..nimestaajabu kusikia haya.
..je Butiama ilistahili maendeleo yote haya?
..tukihalalisha alichofanya Mwalimu kwa Butiama, tutaweza kuharamisha anachofanya Kikwete kwao Lugoba?
..hili hapa chini lina chembe-chembe za ukabila.
..ninavyoelewa Mwalimu siku zote alisisitiza Utaifa/U-Tanzania.
..je, katika faragha alitukuza ukabila/Uzanaki? hebu soma hapa chini??
..HABARI NZIMA INAPATIKANA TOKA GAZETI LA RAIA MWEMA. BONYEZA HAPA
..je Butiama ilistahili maendeleo yote haya?
..tukihalalisha alichofanya Mwalimu kwa Butiama, tutaweza kuharamisha anachofanya Kikwete kwao Lugoba?
Jackton Manyerere said:Butiama, enzi za Mwalimu, ilikwisha kuwa na benki mbili, karakana kubwa katika Kanda ya Ziwa, matrekta na malori visivyo idadi, ng'ombe walikamuliwa kwa mashine, ilikwisha kuwa na viwanda vya kushona nguo na useremala; wanafunzi walishonewa sare na kupewa bure, madawati yalizidi mahitaji, maji kila mtaa, umeme, huduma za posta na simu, na kila kilichotakikana katika maisha ya msingi ya binadamu, vyote vilipatikana Butiama.
..hili hapa chini lina chembe-chembe za ukabila.
..ninavyoelewa Mwalimu siku zote alisisitiza Utaifa/U-Tanzania.
..je, katika faragha alitukuza ukabila/Uzanaki? hebu soma hapa chini??
Mzee Lucas Nyerere said:"Miaka yote kulikuwapo minong'ono ya chini kwa chini, watu wakipendekeza Butiama pawe makao makuu ya wilaya, lakini Mwalimu alikataa. Alikataa kwa hoja kuwa ukisha kuifanya Butiama kuwa Wilaya, maana yake ni kwamba uhalisia na ukweli kuhusu historia ya kijiji hicho kwa Tanzania , Afrika na dunia yote, vitapotea.
"Pia Mwalimu alipinga kwa sababu alisema kwa kuifanya Butiama kuwa Wilaya, ‘kikabila kidogo' cha Wazanaki kitapotea. Lakini kubwa aliloamini Mwalimu ni kwamba Butiama ibaki kijiji ili kulinda historia yake,"
..HABARI NZIMA INAPATIKANA TOKA GAZETI LA RAIA MWEMA. BONYEZA HAPA
Last edited: