Je, Mungu ndiye aliyeumba dhambi?

Saguda47

JF-Expert Member
May 1, 2016
10,738
18,484
Wakuu hamjambo!

Kama kichwa cha Uzi huu kinavyouliza, Mimi nikiri kuwa naamini uwepo wa Mungu mmoja aliyeumba vyote vinavyoonekana na visivyoonekana pia.

Katika vitabu mbali mbali vya dini, tunaelezwa kuwa dhambi ilitokana na uasi alioufanya shetani dhidi ya Mungu, biblia inaenda mbali kwa kudai kuwa vita vilipiganwa huko mbinguni na shetani alishindwa na akatupwa duniani akiwa na theluthi ya malaika wakawa upande wake.

Maswali:

1. Ikiwa kabla ya shetani kuasi hakukuwa na dhambi yoyote ile, tena alikuwa mbinguni kwenye utakatifu wa MUNGU, je shetani alishawishiwa au alitoa wapi mawazo ya uasi Ikiwa hakukuwa na shetani yeyote mwingine?

2. Kama MUNGU hujua mwanzo hata mwisho wa viumbe vyake, INA maana alikuwa anajua kuwa shetani atakuja kuasi baadae na kusababisha dhambi, kwanini alimuumba?
Jambo la kufikiria hapa ni kuona kwamba MUNGU alimuumba shetani/Lucifer ( dhambi) mahususi ili kuja kuwa upande maovu. Dhana hii inadhihirisha kuwa MUNGU ndie aliyeumba dhambi.

3. Je, lengo la MUNGU lilikuwa mwanadamu aishi milele bila kufa?
Hapa kuna mazoea yalishajengeka hasa kwa wakristo na waislamu kuamini kuwa isingekuwa Eva/Hawa kudanganywa na Shetani basi Leo hii wanadamu wasingekuwa wanakufa ( immortal). Hii dhana haina mantiki hasa ukiwaza kuwa wanadamu wangezaliana na kuishi milele bila kufa nadhani dunia ingekuwa imejaa mabara na visiwa vyote.
Hivyo MUNGU akaamua kuleta mauti ili kudhibiti ( control) idadi ya wanadamu duniani isizidi uwezo wa rasilimali zilizopo, fikiri Leo hii watu wanauwana kugombania ardhi je ingekuwaje akina Adam na bibi yetu Eva wangekuwepo wote?

4. Je, Dini ni matokeo ya mwanadamu kumhofia shetani?
Tunaishi katika jamii ambazo kila MTU ana juhudi za kujikwamua kuondokana na shida Kama magonjwa, njaa, vita, ambazo Mara nyingi wanadamu wanahesabu kuwa hayo yote ni sababu ya shetani, na dini wanaona ndio kimbilio ili kumkwepa shetani asiwadhuru.
Lakini wao wanaamini kuwa wanasali ili kumtukuza MUNGU, lakini kiukweli dini ni hofu ( fear of unknown) isiyo na ithibati yoyote.

5. Je, Mungu anawapenda wanadamu? Hapa jibu laweza kuwa ni ndiyo, bahati mbaya sana ukiangalia uhalisia toka zamani kuna ugumu wa kusema ndiyo au hapana.
Tunaambiwa kuwa mbinguni kulikuwa na vita Kali sana, mwaishowe malaika aitwaye Mikaeli alimshinda shetani, Mungu akamtupa ibilisi huyo huyo duniani kwa wanadamu anaowapenda sana. Mungu hakuona sehemu nyingine ya kulitupa hilo joka ila duniani ambako ndio wanadamu aliwaweka. Hii ni sawa na kuwarushia watoto wako furushi lenye nge wengi huku umewafungia chumbani na kuwataka wajikinge wasing'atwe hata kidogo.

Nimekuja kuamini kuwa: MUNGU yupo ila dini zote ni michezo ya kukamata fikra za wanadamu tu, inawezekana kabisa kuwa dini ziluletwa na shetani mwenyewe ili kuwachonganisha wanadamu wasiishi kwa upendo na amani.
Angalia jinsi Palestine na Israel, syria , Iraq n.k wanavyouana kwa misingi ya dini.

Niishie hapo, naomba waumini/maswahaba mje mtueleze hizi hoja.

Cc: Mshana Jr
Cc: Kiranga
Na wanajamvi wote karibuni.
 
NDIYO na SIYO..!

