Je, mbinu inayotumiwa na CCM kwa kipindi hiki ya kukaa kimya itakisaidia chama hicho?

Hivyo vitu ndio vitawapigia kura.
Relax usipanic mkuu, tulia tu uandike vizuri, rudi darasani kasome katika topic ya Development kuna kitu kinaitwa "indicators of development", kama unakiri kuviona hivyo vitu basi ujue kuna shughuli kubwa za maendeleo zimefanywa....
Screenshot_20200812-091303.jpg
 
Nipende tu kuwakumbusha kauli ya Katibu mkuu CCM kwamba, watafanya kampeni kitanda kwa kitanda, na ndicho kinachoendelea, wako wanashugurika na kushawishi wanawake na wazee, walala hoi wasiokuwa na ajira na maskini kabasa...
Itakuwa hawana la kujibu pia, hivi airport ya chato utaitolea jibu gani?
 
Ilikuwa ikitumika kusaidia wananchi kwa lengo la kuinua uchumi wao lakini kwa sasa inalenga kukipa chama kura. Wameshachelewa
Yani linalokuja kuchwani ni kuandika tuu.. ukiambiwa uprove hizo accusation will buddy..... Watanzania unafiki ndio unaotumaliza
 
Hakuna aliyetegemea Lissu angekuja kama alivyo sasa. Amekuja imara zaidi ya alivyokuwa. CCM walidhani atarudi akiwa muogamuoga kumbe hapana, jamaa liko fiti sana kiakili na kimwili na watu wanamuelewa vizuri sana akiongea maana hana chembechembe za UONGO katika maelezo yake dhidi ya propaganda za CCM za miaka hii minne iliyopita
 
Kama mtu mgeni na siasa za Tz anaweza kusema huyo Lissu si mchezo kweli ndiyo anayechukua nchi,kumbe kama kawaida uchaguzi ukiisha unaona watu wanalalamika kuibiwa kura.
 
MATAGA wamepigwa bumbuwazi ndugu, wala si kukaa kimya eti kimkakati. wamechanganyikiwa kwa jinsi Lissu anavyotoa majibu ya tambo zao za miaka 5.

Lissu kawapiga bumbuwazi MATAGA kwani kwanza hawakuamini jamaa angerejea nchini na pili kwamba angeweza kutoa majibu ya tambo zao this comprehensively.

sasa MATAGA wamerudi kwenye drawing board ili kutunga kiki nyingine fake - Lissu anawasubiri, Watanzania wanasubiri kumsikiliza Lissu.

wameishia kuwaagiza kina Sirro na Kaijage kumjibu Lissu kimkwara but unapompiga mkwara Lissu ni kama kumpiga chura teke.

mimi ni CCM by the way lakini si MATAGA.

habari ndiyo hiyo!

Haaa. Watu mna mambo. Eti siyo mataga
 
CCM wanajielewa kuliko Hawa wanaosadikika Ni wapinzani.
Yani kipenga Cha Mchezo hata hakijapuulizwa Wala watu hawajaingia hata uwanjani tayari washaanza mihemuko ya Mchezo.

Na kwa Akili hizi itachukua miaka mingi Sana CCM kuitoa madarakani.
Amini usiamini mgombea urais wa muungano wa vyama vya Upinzani Ni Benard membe na Wala siyo lissu na huyo membe ni Mgombea wa kimukakati kutoka upande wa pili.
 
Nipende tu kuwakumbusha kauli ya Katibu mkuu CCM kwamba, watafanya kampeni kitanda kwa kitanda, na ndicho kinachoendelea, wako wanashugurika na kushawishi wanawake na wazee, walala hoi wasiokuwa na ajira na maskini kabisa.

Mfano, kupitia TASAF, Sasa hivi majina yameongezwa, haijalishi unakipato gani, ukiwa na umri kuanzia miaka 50 unapewa pesa kupitia TASAF, ndivyo khari ilivyo. Siyo tu hivyo, Kuna mbinu Kali zimepangwa ndani na nje ya chama Cha Mapinduzi, kupitia mgongo wa Serikali, ccm wataendelea na uzinduzi wa miladi na kujinadi kwamba wao Ni vitendo, lakini pia wamechagua kukaa kimya bila kujibu mapigo ya wapinzani, na hapo ndipo watu wengi wanamatamanio kusikia Nani atakuwa mjibu mapigo ya upinzani, ila all in all, je kampeni za kitanda kwa kitanda zitawasaidia CCM? au wanashindwa jinsi ya kumsaidia m/kiti wa ccm?

Siasa Ni sayansi, usimdhalau mpinzani wako
Wanaandaa bao la mkono.
 
Nipende tu kuwakumbusha kauli ya Katibu mkuu CCM kwamba, watafanya kampeni kitanda kwa kitanda, na ndicho kinachoendelea, wako wanashugurika na kushawishi wanawake na wazee, walala hoi wasiokuwa na ajira na maskini kabasa.

Mfano, kupitia TASAF, Sasa hivi majina yameongezwa, haijalishi unakipato gani, ukiwa na umri kuanzia miaka 50 unapewa pesa kupitia TASAF, ndivyo khari ilivyo. Siyo tu hivyo, Kuna mbinu Kali zimepangwa ndani na nje ya chama Cha Mapinduzi, kupitia mgongo wa Serikali.

CCM wataendelea na uzinduzi wa miladi na kujinadi kwamba wao Ni vitendo, lakini pia wamechagua kukaa kimya bila kujibu mapigo ya wapinzani, na hapo ndipo watu wengi wanamatamanio kusikia Nani atakuwa mjibu mapigo ya upinzani, ila all in all.

Je kampeni za kitanda kwa kitanda zitawasaidia CCM? au wanashindwa jinsi ya kumsaidia m/kiti wa ccm?

Siasa Ni sayansi, usimdhalau mpinzani wako
Sitii neno
gersonmsigwa_20200812_142947_0.jpg
 
Nipende tu kuwakumbusha kauli ya Katibu mkuu CCM kwamba, watafanya kampeni kitanda kwa kitanda, na ndicho kinachoendelea, wako wanashugurika na kushawishi wanawake na wazee, walala hoi wasiokuwa na ajira na maskini kabasa.

Mfano, kupitia TASAF, Sasa hivi majina yameongezwa, haijalishi unakipato gani, ukiwa na umri kuanzia miaka 50 unapewa pesa kupitia TASAF, ndivyo khari ilivyo. Siyo tu hivyo, Kuna mbinu Kali zimepangwa ndani na nje ya chama Cha Mapinduzi, kupitia mgongo wa Serikali.

CCM wataendelea na uzinduzi wa miladi na kujinadi kwamba wao Ni vitendo, lakini pia wamechagua kukaa kimya bila kujibu mapigo ya wapinzani, na hapo ndipo watu wengi wanamatamanio kusikia Nani atakuwa mjibu mapigo ya upinzani, ila all in all.

Je kampeni za kitanda kwa kitanda zitawasaidia CCM? au wanashindwa jinsi ya kumsaidia m/kiti wa ccm?

Siasa Ni sayansi, usimdhalau mpinzani wako
Sasa hivi ccm maji yako shingoni.
Hata majina ya wagombea ubunge na udiwani wameshindwa kutoa mapema,
wanasubiri siku 1 kabla ya dirisha la kuchukua form kufungwa ili watakaokatwa washindwe kuhamia upande wa pili.
hiyo ndio habari ya lumumba kwa sasa.
 
CCM wanacheza mchezo wao,ukiona kwa sasa wapo kimya ujue wanatengeneza containment procedures .Iwapo Lissu au Membe atakatwa na NEC.
Au labda Wako kimya wakitafakhari hoja za upinzani ,tarehe 26 wanaanza maangamizi..
 
CCM wanajielewa kuliko Hawa wanaosadikika Ni wapinzani.
Yani kipenga Cha Mchezo hata hakijapuulizwa Wala watu hawajaingia hata uwanjani tayari washaanza mihemuko ya Mchezo.

Na kwa Akili hizi itachukua miaka mingi Sana CCM kuitoa madarakani.
Amini usiamini mgombea urais wa muungano wa vyama vya Upinzani Ni Benard membe na Wala siyo lissu na huyo membe ni Mgombea wa kimukakati kutoka upande wa pili.
Umesikia wapi?Umesikia wapi kuna mgombea Uraisi wa muungano wa vyama upinzani...Lengo lenu limefeli hatumtaki Membe hata vijana wa ACT hawamtaki
 
Umesikia wapi?Umesikia wapi kuna mgombea Uraisi wa muungano wa vyama upinzani...Lengo lenu limefeli hatumtaki Membe hata vijana wa ACT hawamtaki
Mkuu Akili yako ya kisaisa Ni ndogo Huwezi nielewa kwasasa subiri Muda ukifika ndo utajua Nini namanisha.
 
Subiri kampeni zianze ndipo utakua ccm tumejipanga vipi
Ccm chama kikubwa sio kuongea hovyo na kuropoka,kwa sasa tupo bize kudurusu Sera zetu,filimbi ikianza tu tutaenda chini kabisa kueleza tumefanya Nini,na tukipewa dola tutafanya nini.nyie hangaikeni na uwanja na mbuga chato
Pale ambapo "msaidi wa kazi za nyumbani" anapovaa viatu na nguo za bosi wake na yeye kujiona kuwa ni bosi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Subiri kampeni zianze ndipo utakua ccm tumejipanga vipi
Ccm chama kikubwa sio kuongea hovyo na kuropoka,kwa sasa tupo bize kudurusu Sera zetu,filimbi ikianza tu tutaenda chini kabisa kueleza tumefanya Nini,na tukipewa dola tutafanya nini.nyie hangaikeni na uwanja na mbuga chato
kipi kipya kisichozoeleka kwa wanachi zaidi ya marudio hayo hayo ya sgr,flyover,ndege,mabeberu, na stiglers
 
Miaka mitano yote wamepiga siasa wenyewe mpaka kufika hatua ya kujiona upinzani wameuua saivi hawana la kuwaambia wananchi zimebaki tu mboyoyo mboyoyo za kila siku.

Kwa kifupi ccm wamepanic na raundi hii Zanzibar wanaipoteza na hapo ndipo watakopo gundua kuwa ni utopolo tu walikuwa wanafanya miaka mitano.
uzuri Mkapa hayupo safari hii mpira mtamu,wazungu ndo watakaoamua huu mtifuano.
 
Back
Top Bottom