kipindi cha miaka 20 iliyopita na kuongezeka kwa asilimia 91 katia miaka kumi tu. ikiwa na watu wapatao milioni 70 dunia nzima, leo hii ni sekta ya dola billioni 100.


Doors of opportunity don't open they unlock: its up to you to turn the knob" Lily Taylor

Do you want to work when you want, how you want and with whom you want? if the answer is YES! then TURN THE KNOB HERE. , but if NO then ignore this.
Mungu tu ndugu yangu, yeye ndiye aliyekuumba, na anjua utakufa lini na kifo gani
 
Mkuu kuna watu wako addicted to work. Akitoka kazini late hour anasalimia then laptop. hana cha jmos wala J2 hao naona hawatakuewewa sana ila mimi nimekusona mkuu. Nakubaliana sana na busara zako, tufike mahali tusiwe watumwa wa hizi kazi hadi mtu anapata magonjwa ya ajabu ajabu wakati wenye makampuni yao wanajitajirisha na kuneemeka.

Wengi hawajui kuwa Mungu akutuumba tuwe hivyo, alitupa mamlaka ya kutawala kila kitu humu duniani lakini wengi tunakuwa submissive kwa watu wengine kinyume na mpango wa Mungu.
 
Back
Top Bottom