Najua hutaelewa maana kichwa chako kitakuwa kidogo. Iko hivi Mungu ni chanzo cha kila kitu hapa duniani na mbinguni ila sasa kwasababu na makusudi maalum.

Kitalaam( sheria&law philosophy) waliosoma criminology wanajua kuwa ni sheria tu, inayoweza kuunda/kuumba kosa. Kwa msingi huo nasema dhambi ni kosa au crime kwa Mungu na hakuna dhambi ambayo haivunji AMRI/SHERIA ZA Mungu rejea vitabu vya sheria ya Musa(vitabu vitano vya mwanzo katika agano jipya).

Pili siyo Mungu aliyeumba dhambi Mungu kaumba sheria na kuziwekea utaratibu wa kuzitekeleza siye tunaozivunja ndiyo waumba dhambi, ingawa Shetani anasingiziwa kila kukicha.

Bila shaka nimejibu kwa ufupi.
 
NDIYO na SIYO..!

Najua hutaelewa maana kichwa chako kitakuwa kidogo. Iko hivi Mungu ni chanzo cha kila kitu hapa duniani na mbinguni ila sasa kwasababu na makusudi maalum.

Kitalaam( sheria&law philosophy) waliosoma criminology wanajua kuwa ni sheria tu, inayoweza kuunda/kuumba kosa. Kwa msingi huo nasema dhambi ni kosa au crime kwa Mungu na hakuna dhambi ambayo haivunji AMRI/SHERIA ZA Mungu rejea vitabu vya sheria ya Musa(vitabu vitano vya mwanzo katika agano jipya).

Pili siyo Mungu aliyeumba dhambi Mungu kaumba sheria na kuziwekea utaratibu wa kuzitekeleza siye tunaozivunja ndiyo waumba dhambi, ingawa Shetani anasingiziwa kila kukicha.

Bila shaka nimejibu kwa ufupi.
Sawa mkuu, nikuulize hivi!
Je, unaweza kutenda dhambi pasipo kushawishiwa na shetani?

Kwa Maelezo yako, MUNGU siyo kisababishi cha dhambi?
Jiulize iwapo MUNGU asingemuumba shetani dhambi ingetoka wapi?

Mtiririko ni kama huu:-

MUNGU > Shetani> dhambi.

Ukimuondoa MUNGU kwenye huo mlinganyo INA maana dhambi isingekuwepo,
 
Mungu umsemae hapo anasifa za uovu na wema,hebu fikiri kwanini alimfanya farao kuwa mkaidi halafu akamuangamiza..? kama sivyo basi Mungu huyo atakuwa si muweza wa kila kitu!,kuna vitu ameshindwa kuviangamiza!,maana kama shetani anasababisha dhambi kwa wanadamu hlf anamuangalia kama pambo chumbani basi hata yeye anahatia na wadhambi hao! wengine humsema Mungu ndo mpangaji wa yote!,hivyo kauli hii humaanisha kuna watu amewapangia waende motoni na wengine peponi! anasifa ya ubaguzi wa hali ya juu..
 
Mungu umsemae hapo anasifa za uovu na wema,hebu fikiri kwanini alimfanya farao kuwa mkaidi halafu akamuangamiza..? kama sivyo basi Mungu huyo atakuwa si muweza wa kila kitu!,kuna vitu ameshindwa kuviangamiza!,maana kama shetani anasababisha dhambi kwa wanadamu hlf anamuangalia kama pambo chumbani basi hata yeye anahatia na wadhambi hao! wengine humsema Mungu ndo mpangaji wa yote!,hivyo kauli hii humaanisha kuna watu amewapangia waende motoni na wengine peponi! anasifa ya ubaguzi wa hali ya juu..
Kweli kabisa mkuu, MUNGU anafanya lolote atakalo yeye, Lowe jema ama baya.
 
Kabla ya kuendelea naomba uniambie kuwa unaamini kuwa dhambi, Shetani, na baraka zipo?
Dhambi ni nini? Shetani ni nini na baraka ni nini?

Mtu anaweza kuniambia kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani,kuvuka barabara na gari wakati taa nyekundu imekuwakia usimame, ni dhambi, kwa muktadha wa sheria za usalama barabarani.

Hilo siwezi kukataa.

Mtu anaweza kusema, Assad aliyeua Wa-Syria wengi sana, ni shetani, kwa maana ya kwamba shetani ni mtu anayeua watu wengi sana.

