Je, Miradi mkakati inayotekelezwa awamu ya tano ina tija kwa Mtanzania wa kawaida?

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,087
6,568
Ni swali ambalo mtu kwa haraka unaweza kudhania ni swali ambalo halina logic. Lakini kiuhalisia hili ni swali la msingi ambalo wachumi wanaoishauri serikali walipaswa kujiuliza kabla ya kushauri serikali kutekeleza miradi inayoigharimu serikali yetu matrilioni ya Tsh.

Mradi wa JNHP utakuwa na tija kwa mtanzania ambae mpaka sasa ni mtu anayeishi maisha duni? Mtu ambae anaishi kwa kusaka chakula tu.

Je Sgr itakuwa na manufaa ya kumletea ahueni mtu ambae anaishi kwenye lindi la umaskini? Hana pa kulala pazuri,hana elimu ya kutosha na anakaa kijijini au mjini kwenye slums?

Daraja la Busisi je litawasaidia nini wananchi wa Tanzania? Ambao hata ada za shule, gharama za hospital na malazi ni tabu kuzipata!

Kama nchi ambayo ni masikini, tulihitaji treni ya umeme kwa sasa? Tulihitaji mradi kama JNHP wakati mahitaji yetu kama nchu hayazidi Mw 1000? Je tulihitaji kujenga madaraja makubwa kama Busisi na Oysterbay?

Mtazamo wangu, sisi ni nchi maskini, tulihitaji kuboresha sekta ya afya, elimu na miundombinu sio kwa kiasi kikubwa cha pesa namna hii. Mfano tulitakiwa kujenga SGR kama ya Jirani zetu Kenya ambayo haina gharama kubwa, hakukuwa na umuhimu wa madaraja kama Busisi na Oysterbay. Bora tungeboresha elimu na afya kwa kuzifanya ziwe bure.

Nawakilisha.
 
Kuliko kununua ndege bora tungenunua matrekta, kila kijiji kiwe na matraktor kama mawili, na kuweka ruzuku kwenye mbolea, kisha kuwekeza nguvu katika mazao ya kimkakati kama korosho, pamba, parachichi, tumbaku na kahawa. Ndani ya hii miaka mitano tungekuwa na matokeo ya dhahiri badala ya ndege zilizopark.
 
Maji ya bomba au maji tiririka ni tatizo sugu. Maji ni bidhaa inayohitajika kwa matumizi ya binadamu kuliko vocha ya simu. Kama makampuni ya simu yanatengeneza faida maji yangeweza kutengeneza faida mara dufu.

Kama miradi mikubwa ya maji ingepewa kipaumbele hata kwa mikopo. Kupump maji kwa wingi, kutengeneza reservoirs za kukusanya maji ya mito na ya mvua.

Zabuni zitolewe kwa wenye shahada za Civil Engineering kutandaza mabomba. Matangazo yawekwe kila mahali tunakuketea maji mpaka nyumbani kwako.

Ndani ya mwaka mmoja tu makusanyo ya mapato ya maji yataonekana. Asiye lipa bill anakatiwa maji.
 
Kuliko kununua ndege bora tungenunua matrekta, kila kijiji kiwe na matraktor kama mawili, na kuweka ruzuku kwenye mbolea, kisha kuwekeza nguvu katika mazao ya kimkakati kama korosho, pamba, parachichi, tumbaku na kahawa. Ndani ya hii miaka mitano tungekuwa na matokeo ya dhahiri badala ya ndege zilizopark.
Ndege zimepark dunia nzima, matrekta yangesaidia kuachana na umaskini?
 
Ndege zimepark dunia nzima, matrekta yangesaidia kuachana na umaskini?

Hata kama zingekuwa huko dunia nzima hazijapark, za kwetu zilikuwa haziendeshwi kwa faida kutokana na uwezo mdogo wa ushindani kwa shirika letu lisilofahamika.

Kuondoa umasikini ingekuwa ni hatua itakayofuata baada ya watu kupata ajira kutokana na hayo matraktor. Ifahamike wananchi wengi wangelima kwa tractor na kwa gharama nafuu, hivyo kupandisha ubora na wingi wa mazao yao. Kwa vyovyote vile uchumi wa hao watu ungeinuka na hatimaye taifa kwa ujumla. Hili nililisema toka mwanzo kabla ndege ya kwanza haijanunuliwa, na nitaendelea kushikilia jambo hili kwani nina uhakika na nikisemacho.

