Je, moto wa ajabu ardhini rombo ni dalili za kulipuka volcano iliyolala ya mlima Kilimanjaro?

Wanasayansi wa bongo ni bure kabisa yaani ni empty set ,jana maTV yote yameonyesha kwamba wamegundua mifupa ya mjusi iliyoishi miaka milioni 160 hahaaaaa ukiangalia hiyo mifupa ni kama jiwe lilitokana na zege,mfupa ukae miaka milioni 160 halafu utoke kama jiwe hahahaaaa nonsense.

Hapo wakija wazungu hapo rombo watatoa report sahihi lakini hao ma geologist wabongo wanaenda kupiga perdiem tu.
Hiyo mifupa inashangaza hapo tumepigwa taarifa gongana hile

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ramli tu Kaka. Wataanza kusema mara carbon 14 na utumbo mwingine mwingi wa kutughiribu tuwaone Wana akili wakati ndio haohao wanaoamini mwenge unaleta amani vitani
Nitakujibu la mwenge, mwenge hutumika tu kama ishara na alama, ni kama Roman catholic wanavyofanyaga njia ya msalaba ni kuyaenzi yale tunayoyaamini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkubwa andiko lako ni zuri, ila unajichanganya katika miaka. Unasema mlima ulitokea miaka 1000 iliyopita. Baadae unasema tena Mawezi ilitokea miaka millioni kadhaa iliyopita. Kisha unasema tena Kibo iliacha kurusha volcano miaka 200,000 na kitu iliyo pita. Kwenye miaka zingatia kuangalia wapi kuna makosa.
Lakini hata mie uwa nawasiwasi sana, nahisi ipo siku mlima kilimanjaro utalipuka volcano ya sasa haifiki nje, lakini kuna siku itafika! Mie si mwana sayansi lkn kuna siku jambo litatokea.
 
Hadithi kama hii inafanana na ile wanayosema zanzibar kuna siku itazama this depend to its foundations
 
Hayo mambo ya miaka Laki , mara milioni. Mie wala hayaniingii akilini.
Kwa mujibu wa Biblia dunia imeishi miaka takribani elfu 6. Kadri muda unavyendelea inazidi kuchakaa na kuwayawaya.
 
Wanasayansi wa bongo ni bure kabisa yaani ni empty set ,jana maTV yote yameonyesha kwamba wamegundua mifupa ya mjusi iliyoishi miaka milioni 160 hahaaaaa ukiangalia hiyo mifupa ni kama jiwe lilitokana na zege,mfupa ukae miaka milioni 160 halafu utoke kama jiwe hahahaaaa nonsense.

Hapo wakija wazungu hapo rombo watatoa report sahihi lakini hao ma geologist wabongo wanaenda kupiga perdiem tu.
Wamesema ule moto umesababishwa na takataka zilizofukiwa chini, huyu mtoa mada hafatilii media
 
Mkubwa andiko lako ni zuri, ila unajichanganya katika miaka. Unasema mlima ulitokea miaka 1000 iliyopita. Baadae unasema tena Mawezi ilitokea miaka millioni kadhaa iliyopita. Kisha unasema tena Kibo iliacha kurusha volcano miaka 200,000 na kitu iliyo pita. Kwenye miaka zingatia kuangalia wapi kuna makosa.
Lakini hata mie uwa nawasiwasi sana, nahisi ipo siku mlima kilimanjaro utalipuka volcano ya sasa haifiki nje, lakini kuna siku itafika! Mie si mwana sayansi lkn kuna siku jambo litatokea.
Kweli mkubwa nilikosea na nimeshasahihisha, badala ya miaka milioni moja niliandika elfu moja. Ingawa namimi pia si mwanasayansi mbobevu lakini hebu ngoja kwa uelewa kidogo nilio nao nijaribu kuweka vizuri hapa: Tangu kilele cha kwanza (Shira cone) kuanza kufoka wanakadiria ni miaka milioni 2.4 mpaka 3.5 iliyopita. Baadae tena miaka milioni moja(1.0) shira kilizimika vikajitokeza viotea vingine viwili ambavyo ni Kibo na Mawenzi. Viliendelea kufoka mpaka kufikia miaka 450,000(laki nne na nusu) ambapo Mawenzi kilizimika na kuacha kufoka(volcano mfu) huku Kibo kikiendelea kufoka mpaka hivi karibuni kabisa miaka 200,000(laki mbili) nacho kikasimama kwa muda kama volcano iliyolala. Kwa ujumla tangu vilele vyote kuanza mpaka sasa hivi inakadiriwa ni miaka zaidi ya milioni 2.5 na tokea mlipuko wa hivi karibuni kabisa kutokea inakisiwa ni miaka laki mbili(200,000)
 
Ngoja tuendelee kufanya tafuti, ivi iyo mifupa haikuwa jivu baada ya volcano kulipuka Mana napata mashaka kuhusu carbon14
 
Wamesema ule moto umesababishwa na takataka zilizofukiwa chini, huyu mtoa mada hafatilii media
Ni jambo la kheri mkuu ikiwa mboji itakuwa ndiyo chanzo cha huu moto na wala si volcano kama nilivyohisi maanake kwa vyovyote vile ikiwa ni mboji itazimika tu pindi mvua zikinyesha au mbolea ikiteketea yote kwa moto. Lakini niulize wadau wengine hali kama hiyo ya mboji kuwaka imewahi kutokea mahali pengine hata nje ya Tanzania na mifano ikarekodiwa? basi mwenye taarifa japo atujuze tupate kujua zaidi tafadhali.
 
Ngoja tuendelee kufanya tafuti, ivi iyo mifupa haikuwa jivu baada ya volcano kulipuka Mana napata mashaka kuhusu carbon14
Hata ikiwa jivu Watafiti wanachotafuta ni viasili vya Carbon itokanayo na kiumbe hai kilichokufa, hayohayo majivu wanaweza wakayatumia kama sampuli katika utafiti. Pia kiumbe hai si lazima kiwe ni mifupa ya binadamu au wanyama pekee bali hata miti na manyasi vinaweza kutumika. Uji wa volcano unapofunika mahali masalia ya viumbe hai yanaweza yasiungue moja kwa moja kutegemeana na ni kitu gani kilikuwa juu ya hayo masalia. Mfano ikiwa pengine yalikingwa na utando mwingine wa udongo au tabaka la takataka za viumbe wengine wafu kuna uwezekano baada ya miaka mingi ukaja kuzikuta hazijaharibika kwa chochote
 
Kwa wakaazi wa Wilaya ya Rombo na maeneo mengine yote kuuzunguka mlima Kilimanjaro chochote kinachotokea kuhusiana na Mlima huu ni lazima kiwaguse moja kwa moja kutokana na maisha yao kutegemea miteremko yake kwa maelefu ya miaka iliyopita. Ingawa uwezekano wa Volcano ya mlima huu kulipuka wanasayansi wanasema ni mdogo sana lakini bado wanasisitiza kwamba ni jambo linaloweza siku moja kuja kutokea kutokana na sababu kwamba volcano yake imelala tu na si kama imekufa kabisa.

Mlima mrefu kuliko yote Afrika Kilimanjaro(Kibo) ni mlima uliotokea Duniani baada ya mlipuko wa Volcano chini ya ardhi yapata miaka zaidi ya 1,000,000 hivi iliyopita. Ukiwa na vilele duara 3 (cones), Shira, Kibo na Mawenzi, kila kimoja kilijitengeneza kwa wakati wake huku Shira(kilele-mama) kikiwa ndicho kilichoanza kutokea yapata miaka zaidi ya mlioni 2.5 iliyopita kisha kikaja kuzimika kabisa (kufa) na kuzuka Mawenzi na Kibo vilivyoanza wakati mmoja miaka 1,000,000 iliyopita.

Kufikia miaka 450,000 iliyopita kilele cha Mawenzi kilisimama kabisa kurusha volcano na kuwa volcano mfu pia(iliyokufa) huku Kibo kikiendelea kurusha volcano yake mpaka ilipofika miaka 150,000 hadi 200,000 iliyopita ambapo nacho kilisimama lakini kwa muda tu siyo kufa kabisa kama wenzake Mawenzi na Shira. Hii inamaanisha kwamba kuna uwezekano siku yeyote ile Kibo kikaja kuanza tena kulipuka na kurusha volcano na majivu ya moto.

Kwa mujibu wa Wataalamu wa mambo ya miamba(geologists) Mlima Kilimanajaro na milima mingine ya kivolcano iliyopo Africa Mashariki kama mlima Kenya, mlima Meru, Mlima Elgon, Ol Doinyo Lengai, Dalafilla, longonot, mlima Nyiragongo pamoja na Maziwa mbalimbali kama vile ziwa Victoria, Nyasa, Tanganyika, Turkana nk. ingawa si vyote vipo ndani ya bomde la ufa lakini vyote ni matokeo ya shughuli za kivolcano zilizosababishwa na mpasuko wa umbo la nje la ardhi ya dunia ( tectonic plates) ambazo kila moja hujivuta kutoka kwa mwenzake na kusababisha Bonde kubwa la ufa kutokea katikati.

Mpasuko huo umesababisha baadhi ya maeneo kuwa dhaifu hivyo kusababisha eneo la ndani kabisa la Dunia ambalo kimsingi huwa na joto kali sana kupitisha uji-uji wenye mchanganyiko wa madini mbalimbali na miamba nje ya uso wa dunia(volcano). Uji huu ndio husababisha milima kama Kilimanjaro kutokea taratibu baada ya maelfu ya miaka kupita ukitiririka. Bonde la ufa limeanzia huko Ethiopia mpaka Msumbiji likipitia nchi za Somalia, Kenya, Uganda, Burundi, rwanda, Malawi na Zambia.

Katika eneo ulipozuka mlima Kilimanjaro na kwa kuwa bado shughuli za kivolcano bado zinaendelea chini ya ardhi hasa ukanda mzima wa Bonde la Ufa la Afrika Mashariki basi kuibuka kwa hali kama tunayoishuhudia Rombo yawezekana isiwe ni jambo la ajabu sana. Eneo tukio la Rombo lilipotokea si mbali na ulipo Mlima Kilimanjaro.


VIASHIRIA VINGINE.

ZIWA CHALA

Ziwa chala ni moja kati ya “vijitoto” vilivyotokana na volcano iliyounda mlima Kilimanjaro, ni ziwa lililopo Wilayani Rombo na linakadiriwa kutokea muda sawa na kilele cha Kibo miaka takriban 200,000 ilyopita. Utafiti uliofanyika kwenye ziwa hilo kwa kuchunguza matabaka ya mlundikano wa majivu ya volcano (tephra layers) ndio uliothibitisha muda halisi wa kutokea kwa mlipuko wa mwisho kiasi cha mikaka 150,000 hadi 200,000 tofauti na jinsi ilivyodhaniwa kabla kwamba ni mamilioni ya mika mingi iliyopita. Hivyo unaweza kuona miaka 200 elfu si mingi sana katika umri wa kijiolojia.

Mpaka sasa hivi hata watu wanaopanda mpaka kufika kilele cha Uhuru wanaweza kuhisi harufu ya gesi za salphur kutokea katika Crater ya mlima Kilimanjaro pale juu kabisa, ishara kwamba bado kuna shughuli za kivolkano bado zinaendelea chini ya mlima huu lakini kwa kiwango cha chini (under low pressure) kiasi majivu na uji wa miamba haviwezi kuruka umbali mrefu

Binafsi mimi (Haya ni maoni yangu lakini) nimefikiria moto wa Rombo labda inawezekana ikawa ni moja kati ya viotea vya mlima Kilimanjaro (monogenetic parasitic eruption associated with Mt Kilimanjaro) mfano wa ziwa chala na vilele vingine mfano kama ilivyotokea mawenzi na Kibo baada ya Shira, ingawa hivi vya sasa vyaweza kuwa na athari ndogo sana na vinavyoisha muda mfupi tu vikiwa na majivu ya udongo wa moto badala ya volcano na uji mzito wa miamba ya chuma shauri ya presha ndogo iliyopo ardhini kwa sasa.

Katika maeneo mengine Afrika Mashariki katika ukanda wa Bonde la Ufa kumewahi kuripotiwa moto wa ardhini ingawa sifikirii kama unafanana kabisa na huu wa Rombo. Huko Kenya mpaka wamefikia hatua ya kufua umeme kwa kutumia moto kama huu (Geothermal energy). Katika maeneo mengine duniani mfano katika msitu wa Amazon nimewahi kusoma kuna eneo fulani pana mto wa maji moto yanayochemka, nadhani pengine inaweza kuwa ni kitu kama hikihiki kilichotokea Rombo.


MATETEMEKO YA ARDHI


Bado Rombo na maeneo mengine kando kando ya Kilimanjaro kuna nyakati hutokea matetemeko ya ardhi, ishara nyingine kwamba shughuli za kivolcano chini ya eneo zima na ukanda wa bonde la ufa la Afrika Mashariki bado zinaendelea. Tetemeko la ardhi la mwisho lilitokea Rombo mwaka jana.

Tafiti nyingi sana zimeshafanyika na wanasayansi kuhusiana na uwezekano wa kulipuka tena kwa mlima Kilimanjaro, unaweza kutafuta “google’ na kuona ingawa karibu kila mtafiti anasema kwamba hamna uwezekano mkubwa wa mlima huo kulipuka tena hivi karibuni na hata yawezekana kilele cha Kibo kikaja kufa kabisa kama wenzake Shira na Mawenzi. Hili lakini halina uhakika kwa asilimia mia moja.

Wakaazi wa Kilimanjaro tukio kama hili la Rombo halipaswi kutupa taharuki, badala yake tutulie tukichukua tahadhari pamoja na ushauri serikali itakaoutoa baada ya Wataalamu wake kumaliza uchunguzi.

Ingawa Wataalamu wengi wameshafanya tafiti mbalimbali na kuthibitisha volcano ya mlima Kilimanjaro kutokuweza kulipuka hivi karibuni na hata hivyo kungelikuwa na viashiria vikubwa zaidi kama matetemeko na gesi nyingi kuonekana katika crater ya Kibo. Mabadiliko makubwa ya kijiolojia huchukua mamilioni ya miaka hivyo ukilinganisha na umri wa vizazi vyetu usiozidi hata miaka 100 unaweza kuona ni sawa tu na tone dogo sana la maji baharini.

Hata hivyo serikali ina wajibu wataalamu wake kuchunguza na kutoa maelezo ya uhakika zaidi kwetu wananchi ikiwa ni pamoja na tahadhari za kuchukua ikiwa kama kuna hatari zozote zile zinazoweza kuambatana na mabadiliko ya kijiolojia hata kama yatakuwa ni madogo kama haya ya Rombo ili kuepusha Wananchi kuingia taharuki au kwenye imani zingine potofu mfano za ushirikina nk.
View attachment 1960785
Makala hii imeandikwa na mtafiti wa masuala ya kijamii kwa msaada wa vyanzo mbalimbali mtandaoni.
….. walishangilia/kusherehekea kifo cha rais wet mzalendo Dkt Magufuli.
 
Kwa wakaazi wa Wilaya ya Rombo na maeneo mengine yote kuuzunguka mlima Kilimanjaro chochote kinachotokea kuhusiana na Mlima huu ni lazima kiwaguse moja kwa moja kutokana na maisha yao kutegemea miteremko yake kwa maelefu ya miaka iliyopita. Ingawa uwezekano wa Volcano ya mlima huu kulipuka wanasayansi wanasema ni mdogo sana lakini bado wanasisitiza kwamba ni jambo linaloweza siku moja kuja kutokea kutokana na sababu kwamba volcano yake imelala tu na si kama imekufa kabisa.

Mlima mrefu kuliko yote Afrika Kilimanjaro(Kibo) ni mlima uliotokea Duniani baada ya mlipuko wa Volcano chini ya ardhi yapata miaka zaidi ya 1,000,000 hivi iliyopita. Ukiwa na vilele duara 3 (cones), Shira, Kibo na Mawenzi, kila kimoja kilijitengeneza kwa wakati wake huku Shira(kilele-mama) kikiwa ndicho kilichoanza kutokea yapata miaka zaidi ya mlioni 2.5 iliyopita kisha kikaja kuzimika kabisa (kufa) na kuzuka Mawenzi na Kibo vilivyoanza wakati mmoja miaka 1,000,000 iliyopita.

Kufikia miaka 450,000 iliyopita kilele cha Mawenzi kilisimama kabisa kurusha volcano na kuwa volcano mfu pia(iliyokufa) huku Kibo kikiendelea kurusha volcano yake mpaka ilipofika miaka 150,000 hadi 200,000 iliyopita ambapo nacho kilisimama lakini kwa muda tu siyo kufa kabisa kama wenzake Mawenzi na Shira. Hii inamaanisha kwamba kuna uwezekano siku yeyote ile Kibo kikaja kuanza tena kulipuka na kurusha volcano na majivu ya moto.

Kwa mujibu wa Wataalamu wa mambo ya miamba(geologists) Mlima Kilimanajaro na milima mingine ya kivolcano iliyopo Africa Mashariki kama mlima Kenya, mlima Meru, Mlima Elgon, Ol Doinyo Lengai, Dalafilla, longonot, mlima Nyiragongo pamoja na Maziwa mbalimbali kama vile ziwa Victoria, Nyasa, Tanganyika, Turkana nk. ingawa si vyote vipo ndani ya bomde la ufa lakini vyote ni matokeo ya shughuli za kivolcano zilizosababishwa na mpasuko wa umbo la nje la ardhi ya dunia ( tectonic plates) ambazo kila moja hujivuta kutoka kwa mwenzake na kusababisha Bonde kubwa la ufa kutokea katikati.

Mpasuko huo umesababisha baadhi ya maeneo kuwa dhaifu hivyo kusababisha eneo la ndani kabisa la Dunia ambalo kimsingi huwa na joto kali sana kupitisha uji-uji wenye mchanganyiko wa madini mbalimbali na miamba nje ya uso wa dunia(volcano). Uji huu ndio husababisha milima kama Kilimanjaro kutokea taratibu baada ya maelfu ya miaka kupita ukitiririka. Bonde la ufa limeanzia huko Ethiopia mpaka Msumbiji likipitia nchi za Somalia, Kenya, Uganda, Burundi, rwanda, Malawi na Zambia.

Katika eneo ulipozuka mlima Kilimanjaro na kwa kuwa bado shughuli za kivolcano bado zinaendelea chini ya ardhi hasa ukanda mzima wa Bonde la Ufa la Afrika Mashariki basi kuibuka kwa hali kama tunayoishuhudia Rombo yawezekana isiwe ni jambo la ajabu sana. Eneo tukio la Rombo lilipotokea si mbali na ulipo Mlima Kilimanjaro.


VIASHIRIA VINGINE.

ZIWA CHALA

Ziwa chala ni moja kati ya “vijitoto” vilivyotokana na volcano iliyounda mlima Kilimanjaro, ni ziwa lililopo Wilayani Rombo na linakadiriwa kutokea muda sawa na kilele cha Kibo miaka takriban 200,000 ilyopita. Utafiti uliofanyika kwenye ziwa hilo kwa kuchunguza matabaka ya mlundikano wa majivu ya volcano (tephra layers) ndio uliothibitisha muda halisi wa kutokea kwa mlipuko wa mwisho kiasi cha mikaka 150,000 hadi 200,000 tofauti na jinsi ilivyodhaniwa kabla kwamba ni mamilioni ya mika mingi iliyopita. Hivyo unaweza kuona miaka 200 elfu si mingi sana katika umri wa kijiolojia.

Mpaka sasa hivi hata watu wanaopanda mpaka kufika kilele cha Uhuru wanaweza kuhisi harufu ya gesi za salphur kutokea katika Crater ya mlima Kilimanjaro pale juu kabisa, ishara kwamba bado kuna shughuli za kivolkano bado zinaendelea chini ya mlima huu lakini kwa kiwango cha chini (under low pressure) kiasi majivu na uji wa miamba haviwezi kuruka umbali mrefu

Binafsi mimi (Haya ni maoni yangu lakini) nimefikiria moto wa Rombo labda inawezekana ikawa ni moja kati ya viotea vya mlima Kilimanjaro (monogenetic parasitic eruption associated with Mt Kilimanjaro) mfano wa ziwa chala na vilele vingine mfano kama ilivyotokea mawenzi na Kibo baada ya Shira, ingawa hivi vya sasa vyaweza kuwa na athari ndogo sana na vinavyoisha muda mfupi tu vikiwa na majivu ya udongo wa moto badala ya volcano na uji mzito wa miamba ya chuma shauri ya presha ndogo iliyopo ardhini kwa sasa.

Katika maeneo mengine Afrika Mashariki katika ukanda wa Bonde la Ufa kumewahi kuripotiwa moto wa ardhini ingawa sifikirii kama unafanana kabisa na huu wa Rombo. Huko Kenya mpaka wamefikia hatua ya kufua umeme kwa kutumia moto kama huu (Geothermal energy). Katika maeneo mengine duniani mfano katika msitu wa Amazon nimewahi kusoma kuna eneo fulani pana mto wa maji moto yanayochemka, nadhani pengine inaweza kuwa ni kitu kama hikihiki kilichotokea Rombo.