Kwa muktadha huo Assad anaweza kuwa Shetani.

Mtu anaweza kuniambia, mvua kunyesha ni baraka, inaleta neema kwao. Kwa muktadha huo siwezi kupinga.

Unaposema dhambi, Shetani na baraka unaamanisha nini?
 
Sawa mkuu, nikuulize hivi!
Je, unaweza kutenda dhambi pasipo kushawishiwa na shetani?

Kwa Maelezo yako, MUNGU siyo kisababishi cha dhambi?
Jiulize iwapo MUNGU asingemuumba shetani dhambi ingetoka wapi?

Mtiririko ni kama huu:-

MUNGU > Shetani> dhambi.

Ukimuondoa MUNGU kwenye huo mlinganyo INA maana dhambi isingekuwepo,
Katika quraani
Allah subhana wataallah anasema.
SHETANI NI KATIKA BINADAMU NA MAJINI.
Hivyo binadam anaweza kutenda dhambi pasipo jini kushiriki(ambae hapa anatumika kama shetani).hivyo unaweza kufanya dhambi kubwa hadi yule shetani mwenyewe akakupenda
 
Wakuu hamjambo!

Kama kichwa cha Uzi huu kinavyouliza, Mimi nikiri kuwa naamini uwepo wa Mungu mmoja aliyeumba vyote vinavyoonekana na visivyoonekana pia.

Katika vitabu mbali mbali vya dini, tunaelezwa kuwa dhambi ilitokana na uasi alioufanya shetani dhidi ya Mungu, biblia inaenda mbali kwa kudai kuwa vita vilipiganwa huko mbinguni na shetani alishindwa na akatupwa duniani akiwa na theluthi ya malaika wakawa upande wake.

Maswali:

1. Ikiwa kabla ya shetani kuasi hakukuwa na dhambi yoyote ile, tena alikuwa mbinguni kwenye utakatifu wa MUNGU, je shetani alishawishiwa au alitoa wapi mawazo ya uasi Ikiwa hakukuwa na shetani yeyote mwingine?

2. Kama MUNGU hujua mwanzo hata mwisho wa viumbe vyake, INA maana alikuwa anajua kuwa shetani atakuja kuasi baadae na kusababisha dhambi, kwanini alimuumba?
Jambo la kufikiria hapa ni kuona kwamba MUNGU alimuumba shetani/Lucifer ( dhambi) mahususi ili kuja kuwa upande maovu. Dhana hii inadhihirisha kuwa MUNGU ndie aliyeumba dhambi.

3. Je, lengo la MUNGU lilikuwa mwanadamu aishi milele bila kufa?
Hapa kuna mazoea yalishajengeka hasa kwa wakristo na waislamu kuamini kuwa isingekuwa Eva/Hawa kudanganywa na Shetani basi Leo hii wanadamu wasingekuwa wanakufa ( immortal). Hii dhana haina mantiki hasa ukiwaza kuwa wanadamu wangezaliana na kuishi milele bila kufa nadhani dunia ingekuwa imejaa mabara na visiwa vyote.
Hivyo MUNGU akaamua kuleta mauti ili kudhibiti ( control) idadi ya wanadamu duniani isizidi uwezo wa rasilimali zilizopo, fikiri Leo hii watu wanauwana kugombania ardhi je ingekuwaje akina Adam na bibi yetu Eva wangekuwepo wote?

4. Je, Dini ni matokeo ya mwanadamu kumhofia shetani?
Tunaishi katika jamii ambazo kila MTU ana juhudi za kujikwamua kuondokana na shida Kama magonjwa, njaa, vita, ambazo Mara nyingi wanadamu wanahesabu kuwa hayo yote ni sababu ya shetani, na dini wanaona ndio kimbilio ili kumkwepa shetani asiwadhuru.
Lakini wao wanaamini kuwa wanasali ili kumtukuza MUNGU, lakini kiukweli dini ni hofu ( fear of unknown) isiyo na ithibati yoyote.

5. Je, Mungu anawapenda wanadamu? Hapa jibu laweza kuwa ni ndiyo, bahati mbaya sana ukiangalia uhalisia toka zamani kuna ugumu wa kusema ndiyo au hapana.
Tunaambiwa kuwa mbinguni kulikuwa na vita Kali sana, mwaishowe malaika aitwaye Mikaeli alimshinda shetani, Mungu akamtupa ibilisi huyo huyo duniani kwa wanadamu anaowapenda sana. Mungu hakuona sehemu nyingine ya kulitupa hilo joka ila duniani ambako ndio wanadamu aliwaweka. Hii ni sawa na kuwarushia watoto wako furushi lenye nge wengi huku umewafungia chumbani na kuwataka wajikinge wasing'atwe hata kidogo.

