nnunu
JF-Expert Member
- Mar 4, 2011
- 654
- 230
NINA RAFIKI YANGU WA KIKE NI MFANYAKAZI ANAOMBA USHAURI KATIKA HILI.
ANA RAFIKI YAKE WA KIUME WANA UHUSIANO KWA MUDA WA MIAKA 9. SASA HIVI MWANAUME ANAMWOMBA AMUOE , ILA MWANAMKE AMEKATAA NA AMEMWAMBIA SABABU YA KUKATAA, ILA JAMAA AMEMWAMBIA BADO ANAMPA MUDA WA KUFIKIRIA ZAIDI LABDA ANAWEZA KUBADILISHA MSIMAMO AKAKUBALI KUOLEWA NAYE. MWANAMKE ANASITA KUtokana na uchoyo na ubahili wa mwanaume,ameshindwa kubadilika miaka 9 je kweli ataweza kubadilika wakiwa ndoani?.
NI MCHOYO SANA AU MBAHILI KUPITA KIASI.
Tangu waanze uhusiano wao mwanaume hajawahi kumtoa out mwanamke, japo mwanamke ana tabia ya kumtoa out mwanaume, amemwambia kuhusu hili lakin mwanaume anamwahidi kuwa asiwe na hofu ipo siku na yeye atamtoa na hasa watakapooana.Hajawahi kumnunulia zawadi yoyote japo huyu msichana anajitahidi kumnunulia zawadi huyo mpenzi wake. Hajawahi kupewa japo shilingi ya matumizi,ila huyu msichana mara chache huwa anampa, akimuuliza kwa nini hampi mwanaume anamjibu ampe pesa ya nini na yeye anajiweza kwa kila kitu. Ikitokea huyu dada anaumwa mwanaume atakuja kumwangalia hata mara 10 kwa siku lakin bila hata tunda wala huduma yoyote zaidi ya neno nakupenda mpenzi wangu upone haraka. Akiombwa ampeleke mahali na gari anakubali bila matatizo lakin lazima mwanamke ajaze mafuta kwenye gari,mwanamke anaweka na safari inaendeka,mwanamke asipoweka mafuta safari haiendeki.Kukiwa na tatizo lolote mwanaume ni mwepesi kuwepo lakin hachangii gharama yoyote inayohusiana na pesa.
Mwanaume ana kazi tena inayomwingizia pesa nzuri tu, anaishi kwenye nyumba aliyoijenga mwenyewe,ana gari na anajiweza kwa kila kitu, ndugu zake anawahudumia bila matatizo yoyote. Matatizo yote haya amemwambia lakin majibu anayompa ni kuwa huduma zote hizo atampa atakapomwoa.Kuna mwaka alimkopa pesa kabla ya kumkopesha alimuuliza atamlipa lini ,mwanamke alimwambia tarehe ya kumpa,mkopo alipewa ilipofika tu tarehe jamaa alimkumbusha tena asubuhi, mwanamke jion alipotoka ofisini alimlipa.Pia mwanamke aliwahi kuibiwa na wezi vitu vingi sana nyumbani kwake,akaanza upya kununua vitu alivyoibiwa, jamaa hakuchangia hata senti moja zaidi alitoa pole tu kwa mpenzi.Mwanamke alijinunulia kila kitu na mapenzi yao yaliendelea kama kawaida.
Kuna kipindi Ikabidi mwanamke amwambie MAMA WA MWANAUME(Mkwe) ili ajaribu kuongea na mwanaye, Mama mkwe alimjibu kuwa huyu mtoto amerithi tabia ya Baba yake kwani hata yeye hajawahi kununuliwa kitu chochote au kupewa pesa na mumewe tangu waoane na mpaka muda huu wanaanza kuzeeka. Kazi ya baba ni kutoa ada tu ya shule,lakin majukumu mengine anayatoa mama.Jibu hili lilimkatisha tamaa sana, ksb yeye upande wake anawaona wazazi wake wanashirikiana kwa kila jambo.
Mwanaume ameahidi kumfanyia yote watakapooAna lakin huyu dada moyo unamsita ksb anahisi maisha yao yatakuwa kama ya wakwe zake, mwanaume anaweza kumwachia majukumu yote ya nyumbani na familia kwa kisingizi kuwa mwanamke si anajiweza (ana kipato cha kumtosheleza). Huyu dada anaona hawezi kuishi na mume wa aina hii ksb ikitokea hana kazi,anaumwa hajiwezi kabisa kungiza kipato maisha si yatamwelemea,pia hana uhakika kama kweli huyo boyfriend wake atabadilika na kuanza kumhudumia.
Kumpenda anampenda na huyu mwanaume ana tabia zingine nzuri na hasa 6 kwa 6 anamridhisha 100% lakin UCHOYO NA UBAHILI umepita kiwango.
JE AMEFANYA MAKOSA KUKATAA KUOLEWA NA HUYU MWANAUME?? UPENDO SI NI KUTOA NA KUPOKEA? UPENDO GANI WA KUPOKEA TU?, HIVI NI KWELI KUWA MWANAMKE ANAYEJIWEZA KIUCHUMI HATAKIWI KUHUDUMIWA NA BOYFRIEND / MUME WAKE??.
SAMAHANI KWA MAELEZO MAREFU NAOMBA UVUMILIVU WENU.
NAOMBA USHAURI WANA JF.
ANA RAFIKI YAKE WA KIUME WANA UHUSIANO KWA MUDA WA MIAKA 9. SASA HIVI MWANAUME ANAMWOMBA AMUOE , ILA MWANAMKE AMEKATAA NA AMEMWAMBIA SABABU YA KUKATAA, ILA JAMAA AMEMWAMBIA BADO ANAMPA MUDA WA KUFIKIRIA ZAIDI LABDA ANAWEZA KUBADILISHA MSIMAMO AKAKUBALI KUOLEWA NAYE. MWANAMKE ANASITA KUtokana na uchoyo na ubahili wa mwanaume,ameshindwa kubadilika miaka 9 je kweli ataweza kubadilika wakiwa ndoani?.
NI MCHOYO SANA AU MBAHILI KUPITA KIASI.
Tangu waanze uhusiano wao mwanaume hajawahi kumtoa out mwanamke, japo mwanamke ana tabia ya kumtoa out mwanaume, amemwambia kuhusu hili lakin mwanaume anamwahidi kuwa asiwe na hofu ipo siku na yeye atamtoa na hasa watakapooana.Hajawahi kumnunulia zawadi yoyote japo huyu msichana anajitahidi kumnunulia zawadi huyo mpenzi wake. Hajawahi kupewa japo shilingi ya matumizi,ila huyu msichana mara chache huwa anampa, akimuuliza kwa nini hampi mwanaume anamjibu ampe pesa ya nini na yeye anajiweza kwa kila kitu. Ikitokea huyu dada anaumwa mwanaume atakuja kumwangalia hata mara 10 kwa siku lakin bila hata tunda wala huduma yoyote zaidi ya neno nakupenda mpenzi wangu upone haraka. Akiombwa ampeleke mahali na gari anakubali bila matatizo lakin lazima mwanamke ajaze mafuta kwenye gari,mwanamke anaweka na safari inaendeka,mwanamke asipoweka mafuta safari haiendeki.Kukiwa na tatizo lolote mwanaume ni mwepesi kuwepo lakin hachangii gharama yoyote inayohusiana na pesa.
Mwanaume ana kazi tena inayomwingizia pesa nzuri tu, anaishi kwenye nyumba aliyoijenga mwenyewe,ana gari na anajiweza kwa kila kitu, ndugu zake anawahudumia bila matatizo yoyote. Matatizo yote haya amemwambia lakin majibu anayompa ni kuwa huduma zote hizo atampa atakapomwoa.Kuna mwaka alimkopa pesa kabla ya kumkopesha alimuuliza atamlipa lini ,mwanamke alimwambia tarehe ya kumpa,mkopo alipewa ilipofika tu tarehe jamaa alimkumbusha tena asubuhi, mwanamke jion alipotoka ofisini alimlipa.Pia mwanamke aliwahi kuibiwa na wezi vitu vingi sana nyumbani kwake,akaanza upya kununua vitu alivyoibiwa, jamaa hakuchangia hata senti moja zaidi alitoa pole tu kwa mpenzi.Mwanamke alijinunulia kila kitu na mapenzi yao yaliendelea kama kawaida.
Kuna kipindi Ikabidi mwanamke amwambie MAMA WA MWANAUME(Mkwe) ili ajaribu kuongea na mwanaye, Mama mkwe alimjibu kuwa huyu mtoto amerithi tabia ya Baba yake kwani hata yeye hajawahi kununuliwa kitu chochote au kupewa pesa na mumewe tangu waoane na mpaka muda huu wanaanza kuzeeka. Kazi ya baba ni kutoa ada tu ya shule,lakin majukumu mengine anayatoa mama.Jibu hili lilimkatisha tamaa sana, ksb yeye upande wake anawaona wazazi wake wanashirikiana kwa kila jambo.
Mwanaume ameahidi kumfanyia yote watakapooAna lakin huyu dada moyo unamsita ksb anahisi maisha yao yatakuwa kama ya wakwe zake, mwanaume anaweza kumwachia majukumu yote ya nyumbani na familia kwa kisingizi kuwa mwanamke si anajiweza (ana kipato cha kumtosheleza). Huyu dada anaona hawezi kuishi na mume wa aina hii ksb ikitokea hana kazi,anaumwa hajiwezi kabisa kungiza kipato maisha si yatamwelemea,pia hana uhakika kama kweli huyo boyfriend wake atabadilika na kuanza kumhudumia.
Kumpenda anampenda na huyu mwanaume ana tabia zingine nzuri na hasa 6 kwa 6 anamridhisha 100% lakin UCHOYO NA UBAHILI umepita kiwango.
JE AMEFANYA MAKOSA KUKATAA KUOLEWA NA HUYU MWANAUME?? UPENDO SI NI KUTOA NA KUPOKEA? UPENDO GANI WA KUPOKEA TU?, HIVI NI KWELI KUWA MWANAMKE ANAYEJIWEZA KIUCHUMI HATAKIWI KUHUDUMIWA NA BOYFRIEND / MUME WAKE??.
SAMAHANI KWA MAELEZO MAREFU NAOMBA UVUMILIVU WENU.
NAOMBA USHAURI WANA JF.