Je, Mungu ndiye aliyeumba dhambi?

Nami naomba nichangie katika hili. Dhambi si kitu useme imeumbwa na Mungu, dhambi ni hali ambayo inamfanya mwanadamu ajiweke mbali na Mungu kutokana na mawazo yake, matendo yake, na ata maneno yake wakati mwingine. Kama ilivyo mbingu si sehemu bali ni hali ya kuwa katika ukalibu na Mungu. Vitabu vya dini vipo wazi sana shida yetu tulio wengi tunasoma " literally " . Mungu amemuumba binadamu na malaika wakiwa huru kama ishara ya upendo kwa viumbe vyake, maana pasipo Uhuru akuna upendo na Uhuru bila nidhamu utupeleka upotovuni ndio maana Mungu akaluhusu viumbe vikose vikiamua lakini alishawajuza maana ndani ya mioyo yetu Mungu mwenyewe ameweka sheria zake. Shida walioipata malaika ndio tuipatayo wanadamu kukataa kuwa viumbe na kutaka kuwa Mungu, ukijichubguza vyema utaona ndani yako kuna maelekeo au matamanio ya wewe kuwa Mungu wa maisha yako. Kifo kinachozungumziwa kwenye maandiko matakatifu sio physical death bali ni spiritual death na ndio maana Adam na Eva walipo kula tunda ( walipo asi ) walijihisi kuwa mbali na Mungu that we call physical death. So in any way we can not escap physical death.
 
Nami naomba nichangie katika hili. Dhambi si kitu useme imeumbwa na Mungu, dhambi ni hali ambayo inamfanya mwanadamu ajiweke mbali na Mungu kutokana na mawazo yake, matendo yake, na ata maneno yake wakati mwingine. Kama ilivyo mbingu si sehemu bali ni hali ya kuwa katika ukalibu na Mungu. Vitabu vya dini vipo wazi sana shida yetu tulio wengi tunasoma " literally " . Mungu amemuumba binadamu na malaika wakiwa huru kama ishara ya upendo kwa viumbe vyake, maana pasipo Uhuru akuna upendo na Uhuru bila nidhamu utupeleka upotovuni ndio maana Mungu akaluhusu viumbe vikose vikiamua lakini alishawajuza maana ndani ya mioyo yetu Mungu mwenyewe ameweka sheria zake. Shida walioipata malaika ndio tuipatayo wanadamu kukataa kuwa viumbe na kutaka kuwa Mungu, ukijichubguza vyema utaona ndani yako kuna maelekeo au matamanio ya wewe kuwa Mungu wa maisha yako. Kifo kinachozungumziwa kwenye maandiko matakatifu sio physical death bali ni spiritual death na ndio maana Adam na Eva walipo kula tunda ( walipo asi ) walijihisi kuwa mbali na Mungu that we call physical death. So in any way we can not escap physical death.
Good

Sent using Jamii Forums mobile app
 
As Christian nijuavyo dhambi ni uasi uasi ni kwenda kinyume /against God sasa kwanin shetan alitoka wapi ...? One thing Shetan ni jina la laana kabla hapo alkua lusfa... Lusifa then shetan huyu hakwenda against sheria za Mungu bali kutak utawala kabisaa yaani kumpindua Mungu utawala wake apa sasa ndio matokeo ya kulaaniwa lusfa adi shetan lakin haya yote before creating earth and human being so binadam anakuj kuumbwa kwa mfano wa Mungu lakin tiar shetan ameshaadhibiwa ni suala la muda tuu everything is over
What's the main causative of sins?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulitumia logic, "Mungu ni Muumba wa vyote" dhambi ikiwemo. Jibu ni ndio isiyokuwa na mashaka. Hakuna free Will!!
 
Umekusanya dini zote kwenye kapu moja ila hoja zako umejenga kwenye msingi wa mafundisho ya biblia pekee.

Hili jambo linafanywa sana humu sijui ni kwanini?
Amefanya hivyo huenda ni kwasababu anaona biblia ndiyo kitabu ambacho yamkini amewahi kusoma maandiko yake mara kadhaa, ko wewe jibu hoja kwa jinsi ulivyoielewa usione kama ni mbaguzi, hapana, wewe jibu hoja ulizozielewa!
 
Kwani kama ana mamlaka, lazima atumie nguvu nyingi kutonyesha kuwa ana mamlaka?

Ni sawa na mwalimu mkuu, wanafunzi tunajua yeye ndio head teacher, lakini anatumia nguvu nyingi ili kutufanya tuamini bila yeye hakuna tena. Kama kweli ni mwalimu mkuu, kuna ulazima gani yeye kutumia nguvu nyingi.

That's what God has been doing, katumia nguvu nyingi ili tu tuamini bila yeye hakuna.

Na kwa nini tuokoke?
Kwani alivyotuumba haikutosha kufanya tumfate?

Kuna sehemu anasema, "walio wangu nawajua"... hivi kumbe kuna watu tunapoteza muda tu, Mungu anawajua watu wake. Kwanini atubague wakati yeye ndio katuumba?
Mkuu hii hoja imenichekesha sana 😂😂
 
Kwani kama ana mamlaka, lazima atumie nguvu nyingi kutonyesha kuwa ana mamlaka?

Ni sawa na mwalimu mkuu, wanafunzi tunajua yeye ndio head teacher, lakini anatumia nguvu nyingi ili kutufanya tuamini bila yeye hakuna tena. Kama kweli ni mwalimu mkuu, kuna ulazima gani yeye kutumia nguvu nyingi.

That's what God has been doing, katumia nguvu nyingi ili tu tuamini bila yeye hakuna.

Na kwa nini tuokoke?
Kwani alivyotuumba haikutosha kufanya tumfate?

Kuna sehemu anasema, "walio wangu nawajua"... hivi kumbe kuna watu tunapoteza muda tu, Mungu anawajua watu wake. Kwanini atubague wakati yeye ndio katuumba?
Mkuu hii hoja imenichekesha sana 😂😂
 
Amefanya hivyo huenda ni kwasababu anaona biblia ndiyo kitabu ambacho yamkini amewahi kusoma maandiko yake mara kadhaa, ko wewe jibu hoja kwa jinsi ulivyoielewa usione kama ni mbaguzi, hapana, wewe jibu hoja ulizozielewa!
Hakika mkuu
 
Wakuu hamjambo!

Kama kichwa cha Uzi huu kinavyouliza, Mimi nikiri kuwa naamini uwepo wa Mungu mmoja aliyeumba vyote vinavyoonekana na visivyoonekana pia.

Katika vitabu mbali mbali vya dini, tunaelezwa kuwa dhambi ilitokana na uasi alioufanya shetani dhidi ya Mungu, biblia inaenda mbali kwa kudai kuwa vita vilipiganwa huko mbinguni na shetani alishindwa na akatupwa duniani akiwa na theluthi ya malaika wakawa upande wake.

Maswali:

1. Ikiwa kabla ya shetani kuasi hakukuwa na dhambi yoyote ile, tena alikuwa mbinguni kwenye utakatifu wa MUNGU, je shetani alishawishiwa au alitoa wapi mawazo ya uasi Ikiwa hakukuwa na shetani yeyote mwingine?

2. Kama MUNGU hujua mwanzo hata mwisho wa viumbe vyake, INA maana alikuwa anajua kuwa shetani atakuja kuasi baadae na kusababisha dhambi, kwanini alimuumba?
Jambo la kufikiria hapa ni kuona kwamba MUNGU alimuumba shetani/Lucifer ( dhambi) mahususi ili kuja kuwa upande maovu. Dhana hii inadhihirisha kuwa MUNGU ndie aliyeumba dhambi.

3. Je, lengo la MUNGU lilikuwa mwanadamu aishi milele bila kufa?
Hapa kuna mazoea yalishajengeka hasa kwa wakristo na waislamu kuamini kuwa isingekuwa Eva/Hawa kudanganywa na Shetani basi Leo hii wanadamu wasingekuwa wanakufa ( immortal). Hii dhana haina mantiki hasa ukiwaza kuwa wanadamu wangezaliana na kuishi milele bila kufa nadhani dunia ingekuwa imejaa mabara na visiwa vyote.
Hivyo MUNGU akaamua kuleta mauti ili kudhibiti ( control) idadi ya wanadamu duniani isizidi uwezo wa rasilimali zilizopo, fikiri Leo hii watu wanauwana kugombania ardhi je ingekuwaje akina Adam na bibi yetu Eva wangekuwepo wote?