Nimekuja kuamini kuwa: MUNGU yupo ila dini zote ni michezo ya kukamata fikra za wanadamu tu, inawezekana kabisa kuwa dini ziluletwa na shetani mwenyewe ili kuwachonganisha wanadamu wasiishi kwa upendo na amani.
Angalia jinsi Palestine na Israel, syria , Iraq n.k wanavyouana kwa misingi ya dini.

Niishie hapo, naomba waumini/maswahaba mje mtueleze hizi hoja.

Cc: Mshana Jr
Cc: Kiranga
Na wanajamvi wote karibuni.


He/ She wanted/wants life to be very very interesting not boring.
Imagine life without evil, good things, ups and downs, happiness and sorrow, birth and death.
Muhimu kuliko yote inasemekana aliwapa wanadamu uwezo wa kujua na kuchagua kati ya mema na mabaya.
 
Kama kweli Mungu alimaliza kuumba, kila alichoumba aliona ni chema kabisa. Hakukuwa na uasi juu ya uso wa dunia, Lucifer alikuwa msafi, asiye na dhambi.

~Nani alimuingia Lucifer aliyekuwa anaishi patakatifu ili aasi?

~Kama kweli Mungu ni alpha na omega, maana yake alijua kuwa dhambi itaingia ulimwenguni, kwa nini aliruhusu hiyo dhambi iingie?

~Kwa wakristo, kabla ya Yesu kuja kutufia, walikuwa wakiteteteza sadaka(kondoo) ili kusamehewa dhambi zao, kwa nini kondoo aliye mnyama wa kawaida auwawe kila siku ili tu mimi nisamehewe?

~Mungu mwenye rehema, upendo kwa nini aruhusu mwanadamu aishi maisha ya dhiki kiasi hiki? Maradhi, kifo, vita nk.

Why?
Why?
Why?
 
Kama kweli Mungu alimaliza kuumba, kila alichoumba aliona ni chema kabisa. Hakukuwa na uasi juu ya uso wa dunia, Lucifer alikuwa msafi, asiye na dhambi.

~Nani alimuingia Lucifer aliyekuwa anaishi patakatifu ili aasi?

~Kama kweli Mungu ni alpha na omega, maana yake alijua kuwa dhambi itaingia ulimwenguni, kwa nini aliruhusu hiyo dhambi iingie?

~Kwa wakristo, kabla ya Yesu kuja kutufia, walikuwa wakiteteteza sadaka(kondoo) ili kusamehewa dhambi zao, kwa nini kondoo aliye mnyama wa kawaida auwawe kila siku ili tu mimi nisamehewe?

~Mungu mwenye rehema, upendo kwa nini aruhusu mwanadamu aishi maisha ya dhiki kiasi hiki? Maradhi, kifo, vita nk.

Why?
Why?
Why?
Ili maandiko yatimie
 
Mbona mnamsemea huyo kuliko kujisemea yeye mwenyewe kama kweli yupo?

Hayupo ndyo maana mnamsemea.
 
NDIYO na SIYO..!

Najua hutaelewa maana kichwa chako kitakuwa kidogo. Iko hivi Mungu ni chanzo cha kila kitu hapa duniani na mbinguni ila sasa kwasababu na makusudi maalum.

Kitalaam( sheria&law philosophy) waliosoma criminology wanajua kuwa ni sheria tu, inayoweza kuunda/kuumba kosa. Kwa msingi huo nasema dhambi ni kosa au crime kwa Mungu na hakuna dhambi ambayo haivunji AMRI/SHERIA ZA Mungu rejea vitabu vya sheria ya Musa(vitabu vitano vya mwanzo katika agano jipya).

Pili siyo Mungu aliyeumba dhambi Mungu kaumba sheria na kuziwekea utaratibu wa kuzitekeleza siye tunaozivunja ndiyo waumba dhambi, ingawa Shetani anasingiziwa kila kukicha.

Bila shaka nimejibu kwa ufupi.
Umemuelewa vizuri jamaa?

Usijibu kwa kukurupuka
 
31 Reactions
Reply
Back
Top Bottom