MATETEMEKO YA ARDHI


Bado Rombo na maeneo mengine kando kando ya Kilimanjaro kuna nyakati hutokea matetemeko ya ardhi, ishara nyingine kwamba shughuli za kivolcano chini ya eneo zima na ukanda wa bonde la ufa la Afrika Mashariki bado zinaendelea. Tetemeko la ardhi la mwisho lilitokea Rombo mwaka jana.

Tafiti nyingi sana zimeshafanyika na wanasayansi kuhusiana na uwezekano wa kulipuka tena kwa mlima Kilimanjaro, unaweza kutafuta “google’ na kuona ingawa karibu kila mtafiti anasema kwamba hamna uwezekano mkubwa wa mlima huo kulipuka tena hivi karibuni na hata yawezekana kilele cha Kibo kikaja kufa kabisa kama wenzake Shira na Mawenzi. Hili lakini halina uhakika kwa asilimia mia moja.

Wakaazi wa Kilimanjaro tukio kama hili la Rombo halipaswi kutupa taharuki, badala yake tutulie tukichukua tahadhari pamoja na ushauri serikali itakaoutoa baada ya Wataalamu wake kumaliza uchunguzi.

Ingawa Wataalamu wengi wameshafanya tafiti mbalimbali na kuthibitisha volcano ya mlima Kilimanjaro kutokuweza kulipuka hivi karibuni na hata hivyo kungelikuwa na viashiria vikubwa zaidi kama matetemeko na gesi nyingi kuonekana katika crater ya Kibo. Mabadiliko makubwa ya kijiolojia huchukua mamilioni ya miaka hivyo ukilinganisha na umri wa vizazi vyetu usiozidi hata miaka 100 unaweza kuona ni sawa tu na tone dogo sana la maji baharini.

Hata hivyo serikali ina wajibu wataalamu wake kuchunguza na kutoa maelezo ya uhakika zaidi kwetu wananchi ikiwa ni pamoja na tahadhari za kuchukua ikiwa kama kuna hatari zozote zile zinazoweza kuambatana na mabadiliko ya kijiolojia hata kama yatakuwa ni madogo kama haya ya Rombo ili kuepusha Wananchi kuingia taharuki au kwenye imani zingine potofu mfano za ushirikina nk.
View attachment 1960785
Makala hii imeandikwa na mtafiti wa masuala ya kijamii kwa msaada wa vyanzo mbalimbali mtandaoni.
Maelezo yameshatolewa, moto huo umetokana na MBOJI.
kuna mkusanyiko wa majani mengi yanayosombwa na maji na kujikusanya sehemu moja na kusababisha hyo hali.
Moto haukuanzia kwenye miamba.
 
Kwa wakaazi wa Wilaya ya Rombo na maeneo mengine yote kuuzunguka mlima Kilimanjaro chochote kinachotokea kuhusiana na Mlima huu ni lazima kiwaguse moja kwa moja kutokana na maisha yao kutegemea miteremko yake kwa maelefu ya miaka iliyopita. Ingawa uwezekano wa Volcano ya mlima huu kulipuka wanasayansi wanasema ni mdogo sana lakini bado wanasisitiza kwamba ni jambo linaloweza siku moja kuja kutokea kutokana na sababu kwamba volcano yake imelala tu na si kama imekufa kabisa.

Mlima mrefu kuliko yote Afrika Kilimanjaro(Kibo) ni mlima uliotokea Duniani baada ya mlipuko wa Volcano chini ya ardhi yapata miaka zaidi ya 1,000,000 hivi iliyopita. Ukiwa na vilele duara 3 (cones), Shira, Kibo na Mawenzi, kila kimoja kilijitengeneza kwa wakati wake huku Shira(kilele-mama) kikiwa ndicho kilichoanza kutokea yapata miaka zaidi ya mlioni 2.5 iliyopita kisha kikaja kuzimika kabisa (kufa) na kuzuka Mawenzi na Kibo vilivyoanza wakati mmoja miaka 1,000,000 iliyopita.

Kufikia miaka 450,000 iliyopita kilele cha Mawenzi kilisimama kabisa kurusha volcano na kuwa volcano mfu pia(iliyokufa) huku Kibo kikiendelea kurusha volcano yake mpaka ilipofika miaka 150,000 hadi 200,000 iliyopita ambapo nacho kilisimama lakini kwa muda tu siyo kufa kabisa kama wenzake Mawenzi na Shira. Hii inamaanisha kwamba kuna uwezekano siku yeyote ile Kibo kikaja kuanza tena kulipuka na kurusha volcano na majivu ya moto.

Kwa mujibu wa Wataalamu wa mambo ya miamba(geologists) Mlima Kilimanajaro na milima mingine ya kivolcano iliyopo Africa Mashariki kama mlima Kenya, mlima Meru, Mlima Elgon, Ol Doinyo Lengai, Dalafilla, longonot, mlima Nyiragongo pamoja na Maziwa mbalimbali kama vile ziwa Victoria, Nyasa, Tanganyika, Turkana nk. ingawa si vyote vipo ndani ya bomde la ufa lakini vyote ni matokeo ya shughuli za kivolcano zilizosababishwa na mpasuko wa umbo la nje la ardhi ya dunia ( tectonic plates) ambazo kila moja hujivuta kutoka kwa mwenzake na kusababisha Bonde kubwa la ufa kutokea katikati.

Mpasuko huo umesababisha baadhi ya maeneo kuwa dhaifu hivyo kusababisha eneo la ndani kabisa la Dunia ambalo kimsingi huwa na joto kali sana kupitisha uji-uji wenye mchanganyiko wa madini mbalimbali na miamba nje ya uso wa dunia(volcano). Uji huu ndio husababisha milima kama Kilimanjaro kutokea taratibu baada ya maelfu ya miaka kupita ukitiririka. Bonde la ufa limeanzia huko Ethiopia mpaka Msumbiji likipitia nchi za Somalia, Kenya, Uganda, Burundi, rwanda, Malawi na Zambia.

Katika eneo ulipozuka mlima Kilimanjaro na kwa kuwa bado shughuli za kivolcano bado zinaendelea chini ya ardhi hasa ukanda mzima wa Bonde la Ufa la Afrika Mashariki basi kuibuka kwa hali kama tunayoishuhudia Rombo yawezekana isiwe ni jambo la ajabu sana. Eneo tukio la Rombo lilipotokea si mbali na ulipo Mlima Kilimanjaro.


VIASHIRIA VINGINE.

ZIWA CHALA

Ziwa chala ni moja kati ya “vijitoto” vilivyotokana na volcano iliyounda mlima Kilimanjaro, ni ziwa lililopo Wilayani Rombo na linakadiriwa kutokea muda sawa na kilele cha Kibo miaka takriban 200,000 ilyopita. Utafiti uliofanyika kwenye ziwa hilo kwa kuchunguza matabaka ya mlundikano wa majivu ya volcano (tephra layers) ndio uliothibitisha muda halisi wa kutokea kwa mlipuko wa mwisho kiasi cha mikaka 150,000 hadi 200,000 tofauti na jinsi ilivyodhaniwa kabla kwamba ni mamilioni ya mika mingi iliyopita. Hivyo unaweza kuona miaka 200 elfu si mingi sana katika umri wa kijiolojia.

Mpaka sasa hivi hata watu wanaopanda mpaka kufika kilele cha Uhuru wanaweza kuhisi harufu ya gesi za salphur kutokea katika Crater ya mlima Kilimanjaro pale juu kabisa, ishara kwamba bado kuna shughuli za kivolkano bado zinaendelea chini ya mlima huu lakini kwa kiwango cha chini (under low pressure) kiasi majivu na uji wa miamba haviwezi kuruka umbali mrefu

Binafsi mimi (Haya ni maoni yangu lakini) nimefikiria moto wa Rombo labda inawezekana ikawa ni moja kati ya viotea vya mlima Kilimanjaro (monogenetic parasitic eruption associated with Mt Kilimanjaro) mfano wa ziwa chala na vilele vingine mfano kama ilivyotokea mawenzi na Kibo baada ya Shira, ingawa hivi vya sasa vyaweza kuwa na athari ndogo sana na vinavyoisha muda mfupi tu vikiwa na majivu ya udongo wa moto badala ya volcano na uji mzito wa miamba ya chuma shauri ya presha ndogo iliyopo ardhini kwa sasa.

Katika maeneo mengine Afrika Mashariki katika ukanda wa Bonde la Ufa kumewahi kuripotiwa moto wa ardhini ingawa sifikirii kama unafanana kabisa na huu wa Rombo. Huko Kenya mpaka wamefikia hatua ya kufua umeme kwa kutumia moto kama huu (Geothermal energy). Katika maeneo mengine duniani mfano katika msitu wa Amazon nimewahi kusoma kuna eneo fulani pana mto wa maji moto yanayochemka, nadhani pengine inaweza kuwa ni kitu kama hikihiki kilichotokea Rombo.


MATETEMEKO YA ARDHI


Bado Rombo na maeneo mengine kando kando ya Kilimanjaro kuna nyakati hutokea matetemeko ya ardhi, ishara nyingine kwamba shughuli za kivolcano chini ya eneo zima na ukanda wa bonde la ufa la Afrika Mashariki bado zinaendelea. Tetemeko la ardhi la mwisho lilitokea Rombo mwaka jana.

Tafiti nyingi sana zimeshafanyika na wanasayansi kuhusiana na uwezekano wa kulipuka tena kwa mlima Kilimanjaro, unaweza kutafuta “google’ na kuona ingawa karibu kila mtafiti anasema kwamba hamna uwezekano mkubwa wa mlima huo kulipuka tena hivi karibuni na hata yawezekana kilele cha Kibo kikaja kufa kabisa kama wenzake Shira na Mawenzi. Hili lakini halina uhakika kwa asilimia mia moja.

Wakaazi wa Kilimanjaro tukio kama hili la Rombo halipaswi kutupa taharuki, badala yake tutulie tukichukua tahadhari pamoja na ushauri serikali itakaoutoa baada ya Wataalamu wake kumaliza uchunguzi.

Ingawa Wataalamu wengi wameshafanya tafiti mbalimbali na kuthibitisha volcano ya mlima Kilimanjaro kutokuweza kulipuka hivi karibuni na hata hivyo kungelikuwa na viashiria vikubwa zaidi kama matetemeko na gesi nyingi kuonekana katika crater ya Kibo. Mabadiliko makubwa ya kijiolojia huchukua mamilioni ya miaka hivyo ukilinganisha na umri wa vizazi vyetu usiozidi hata miaka 100 unaweza kuona ni sawa tu na tone dogo sana la maji baharini.

Hata hivyo serikali ina wajibu wataalamu wake kuchunguza na kutoa maelezo ya uhakika zaidi kwetu wananchi ikiwa ni pamoja na tahadhari za kuchukua ikiwa kama kuna hatari zozote zile zinazoweza kuambatana na mabadiliko ya kijiolojia hata kama yatakuwa ni madogo kama haya ya Rombo ili kuepusha Wananchi kuingia taharuki au kwenye imani zingine potofu mfano za ushirikina nk.
View attachment 1960785
Makala hii imeandikwa na mtafiti wa masuala ya kijamii kwa msaada wa vyanzo mbalimbali mtandaoni.
Moto wa Rombo bahati nzuri ulikuwa moto wa kawaida uliotokana na shughuri za binaadamu, kwenye eneo husika kulikuwa na taka za mimea zilizofukiwa kwenye shimo na moto ulipozifikia uliingia chini na kuendelea kama ufanyavyo kwenye tanuru la mkaa. Wataalamu walichimba na kuyatoa mabaki hayo na ndiyo ukawa mwisho wa moto huo na jarada kufungwa pia kuwezesha wanarombo kuendelea kunywa pombe zao bila hofu, ila bado ninamkumbuka mrombo mmoja aliyesikika akisema "hata ukiweka nyama inaiva".
 
Ni jambo la kheri mkuu ikiwa mboji itakuwa ndiyo chanzo cha huu moto na wala si volcano kama nilivyohisi maanake kwa vyovyote vile ikiwa ni mboji itazimika tu pindi mvua zikinyesha au mbolea ikiteketea yote kwa moto. Lakini niulize wadau wengine hali kama hiyo ya mboji kuwaka imewahi kutokea mahali pengine hata nje ya Tanzania na mifano ikarekodiwa? basi mwenye taarifa japo atujuze tupate kujua zaidi tafadhali.
Sehemu zenye jua kali mawe na mbuga kavu moto huweza kuwaka wakati wowote. Mioto tuionayo maporini mingine ilianza yenyewe kutokana na joto la jua.
 
Ahsante kwa taarifa na maarifa...

Nawaza, mlima Kilimanjaro Volcano ikianza kulipukoa tena sii itatuharibia barafu kwa kuiyeyusha yote, alafu mlima unabaki kipara...
 
Back
Top Bottom