The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Amani iwe juu yenu wanajamvi wenzangu?
Kwa miaka kibao sasa makampuni ya simu za mkononi hapa nchini (pengine hata nje ya nchi) yamekuwa yaki-promote biashara zao kwa michezo mbalimbali ya kubahatisha. Makampuni haya yamewahi kutoa fedha nyingi tu, magari mengi tu, muda wa maongezi na kadhalika. Mengi ya matukio makubwa ya utoaji wa zawadi yamekuwa yakioneshwa kupitia runinga.
Swali ambalo baadhi ya jamaa zangu wamekuwa wakiuliza na mwishowe hata mimi binafsi kuanza kujiuliza ni je Michezo hii huwa ni ya kweli? Je inafuata taratibu zote za haki kwa washiriki wote au kuna ujanja ujanja?
Najua michezo hii inaratibiwa na taasisi ya kiserikali (Bodi ya Michezo ya Bahati Nasibu au kitu kama hicho) lakini Tz kwa rushwa tunatisha sasa, hapa pia napata swali; Je Kama Makampuni haya yatafanya janja ili kutoa zawadi kwa upendeleo (kwa watu maalum waliopangwa) au kiusanii (mfano show tupu mbele ya kamera halafu zawadi halisi ziro) msimamizi atasema nini akipewa chake? Na je wenye swali hili hapo juu watajuaje kama ni viini macho?
Samahani kwa nitakaowakera, lengo langu ni kupata maoni yenu tu.
Kuna watu wanaotumia fedha nyingi kujaribu kupata bahati na zawadi hizo. Ni imani yangu basi watu hawa wanastahili kuendeshewa mchezo au bahati nasibu hizo kwa haki na kutodanganywa hata kama hawataibuka washindi.
Tafadhali naomba kuwasilisha.
Kwa miaka kibao sasa makampuni ya simu za mkononi hapa nchini (pengine hata nje ya nchi) yamekuwa yaki-promote biashara zao kwa michezo mbalimbali ya kubahatisha. Makampuni haya yamewahi kutoa fedha nyingi tu, magari mengi tu, muda wa maongezi na kadhalika. Mengi ya matukio makubwa ya utoaji wa zawadi yamekuwa yakioneshwa kupitia runinga.
Swali ambalo baadhi ya jamaa zangu wamekuwa wakiuliza na mwishowe hata mimi binafsi kuanza kujiuliza ni je Michezo hii huwa ni ya kweli? Je inafuata taratibu zote za haki kwa washiriki wote au kuna ujanja ujanja?
Najua michezo hii inaratibiwa na taasisi ya kiserikali (Bodi ya Michezo ya Bahati Nasibu au kitu kama hicho) lakini Tz kwa rushwa tunatisha sasa, hapa pia napata swali; Je Kama Makampuni haya yatafanya janja ili kutoa zawadi kwa upendeleo (kwa watu maalum waliopangwa) au kiusanii (mfano show tupu mbele ya kamera halafu zawadi halisi ziro) msimamizi atasema nini akipewa chake? Na je wenye swali hili hapo juu watajuaje kama ni viini macho?
Samahani kwa nitakaowakera, lengo langu ni kupata maoni yenu tu.
Kuna watu wanaotumia fedha nyingi kujaribu kupata bahati na zawadi hizo. Ni imani yangu basi watu hawa wanastahili kuendeshewa mchezo au bahati nasibu hizo kwa haki na kutodanganywa hata kama hawataibuka washindi.
Tafadhali naomba kuwasilisha.