Je, Msajili wa Vyama vya siasa alikaa lini na IGP akaambiwa kuna kikao?

Utaanzaje kumhoji mtu aliyeshika silaha na anakulazimisha umtii?
Wananchi sio wajinga.
Ukimtesa mtu unatesa na mke wake, watoto wake, na ndugu zake wasio na hatia.
Hawa wanaotesa wenzao ndiyo hawatumii akili, sio wananchi wasio na hatia ambao baadhi ni 'malaika' wasiojua hata kusema.

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
Kwa hiyo kwa maoni yako suluhu ni kukubali kuendelea "kulazimishwa kutii" milele?
Ingekuwa hivyo si basi tungekuwa bado wakoloni tunao hapa au?
 
Siyo kosa Lao au lrtu Bali ni ukosefu wa elimi ya uraia. Muulize Anna Tibaijuka wakati ule alipoanzisha bawata, na kutaka Kuanzisha Elimu ya uraia. Kilichofuata ni nini?. Hakika tuna safari ngumu na ndefu. Wengine wanajita ni mamba na safari haiwahusu Bali ni ya kenge pekee mwisho wa siku mamba wanageuka kuwa kenge na wenyewe.
Mkuu, ninachojua ni kwamba hakuna jambo linalodumu milele.

CCM wamejiwekea mazingira ya kujiondoa madarakani. Kama hapatatokea watu wachache waliosalia huko ndani ya chama hicho wakachukua hatua haraka na kubadili mwenendo wa chama ulivyo sasa, uhai wa chama hicho utakuwa unaelekea ukingoni.
 
kuhusu uhuru muda wa wakoloni kutawala uliisha kulingana na mikataba ya kimataifa, ndiyo maana unaona hakuna nchi inayotawaliwa tena. Kati ya wote Madela pekee yake ndiyo alipata shida wengine utadanganywa
Nimekusoma mara kadhaa humu ukirudiarudia upuuzi huu kiasi kwamba sasa unajiona bingwa juu yake na kuendelea kueneza upumbavu ukidhani wewe ni mjuaji sana.
Ngoja nikuachie hapa ujitafakari kwanza. Ukiwa na akili nzuri utaona upotofu mkubwa katika dhana hii ya kipuuzi kabisa.
 
Kwa upande wangu nakiona ni kikao muhimu sn sababu watakaoendelea kuumia ni vyama vya upinzani, Sirro ana mabomu, risasi, mahabusu na mahakama ndiyo kinachompa kiburi, vita yoyote ile humalizwa kwa mazungumzo.
Mkuu tatizo haliko Kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na Vyama vyenyewe wala Kwa IGP Bali tatizo kuu liko kwenye TAMKO la M/Kiti wa CCM Taifa. Yeye ndiye angeitwa na Msajili kulitolea ufafanuzi tamko lake. Nchi hii bila Katiba Mpya Rais ataendelea kutumia Mamlaka yake vibaya kukinufaisha Chama chake Huku akiwaumiza wengine.
 
Mkuu tatizo haliko Kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na Vyama vyenyewe wala Kwa IGP Bali tatizo kuu liko kwenye TAMKO la M/Kiti wa CCM Taifa. Yeye ndiye angeitwa na Msajili kulitolea ufafanuzi tamko lake. Nchi hii bila Katiba Mpya Rais ataendelea kutumia Mamlaka yake vibaya kukinufaisha Chama chake Huku akiwaumiza wengine.
Hawezi kumuita sababu ni mamlaka yake ya uteuzi
 
Nimekusoma mara kadhaa humu ukirudiarudia upuuzi huu kiasi kwamba sasa unajiona bingwa juu yake na kuendelea kueneza upumbavu ukidhani wewe ni mjuaji sana.
Ngoja nikuachie hapa ujitafakari kwanza. Ukiwa na akili nzuri utaona upotofu mkubwa katika dhana hii ya kipuuzi kabisa.
Mpuuzi wewe utanisaidia nini? baki na shida zako huko
 
Back
Top Bottom