4. Je, Dini ni matokeo ya mwanadamu kumhofia shetani?
Tunaishi katika jamii ambazo kila MTU ana juhudi za kujikwamua kuondokana na shida Kama magonjwa, njaa, vita, ambazo Mara nyingi wanadamu wanahesabu kuwa hayo yote ni sababu ya shetani, na dini wanaona ndio kimbilio ili kumkwepa shetani asiwadhuru.
Lakini wao wanaamini kuwa wanasali ili kumtukuza MUNGU, lakini kiukweli dini ni hofu ( fear of unknown) isiyo na ithibati yoyote.

5. Je, Mungu anawapenda wanadamu? Hapa jibu laweza kuwa ni ndiyo, bahati mbaya sana ukiangalia uhalisia toka zamani kuna ugumu wa kusema ndiyo au hapana.
Tunaambiwa kuwa mbinguni kulikuwa na vita Kali sana, mwaishowe malaika aitwaye Mikaeli alimshinda shetani, Mungu akamtupa ibilisi huyo huyo duniani kwa wanadamu anaowapenda sana. Mungu hakuona sehemu nyingine ya kulitupa hilo joka ila duniani ambako ndio wanadamu aliwaweka. Hii ni sawa na kuwarushia watoto wako furushi lenye nge wengi huku umewafungia chumbani na kuwataka wajikinge wasing'atwe hata kidogo.

Nimekuja kuamini kuwa: MUNGU yupo ila dini zote ni michezo ya kukamata fikra za wanadamu tu, inawezekana kabisa kuwa dini ziluletwa na shetani mwenyewe ili kuwachonganisha wanadamu wasiishi kwa upendo na amani.
Angalia jinsi Palestine na Israel, syria , Iraq n.k wanavyouana kwa misingi ya dini.

Niishie hapo, naomba waumini/maswahaba mje mtueleze hizi hoja.

Cc: Mshana Jr
Cc: Kiranga
Na wanajamvi wote karibuni.
Sisi wayahudi tunaamini mungu ana pande mbili, hasi na chanya,, vyote kaumba yeye, mema na mabaya,,, hata bible imeeleza wazi, God created evil
 
Sawa mkuu, nikuulize hivi!
Je, unaweza kutenda dhambi pasipo kushawishiwa na shetani?

Kwa Maelezo yako, MUNGU siyo kisababishi cha dhambi?
Jiulize iwapo MUNGU asingemuumba shetani dhambi ingetoka wapi?

Mtiririko ni kama huu:-

MUNGU > Shetani> dhambi.

Ukimuondoa MUNGU kwenye huo mlinganyo INA maana dhambi isingekuwepo,
Na ujue kwa mujibu waa biblia, shetani hukutana na kujadiliana mambo mbalimbali na mungu, ikiwemo kuwajaribu watu, rejea kipindi shetani anamjaribu yesu,, au yule jamaa aliefiwa na family yote na akabaki masikini hohe hohe,,,,
 
Dhambi ni nini? Shetani ni nini na baraka ni nini?

Mtu anaweza kuniambia kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani,kuvuka barabara na gari wakati taa nyekundu imekuwakia usimame, ni dhambi, kwa muktadha wa sheria za usalama barabarani.

Hilo siwezi kukataa.

Mtu anaweza kusema, Assad aliyeua Wa-Syria wengi sana, ni shetani, kwa maana ya kwamba shetani ni mtu anayeua watu wengi sana.

Kwa muktadha huo Assad anaweza kuwa Shetani.

Mtu anaweza kuniambia, mvua kunyesha ni baraka, inaleta neema kwao. Kwa muktadha huo siwezi kupinga.

Unaposema dhambi, Shetani na baraka unaamanisha nini?
Shetàni hauwi,, hana huo uwezo, kila mtu amepangiwa atakufaje kwa mujibu wa maandiko,, shetani hana kosa lolote,,
In short hakuna shetani
 
Na ujue kwa mujibu waa biblia, shetani hukutana na kujadiliana mambo mbalimbali na mungu, ikiwemo kuwajaribu watu, rejea kipindi shetani anamjaribu yesu,, au yule jamaa aliefiwa na family yote na akabaki masikini hohe hohe,,,,
Manaake Mungu huruhusu majaribu kwa makusudi fulani.
 
