Je, mchanganyiko wa Dawa za Kienyeji na za hospitalini zinaweza kutibu Ugonjwa wa akili?

Rebeca 83

JF-Expert Member
Jun 4, 2016
14,840
31,583
Hello JF,

Ningependa kujua kama ushawahi kupata tiba, kati ya hizo mbili (Tradition Medicine au Modern Medicine)

Ipi ili work?

Au zote?

Kipi kilichokusukuma utumie kimoja wapo?

Nini kilikusukuma utumie vyote?

Unatushaurije?

----------
Maoni ya Mdau
Matumizi ya dawa za asili sambamba na zile za hospitalini na pia kuzichanganya kunaweza kusababisha matokeo hasi kwa mtumiaji hususani pale zinapotumika kutibu ugonjwa wa aina moja.

Dawa ni kemikali na kuna vitu vinavyohitajika kuzingatiwa ili ziweze kufanya kazi yake, na zinaweza kushindwa kufanya kazi yake vizuri pale ambapo zinapokutana na kemikali zingine kwa maana kila dawa ina namna yake ya utendaji kazi.

Mfano, baadhi ya dawa hususani za hospitalini hufanya kazi mwilini kwa kuzuia uzalishaji wa baadhi ya vitu ndani ya mwili ili kuweza kutengeneza mazingira ya kuudhoofisha ugonjwa na ikitokea ingizo la kemikali nyingine itakayofanya kinyume chake ndipo dawa ile hushindwa kufanya kazi vizuri.

Ndiyo maana hizi dawa tena hasa za hospitalini zina kitu kinaitwa 'Side Effects' na maelekezo maalumu ya jinsi ya kuzitumia ikiwemo pia vitu vya kuepukana navyo.

Jambo la msingi ni kuyasoma kwa makini maelekezo yanayokuja na dawa husika na pia kuzingatia ushauri wa Daktari atakayekupatia dawa kwa ajili ya matibabu.
 
Matumizi ya dawa za asili sambamba na zile za hospitalini na pia kuzichanganya kunaweza kusababisha matokeo hasi kwa mtumiaji hususani pale zinapotumika kutibu ugonjwa wa aina moja.

Dawa ni kemikali na kuna vitu vinavyohitajika kuzingatiwa ili ziweze kufanya kazi yake, na zinaweza kushindwa kufanya kazi yake vizuri pale ambapo zinapokutana na kemikali zingine kwa maana kila dawa ina namna yake ya utendaji kazi.

Mfano, baadhi ya dawa hususani za hospitalini hufanya kazi mwilini kwa kuzuia uzalishaji wa baadhi ya vitu ndani ya mwili ili kuweza kutengeneza mazingira ya kuudhoofisha ugonjwa na ikitokea ingizo la kemikali nyingine itakayofanya kinyume chake ndipo dawa ile hushindwa kufanya kazi vizuri.

Ndiyo maana hizi dawa tena hasa za hospitalini zina kitu kinaitwa 'Side Effects' na maelekezo maalumu ya jinsi ya kuzitumia ikiwemo pia vitu vya kuepukana navyo.

Jambo la msingi ni kuyasoma kwa makini maelekezo yanayokuja na dawa husika na pia kuzingatia ushauri wa Daktari atakayekupatia dawa kwa ajili ya matibabu.
 
swali lako pana sana.

MI nilumwa kichwa sikuwa kichaa ila akili haikuwa sawa ilibidi nisimame kufanya kazi ya ajira

1.waganga wa kienyeji wanaopiga raml
2.waganga wa kienyeji wasiopiga ramli
3 Dawa zza kienyeji tuziuazo kwa urithi za magonjwa ya kawaida sio lazima kwenda kwa hao hapo juu
4. Hawa waliojitokeza sasa hivi wwanajitangaza mpaka kwenye media.

hao wote hapo juu nimefika kwao kasoro . Namba 4 hawashughuliki na mambo hayo ya kichwa

Nilienda huko baada ya kwenda Ocean rd na kuambiwa sina matatizo na pia kumwona dr Bingwa wa magonjwa
ya akili na kuniambia siumwi wakati mi naumwa sana tu.

Katika namba na 1 na 2 hapo juu sio kwamba hazifanyi kazi zinafanya kazi ila ni ushirikina na kuna matapeli wengi
Mi kwa upande wangu waliweza kunisaidia kupata nafuu kwa muda halafu matatizo yalikuwa yanarudia tena.

huenda wengine wanapona ndio
maana 1 na 2 wapo wengi sana hapa mjini ila wote kusema ukweli mi naona ni wachawi tu ndio maana hata utafiti ina kuwa ngumu hawako wazi katika mambo yao. Wangekuwa wazi data zote ungepata kwao

Mi nilipona ila sio kwa hospitali au kwa hao ma dokta feki.
 
Kama mtu anaugonjwa wa akili wa kuzaliwa nao means hakua na drug addiction yoyote tafuta dawa za kienyeji ndio za uhakika zaidi.

Ila dawa yenyewe iwe na sifa ifuatayo,
Mtumiaji atumie asubuhi tumbo likiwa halina kitu pia akichwa dawa hiyo lazima kuitapika ndio ugonjwa utaisha.
 
wakurochi,
Pole mkuu,kwa hio uliombewa? its hard to get data,watu wanaenda kwa waganga kimya kimya:D:D:D:oops:, I wish wangekuwa open tuone tunasaidianaje?
 
Mpeni mtoa mada mbinu aweze kwenda kutibiwa maana kadri siku zinavyokwenda hali yake inazidi kua mbaya
 
Back
Top Bottom