Je Muungano Ukifa Na CCM Itakufa?

Mar 25, 2011
28
6
Napenda kuwauliza WanaCCM wote bara na Visiwani, Je Muungano ukifa na CCM itakufa? Kwani chanzo cha CCM ni Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Muungano wa Vyama vya siasa kati ya TANU na ASP, Kwa Hiyo Kufa kwa Muungano ni Kufa kwa CCM na Kuwepo kwa CCM ni kuwepo kwa CCM
 
Hapana haiwezi kufa ila ikishindwa katika uchaguzi ujao wa 2015 basi itakufa na wao wanalijua hili ndio sababu kubwa ya kufanya hata ugaidi, kutaka kuchakachua katiba mpya, kutumia vyombo vya dola kutesa, kupiga na hata kuwaua wafuasi wa CHADEMA ili kuhakikisha wanapunguza speed ya CHADEMA au kuisambaratisha kabisa. Mie si mwanaCCM ni CHADEMA wa kutupa.
 
CCM ilishakufa zamani.

Hii CCM unayoiona leo ipo,inaendelea kuwepo kutokana na kubebwa na Tume ya Uchaguzi(ushindi wa kishindo). CCM inabebwa na vyombo vya dola.

Mkulu alishasema kuwa CCM inabebwa na Jeshi la polisi.

CCM inabebwa na ile idara nyeti pia.

CCM ilishakufa, Siku "vyombo vya dola" vikiacha kutumika kama vyombo vya CCM, vikiamua kuzima mashine ya "life support". CCM itazikwa rasmi.

CCM uionayo ni maigizo tu.
 
Hapana haiwezi kufa ila ikishindwa katika uchaguzi ujao wa 2015 basi itakufa na wao wanalijua hili ndio sababu kubwa ya kufanya hata ugaidi, kutaka kuchakachua katiba mpya, kutumia vyombo vya dola kutesa, kupiga na hata kuwaua wafuasi wa CHADEMA ili kuhakikisha wanapunguza speed ya CHADEMA au kuisambaratisha kabisa. Mie si mwanaCCM ni CHADEMA wa kutupa.

Je nini itakuwa hatima ya CCM iwapo Itashindwa katika Uchanguzi mkuu wa uraisi wa JMT hapo 2015, harafu ama CCM au CUF ikishinda Katika Uchaguzi wa Tanzania VIsiwani?
 
Je nini itakuwa hatima ya CCM iwapo Itashindwa katika Uchanguzi mkuu wa uraisi wa JMT hapo 2015, harafu ama CCM au CUF ikishinda Katika Uchaguzi wa Tanzania VIsiwani?

Hivi visiwa ni Mafia na Ukerewe?

Usijaribu kulichakachua jina Tanzania.
Ukitumia Tanzania,maana yake ni Tanganyika na Zanzibar.

Ninyi kwa usanii wenu ndio mmetupotezea jina letu la Tanganyika.
 
Back
Top Bottom