Maandiko gani Sakayo, binafsi nakuwa na maswali hadi naacha nisije kusema neno zito.

Mungu alifarakanisha mataifa, ili yapigane watu wafe. Mungu gani afanye hivyo watu wafe?

Kumbuka safari ya waisraeli toka Misiri kwenda Kaanani, watu wengi walikufa kabla ya kufika huko, Kweli Mungu anapenda watu wake wafe?

Herode mfalme, aliuwa watoto wachanga sana, huyo Mungu alikuwa wapi aache vichanga vife?

Why? Why?
Maandiko yanadai, mungu aliufanya moyo wa farao kuwa mgumu ili asiwatoe waisrael ili mungu apate kuwauwa wamisri,,
Mungu huyo huyo alimnyatia moses, akiruka mashonde hapa na pale na akimvizia kumuua moses,, hatimae mungu akamkaba kabali ya nguvu moses akitaka kumtoa roho,,
Kama si mke wa moses kuwahi kumkata govi mtoto wa moses, sàa hizi tungekuwa tunaongea habari nyingine kabisa
 
Halafu ujue hawa wawili wanakutana sana, tangu shetani afukuzwe huko juu.

~Walikutana kipindi Ayoub anataka kujaribiwa, wakakubaliana kuwa Ayoub ajaribiwe tu ila asiuwawe...WALIKUBALIANA.

~Walikutana tena Yesu alipokuwa akijaribiwa huko nyikani, ila Yesu akamfukuza baada ya shetani kufanya mzaha na utani.

Kumbe bwana wanakutana na kukubaliana kabisa...Dah!!
Ndio
 
Kwanza mtoa hoja lazima ujue Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakob, Mussa na Elia ndiyo Mungu mkuu, LAKINI kuna MIUNGU mingine.

Na ndiyo maana katika amri 10 aliyopewa Mussa pale mlima Sinai amri ya kwanza kabisa inasema hivi " Usiwe na miungu mingine ila mimi tu"

Kwa hiyo kuwekana sawa katika mjadala huu tujue kwamba Mungu Mwenyezi alijua kuna Miungu wengine ambao wana nguvu pia.

Kwa hiyo bali ulimwengu huu uliumbwa ukiwa na Miungu wengi naMalaika wengi.
 
Kwanza mtoa hoja lazima ujue Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakob, Mussa na Elia ndiyo Mungu mkuu, LAKINI kuna MIUNGU mingine.

Na ndiyo maana katika amri 10 aliyopewa Mussa pale mlima Sinai amri ya kwanza kabisa inasema hivi " Usiwe na miungu mingine ila mimi tu"

Kwa hiyo kuwekana sawa katika mjadala huu tujue kwamba Mungu Mwenyezi alijua kuna Miungu wengine ambao wana nguvu pia.

Kwa hiyo bali ulimwengu huu uliumbwa ukiwa na Miungu wengi naMalaika wengi.
Focus ya mjadala ipo kwa Mungu mkuu
 
Focus ya mjadala ipo kwa Mungu mkuu
yes ni kweli, ila tujue pia ulimwengu hu una sheria zake hivyo overall si Mungu huyu Mkuu kufanya kila jambo atakalo hapana ni lazima afuate sheria za uumbaji wa ulimwengu.

Na ndiyo maana ilikuwa hamna namna ya ondoleo la dhambi la ulimwengu bila Yesu Kristo kufa msalabani - Swali je Mungu kwa nini aliruhusu hilo? hakukuwa na njia nyingine sababu yeye ni muweza wa yote?

Jibu: Ulimwengu una Sheria na Mungu pamoja na uweza wake hataki kuziruka ni lazima zifuatwe.

Kwa hiyo Dhambi ni zao la Miungu mingine kujaribu kupambana na Mungu Mkuu, maana sisi wanadamu tumeumbwa kwa mfano wa Mungu Mkuu, sasa miungu mingine inajaribu kuturubuni ili tumchukie muumba wetu na tuiabudu yenyewe.

Hii miungu ina nguvu pia, jiulize mchawi anaruka angani ama anaingia kwako usiku wakati mlango umefungwa, Je hiyo nguvu anapata wapi?
 
Back
Top Bottom