Je, Mtoto wa kambo ana haki ya kurithi mali?

Kitakachouua wewe ni mkeo, mume aliyezaa naye na huyo mtoto wa kambo.

Mtoto msomeshe hujui kesho yake.

Mali hauondoki nazo, wagawie watoto wote sawa,

Mkeo naye ana haki hata kama alivikuta, si anakupikia, kukufulia, kuzaa, kukuandalia hata maji uoge, naye mgawie.

Ila, ikitokea umetangulia kufa hao wanao wako taabuni.

Hakuna mtoto mbaya kuliko mtoto wa kambo japo siyo wote...
Wanawake mnateteana kwa sababu mnayajua madhambi yenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je, mkeo ni wa ndoa? ndoa inatambulika kwa kuwa na cheti cha ndoa. Lakini linapokuja suala la maamuzi na kama umezaa nae mahakama huchukulia kama mke (ila sio hata km umezaa nae watoto 100) ili iamue kesi.

Lakini urithi kwa mtoto wa kambo ni maamuz yak sheria inakutaka wewe uamue umpe au uache.

Pia unaweza ksema ulipomsomesha ndo urith wak .sheria haikulazimishi.lkn pia sheria inaangalia km bdo atahitaj umtunze wewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili swali mi pia huwa najiuliza sana,humu labda ntapata majibu

Sent using Jamii Forums mobile app
Itapendeza kama wanasheria watatupa michango yao katika hili. Sema kwa uelewa wangu ni unaweza kurithi au la, matokeo yatatokana na mkataba wenu Wa ndoa( Pre nup).

Hakuna kitu kinasikitisha kama kuhangaika kutafuta Mali alafu mwanamke anakuja kuchukua kilaini kisa you are ignorant to the law. Kama upo serious na pesa, you must protect your assets legally.
 
Sheria ya ndoa ina ruhusu wanandoa kumiliki mali binafsi.kwa mfano kabla ya ndo mwanandoa alikuwa na nyumba yake hiyo haitabadilika na kuwa mali ya wote pindi watakapofunga ndoa!ila mali zilizotafutwa baada ya ndoa zitahesabika kama mali za wote!...
Kumbe hata mwanaume ana haki na Mali alizotafuta mwanamke baada ya ndoa ,so mkiachana mnagawana zote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hmm!!

Yaani ukute mtu tayari ana mali zake halafu mkishaoana nawe unakuwa haki ya kila kitu ulichokikuta?

Where dey do dat at?

Coz that right there is some next level fuckery.
 
Hivi siku hizi akili zinauzwa ghali sana kiasi kwamba wengine tunashindwa kununua? Mbona majibu yako wazi?!!! Mtoto wa kambo anamrithi MAMA YAKE MZAZI na sio baba wa kambo. Sehemu ya urithi atakayopata mama ndiyo atamgawia mwanaye huyo...
Mkuu ngoja nichomekee kiswali, umesema mtoto wa kambo atarithi kwa mama yake. je mfano x, mama yake kaolewa na k. akazaliwa z so, x ni mtoto wa kambo kwa k, bahati mbaya mama yake x kafariki, na z pia kafariki. je huyu x atawezaje kudai urithi kwa bwana k?
 
Najibu hapo mwisho kwenye mchango wa mwanamke. Mke wako ana haki na mali zako hata kama amezikuta.. mchango wake sio lazima uwe pesa..Kama anatekeleza majukumu ya kulea familia na kukutunza huo ni mchango tosha. Haki anayo kama hajakiuka mambo mengine ya mahusiano yenu...
Hongereni, mimi siwezi kabisa, nikigundua anawasiliana na x biashara imekwisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria za mirathi ni copy and paste za sheria za India..

So mtoto wa nje hapati urithi unless familia imeridhia

there is no such thing as "familia kuridhia mtoto wa nje" kwenye Indian Succession Law.

Kwenye mirathi isiyo na wosia familia inakaa kuridhia jambo moja tu: msimamizi wa mirathi awe nani.

Baada ya hapo Msimamizi atafuata kikokotoo cha kisheria kugawa mali. Mwanaharamu hatambuliki na sheria ya Tanzania iliyotoka India bali watoto halali na mjane.

Kwa upande wa mirathi yenye wosia, mchakato ni tofauti: mwenye mali anaweza kuandika chochote ikiwemo kuwapiga chini watoto halali, haramu, mke, ndugu, na kuamua kuipa hela yake Halmashauri ijenge hospitali, au kuacha imtunze mbwa wake aliyekuwa nae pembeni ya kitanda mpaka anakufa.
 
Najibu hapo mwisho kwenye mchango wa mwanamke. Mke wako ana haki na mali zako hata kama amezikuta.. mchango wake sio lazima uwe pesa..Kama anatekeleza majukumu ya kulea familia na kukutunza huo ni mchango tosha. Haki anayo kama hajakiuka mambo mengine ya mahusiano yenu...
Pole sana mkuu
 
Najibu hapo mwisho kwenye mchango wa mwanamke. Mke wako ana haki na mali zako hata kama amezikuta.. mchango wake sio lazima uwe pesa..Kama anatekeleza majukumu ya kulea familia na kukutunza huo ni mchango tosha. Haki anayo kama hajakiuka mambo mengine ya mahusiano yenu.

Kuhusu mtoto wa kambo subiri wanasheria wabobezi waje. Ila mtoto kufahamu baba yake mzazi ni Jambo la kheri..sema bidada kakiuka makubaliano yenu...

Mtoto alijuaje huyo anayemlea sio baba kama wewe hukumwambia?
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom