Je, mkopeshaji anaweza kukamata mali ambayo mkopaji ameweika kama dhamana ya mkopo pasipo kupata idhini ya Mahakama?

Hii ya kukopesha fedha, ukisoma hukumu ya Mahakama ya Rufaa haijaruhusu perse kuwa hata watu wasiosajiliwa wanaruhusiwa kukopesha kibiashara, kilichoelezwa ni kuwa nia ya mkopo inazingatiwa kama mkopo wenyewe haujakaa kibiashara.

Mfano, Katika kesi hiyo unayoizungumza, mkopaji alikopa Tshs. 2,600,000/= na kuahidi kuzirudisha kama zilivyo baada ya muda fulani, isipokuwa akishindwa kurudisha baada ya muda huo itampasa kurudisha na riba ya asilimia 30 kwa kila mwezi. Kwa hiyo hakukuwa na nia ya kibiashara tofauti na mkopo ungekuwa ni Tshs. 2,600,000/= inayotakiwa kulipwa baada ya miezi 3 ikiwa na riba ya asilimia 30. Hapo lazima leseni ya biashara ingehitajika.
Asante kwa nyongeza mkuu, lakini tukumbuke kesi nyingi za madai ya aina hii ya 'kukopeshana mtaani' zikienda mahakama za mwanzo ambako wakopeshaji wengi hukimbilia mahakimi wengi wamekua wakijikita zaidi katika hii hii sanctity of contract na pale inapoonekana kama riba ilikua unfair basi hu'disregard hiyo na huamua kiwa mkopaji arejeshe kile kiasi pekee alichopokea.
Lakini pamoja na hilo tunaona kuwa watu wanaendelea kudhurumiana kutokana na hizi precedents mbili japo ninaona zinawapa nafuu wakopeshaji wa mtaani kutoka kupoteza fedha zao kwa wakopaji wasio waaminifu.

Halafu pia kama hutajali naomba uweze kuishare hapa hiyo case maana najaribu kuperuze lakini siioni.
 
Niwie radhi mkuu, nilikua namaanisha kuwa kwa sasa mahakama ya juu ilikuja na uamuzi uliokua tofauti kidogo kuhusiana na suala hili la hawa wakopeshaji wa mtaani.

Mwanzoni ilikua kila madai ya hawa wakopeshaji wa mtaani wanaoweka na riba juu yakifika mahakamani basi mahakama ilikua ikijikita katika sheria zilizopo ambazo zilikua zinaelekeza kuwa mwenye mmlaka ya kukopesha tena na riba juu ya huo mkopo ni taasisi za kifedha zilizosaajiliwa na kupewa leseni ya kufanya shughuli hiyo. Sasa wale wakopeshaji wa mtaani walikua wanakosa sifa hii hivyo walikua wanashindwa sana hizi case maana ile shughuli ilikua ni haramu hivyo walipoteza kila kitu kuanzia hela waliyokopesha hadi riba (faida) waliyoitarajia.

Sasa ndio mahakama ya juu imekuja na uamuzi hivi karibuni na kueleza kuwa ikitokea suala kama hilo basi tutaangalia lengo na nia ya awali kabisa ya mkopaji na mkopeshaji na kama tutaona kua hakukua na shuruti ya aina yoyote wakati wa kuingia mkataba huo, basi mkopaji atatapika hizo hela alizokopa na akashindwa kulipa tofauti na ilivyokua hapo mwanzo.
maelezo naona ni mazuri lakini yanawasaidia nyinyi tu wasomi maana mnaongea lugha zenu za kisheria badala kunyumbulisha na si std7 tukaelewa!!!! elezeni kwa lugha rahisi tuelewe wote
 
Asante kwa nyongeza mkuu, lakini tukumbuke kesi nyingi za madai ya aina hii ya 'kukopeshana mtaani' zikienda mahakama za mwanzo ambako wakopeshaji wengi hukimbilia mahakimi wengi wamekua wakijikita zaidi katika hii hii sanctity of contract na pale inapoonekana kama riba ilikua unfair basi hu'disregard hiyo na huamua kiwa mkopaji arejeshe kile kiasi pekee alichopokea.
Lakini pamoja na hilo tunaona kuwa watu wanaendelea kudhurumiana kutokana na hizi precedents mbili japo ninaona zinawapa nafuu wakopeshaji wa mtaani kutoka kupoteza fedha zao kwa wakopaji wasio waaminifu.

Halafu pia kama hutajali naomba uweze kuishare hapa hiyo case maana najaribu kuperuze lakini siioni.
Ukiisoma hii kesi, ili mkopeshaji asidhulumike inabidi awe makini kwenye mkataba wa ukopeshaji. Aoneshe kuwa mkopo unatoka na kurudi kama ulivyotoka bila riba, kama anakusudia kuwekwa riba iwekwe humohumo ndani kwa ndani, yaani isomeke kama principal tu. Mahakama haijahalalisha biashara za kukopeshana kibiashara bila kusajiliwa.
 

Attachments

  • simon-kichele-chacha-vs-aveline-m-kilawe-civit-appeal-no-i5o-2018.pdf
    192.4 KB · Views: 16
Asante sana mkuu kwa hii nakala. Pamoja na mengine, hii imekuja kuokoa wakopeshaji wa mtaani. Maana wakati watu wakiwa na shida huwafuata na hukubaliana na mashart yao pasipo shuruti lakini wakiisha kutatua sida zao halafu wakishindwa kulipa ndio huibuka jina la 'mikopo umiza' unaweza kudhani walishikiwa bunduki.
Ukiisoma hii kesi, ili mkopeshaji asidhulumike inabidi awe makini kwenye mkataba wa ukopeshaji. Aoneshe kuwa mkopo unatoka na kurudi kama ulivyotoka bila riba, kama anakusudia kuwekwa riba iwekwe humohumo ndani kwa ndani, yaani isomeke kama principal tu. Mahakama haijahalalisha biashara za kukopeshana kibiashara bila kusajiliwa.
 
Back
Top Bottom