Nasisitiza, uwekezaji wa pesa ya wananchi kwenye ndege, ni moja ya maamuzi mabovu kabisa ya awamu hii. Pesa hizo zingewekezwa kwenye sekta ya kilimo zingekuwa na tija kuliko ndege. Hata kama kusingekuwa na tija sana kuwekeza kwenye kilimo, bado kwenye kilimo kungekuwa na tija zaidi kuliko kuwekeza kwenye hizo ndege.
 
Mkuu hapana
Sikuungi Mkono either emeeleza tuu bila kujua
Kwa undani!

Hayo Uliyoyataja Elimu,Afya,Kilimo binafsi nimeyachoka Kusikia wimbo huo kila siku Tangu enzi za Nyerere...Yaani Ni Business as usual!
Bora ufanye kitu kimona Kikubwa kionekane...
Kama ni Stieglier tuu...

Then itupatie hela/Iingize hela halafu hela hiyo ikafanye hayo Elimu,Afya,Kilimo,
Sababu wether ujenge reli, Stieglier hayo yapo tuu Kila zmwaka na Hata uyafanyie vipi hayana retun financial returns ya Haraka,Unakuwa mmefanana tuu na Kiongozi aliepita Kuwa Wote mmeshiriki ktk Afya, Elimu nk!
Nothing new, Nothing tangible!

Eti Kila siku watoto unawanunulia nguo, Tuisheni, Chakula,
Wakati wapo nyumba ya Kupanga hahhaa

Jenga nyumba kwa ukumbusho wakae kwenye nyumba yao watakukumbuka baadae...
Chakula watakula tuu, Watavaa tuu chochote.

Cha Msingi ni Kuwa na Mradi Mmoja wa Kimkakati kama Stieglier tuuu ili Kuokoa hela,
Ukimalizika ndo Unahamia mradi mwingine say Reli!

Au Kama Una Kifua fanya Isizidi miwili tuu baasi!
Lakini Stiglier, Busisi, Salender, Reli, Barabara, Makai makuu dom, Umeme, Vimiradi vingiiiiiiii duuu!
 
Sikuungi Mkono either emeeleza tuu bila kujua
Kwa undani!
Hayo Uliyoyataja Elimu,Afya,Kilimo binafsi nimeyachoka Kusikia wimbo huo kila siku Tangu enzi za Nyerere...Yaani Ni Business as usual!
Bora ufanye kitu kimona Kikubwa kionekane...
Kama ni Stieglier tuu...
Then itupatie hela/Iingize hela halafu hela hiyo ikafanye hayo Elimu,Afya,Kilimo,
Sababu wether ujenge reli,Stieglier hayo yapo tuu Kila zmwaka na Hata uyafanyie vipi hayana retun financial returns ya Haraka,Unakuwa mmefanana tuu na Kiongozi aliepita Kuwa Wote mmeshiriki ktk Afya,Elimu nk!
Nothing new,Nothing tangible!
Eti Kila siku watoto unawanunulia nguo,Tuisheni,Chakula,
Wakati wapo nyumba ya Kupanga hahhaa
Jenga nyumba kwa ukumbusho wakae kwenye nyumba yao watakukumbuka baadae...
Chakula watakula tuu,Watavaa tuu chochote.
Cha Msingi ni Kuwa na Mradi Mmoja wa Kimkakati kama Stieglier tuuu ili Kuokoa hela,
Ukimalizika ndo Unahamia mradi mwingine say Reli!
Au Kama Una Kifua fanya Isizidi miwili tuu baasi!
Lakini stiglier,busisi,Salender,Reli,Barabara,Makai makuu dom,Umeme,Vimiradi vingiiiiiiii duuu!
Ukweli ni kuwa masuala ya afya,elimu na miundo mbinu tuko nyuma sana. Jiulize tu hii miradi mikubwa ilitakiwa ifanyike wakati hata huduma za msingi kama maji, elimu na afya bado ni duni?

Je kwa nini tusijenge JHNP,reli ya Sgr ambayo sio ya gharama ya juu kama Kenya.

Madaraja mawili ya Busisi na Oysterbay yana umuhimu?
 
Umenikumbusha miaka kama 5 huko kijijini kwetu, kulikuwa na mjadala kuhusu michango ya kuzika kijijini kwetu. Ilipitishwa azimio kuwa kila mzaliwa wa kijiji chetu lazima ashiriki katika kuchimba kaburi na kama hutashiriki basi faini iwe 5,000.

Wengi wa wasioishi kijini walijitetea na kuomba kusamehewa maana si wakazi wa kijiji chetu ingawa ni wazawa. Ikatolewa hoja kuwa kama mwanakijiji akipata mauti Mjini na akalazimika kusafirishwa au kuzikwa kule, je, wanakijiji wote watachanga na kuzituma mjini? Wote wanakijiji wanaoishi kijijini WALIKATAA katu katu na kudai kuwa nani aliwapeleka mjini. Kama ni hivyo warudi.

Nakumbuka mama mmoja alikuwa mbogo na kueleza kuwa yeye hana mtoto Dar es Salaam; hivyo walio Dar lazima wawe wanatuma hela. Kwa bahati mbaya mama huyo bada ya muda aliugua akapata rufaa ya kwenda hospitali ya wilaya, baadaye ya mkoa, baadaye ya kanda na mwisho Ocean Road Dar. Kufupisha alifariki akiwa Ocean Road na ikabidi tuupeleke mwili kijijini kwa gharama za wale ambao hawakutumwa na mtu kwenda kuishi Dar.

Mkuu sana Nyankurungu2020 usiwe kama wanakijiji wa kwetu kwa kuwa wewe ni mpinzani wa JPM
 
Hata kama zingekuwa huko dunia nzima hazijapark, za kwetu zilikuwa haziendeshwi kwa faida kutokana na uwezo mdogo wa ushindani kwa shirika letu lisilofahamika.

Kuondoa umasikini ingekuwa ni hatua itakayofuata baada ya watu kupata ajira kutokana na hayo matraktor. Ifahamike wananchi wengi wangelima kwa tractor na kwa gharama nafuu, hivyo kupandisha ubora na wingi wa mazao yao. Kwa vyovyote vile uchumi wa hao watu ungeinuka na hatimaye taifa kwa ujumla. Hili nililisema toka mwanzo kabla ndege ya kwanza haijanunuliwa, na nitaendelea kushikilia jambo hili kwani nini uhakika na nikisemacho.

Nasisitiza, uwekezaji wa pesa ya wananchi ni moja ya maamuzi mabovu kabisa ya awamu hii. Pesa hizo zingewekezwa kwenye sekta ya kilimo zingekuwa na tija kuliko ndege. Hata kama kusingekuwa na tija sana kuwekeza kwenye kilimo, bado kwenye kilimo kungekuwa na tija zaidi kuliko kuwekeza kwenye hizo ndege.
Ndugu kwani ukianzisha shirika la ndege unapata faida kwa muda mfupi?

Anyway kuhusu maamuzi mabovu unaweza kuwa sahihi. Maana hata Daraja la Oysterbay/ salender halina umuhimu tena maana lilikuwa kwa ajiri ya viongozi wakuu kukwepa foleni,sasa wamehia Dodoma.
 
Ukweli ni kuwa masuala ya afya,elimu na miundo mbinu tuko nyuma sana. Jiulize tu hii miradi mikubwa ilitakiwa ifanyike wakati hata huduma za msingi kama maji, elimu na afya bado ni duni?

Je kwa nini tusijenge JHNP,reli ya Sgr ambayo sio ya gharama ya juu kama Kenya.

Madaraja mawili ya Busisi na Oysterbay yana umuhimu?
Kwa huu mstari ulouandika, kichwa chako kinatakiwa kuangaliwa kwa umakini
 
Umenikumbusha miaka kama 5 huko kijijini kwetu, kulikuwa na mjadala kuhusu michango ya kuzika kijijini kwetu. Ilipitishwa azimio kuwa kila mzaliwa wa kijiji chetu lazima ashiriki katika kuchimba kaburi na kama hutashiriki basi faini iwe 5,000.

Wengi wa wasioishi kijini walijitetea na kuomba kusamehewa maana si wakazi wa kijiji chetu ingawa ni wazawa. Ikatolewa hoja kuwa kama mwanakijiji akipata mauti Mjini na akalazimika kusafirishwa au kuzikwa kule, je, wanakijiji wote watachanga na kuzituma mjini? Wote wanakijiji wanaoishi kijijini WALIKATAA katu katu na kudai kuwa nani aliwapeleka mjini. Kama ni hivyo warudi.

Nakumbuka mama mmoja alikuwa mbogo na kueleza kuwa yeye hana mtoto Dar es Salaam; hivyo walio Dar lazima wawe wanatuma hela. Kwa bahati mbaya mama huyo bada ya muda aliugua akapata rufaa ya kwenda hospitali ya wilaya, baadaye ya mkoa, baadaye ya kanda na mwisho Ocean Road Dar. Kufupisha alifariki akiwa Ocean Road na ikabidi tuupeleke mwili kijijini kwa gharama za wale ambao hawakutumwa na mtu kwenda kuishi Dar.

Mkuu sana Nyankurungu2020 usiwe kama wanakijiji wa kwetu kwa kuwa wewe ni mpinzani wa JPM
Kwa ufupi sijakuelewa,hoja ya msingi hapa ni kuwa na miradi mkakati ambayo ina manufaa kwa kila mtanzania.

Mfano kila mtu anajua tunahitaji reli ya kisasa ambayo ni Sgr,lakini Tanzania hii ambayo watanzania 80% ni waganga njaa,tunahitaji reli ya umeme kama nchi za ulaya?

Tunatakiwa kufanya maendeleo yanayomgusa kila mtu. Daraja la bil 700 litamsaidia vipi mwananchi wa Sengerma vijijini ambae hana maji?
 
Ndugu kwani ukianzisha shirika la ndege unapata faida kwa muda mfupi?

Anyway kuhusu maamuzi mabovu unaweza kuwa sahihi. Maana hata Daraja la Oysterbay/ salender halina umuhimu tena maana lilikuwa kwa ajiri ya viongozi wakuu kukwepa foleni,sasa wamehia Dodoma.

Kutokana na changamoto za ushindani wa Biashara ya ndege duniani, hizo ndege zetu hata zikae miaka 20 sioni zikileta faida.

Kwa taarifa yako, Magufuli ndio kahamia Dodoma, akitoka tu madarakani viongozi wote wanarudi Dar. Angalia hata kwa sasa serekali inafanyia kazi barabarani kati ya Dodoma na Dar. Viongozi wote wako Dar na kwenda kufanya kazi Dodoma kwa shingo upande. Hivyo hilo daraja lao bado watalitumia tu kuanzia 2026, iwapo Magu atakubali kwa shingo upande kutoka madarakani.
 
Kwa ufupi sijakuelewa,hoja ya msingi hapa ni kuwa na miradi mkakati ambayo ina manufaa kwa kila mtanzania.

Mfano kila mtu anajua tunahitaji reli ya kisasa ambayo ni Sgr,lakini Tanzania hii ambayo watanzania 80% ni waganga njaa,tunahitaji reli ya umeme kama nchi za ulaya?

Tunatakiwa kufanya maendeleo yanayomgusa kila mtu. Daraja la bil 700 litamsaidia vipi mwananchi wa Sengerma vijijini ambae hana maji?
Huwezi kunielewa kwa vile upo naive na sijui elimu yako. Aidha wewe ni mbinafsi kama Tundu Lissu. Kama huwezi kuona umuhimu wa daraja la Busisi kwa watanzania wote, nikupe pole ya mwaka mpaya
 
Kutokana na changamoto za ushindani wa Biashara ya ndege duniani, hizo ndege zetu hata zikae miaka 20 sioni zikileta faida.

Kwa taarifa yako, Magufuli ndio kahamia Dodoma, akitoka tu madarakani viongozi wote wanarudi Dar. Angalia hata kwa sasa serekali inafanyia kazi barabarani kati ya Dodoma na Dar. Viongozi wote wako Dar na kwenda kufanya kazi Dodoma kwa shingo upande. Hivyo hilo daraja lao bado watalitumia tu kuanzia 2026, iwapo Magu atakubali kwa shingo upande kutoka madarakani.
Hilo la ndege kutopata faida una uhakika gani?

Hilo la serikali kurudi dar unao uhakika gani?
 
Huwezi kunielewa kwa vile upo naive na sijui elimu yako. Aidha wewe ni mbinafsi kama Tundu Lissu. Kama huwezi kuona umuhimu wa daraja la Busisi kwa watanzania wote, nikupe pole ya mwaka mpaya
Nafikiri suala la elimu halihusiki hapa.

Wewe unajua umuhimu wake tuambie. Maana kama ninfoleni bora kuwa na kivuko kikubwa cha magari cha bil 50. Lakini pesa nyingime ikatumika kusambaza maji,kuboresha elimu na afya kwa sasa. Bil 700 ni pesa nyingi sana wakati hata Sengerema shida ya maji ni kubwa

Hii inaonyesha mipango ya kutatua kero za wananchi ni duni sana.
 
Back
Top Bottom