Je nani amewakumbuka wanafuzi wote waliofeli /au kukosa nafasi za kusoma kwa Tangu nchi ipate uhuru?

environmental

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
1,054
137
Taifa limewatelekeza wanafuzi waliofeli mitihani yao bila kujua sababu gani wamefeli. Wakati nchi imepata uhuru darasa la nane alikuwa anapata kazi nzuri tuu leo ajira imekuwa ngumu hata kwa chuo kikuu. Kulinganisha uwiano ukiwa na elemu ya chuo kikuuu mtazamo wangu unatakiwa uwe mfikirivu hata utengeneza ajira kwa watu mia tano kwa upeo wao wa elimu. Nilisikitika sana pale prof Baregu akililia kuajiriwa na udsm wakati yeye ana uwezo kama wa Prof Kairuki akaanzisha chuo. mawazo yetu yamejikita kuwanyanyapaa wenye elimu ndogo huku sisi tukijifanya wafikirivu wakubwa( greater thinker) wakati akili zetu zimejaa zarau sisizo na kikomo kwa ambao hawajabahatika ni hii elimu. Taifa linatutegemea tushikamane na tuachee hii tabiia ya kuwakudharau viumbe wengine wa Mungu, najua heshima mnatoa kulingana na CV ya mtu na zarau pia mnatoa kwa wenye cv ya darasa la saba. Ndoto yangu Tanzania yenye kuajiri kuanzia elimu ya msingi na inatoa nafasi na muongozo mwepesi kwa yeyote mwenye kutaka kujiendeleza.
 
Back
Top Bottom