Je mawe ya nyoka ni tiba sahihi?

Kimbori

JF-Expert Member
Feb 21, 2012
5,445
3,201
Haya mawe yanayouzwa kwa mbwebwe nyingi ya kwamba yanao uwezo wa kuondoa sumu ya nyoka yananipa maswali kadhaa ikiwayo:
- je ni kweli yanaondoa sumu ya nyoka?;
- je yanaondoa aina zote za sumu za nyoka?
Naomba kupata elimu kadiri ya uelewa wako.
 
NA MIMI NAOMBA NIDANDIE THREAD YAKO KWA KUULIZA SWALI
...hivi haya mawe ni natural au yanatengenezwa na watu?,,,na kama natural,yanatokeaje tokeaje?
 
navyofahamu mimi ile ni kwa ajili ya huduma ya kwanza hasa vijijini ambapo hospitali zipo mbali, kitu kimoja ambacho ni kibaya zaidi kutokana na ugumu wa maisha vijana wengi wanauza mawe feki kama ilivyo kwa wamasai ambao tiba zao nyingi hapa mjini kwa sasa ni za kisanii
 
Haya mawe yanayouzwa kwa mbwebwe nyingi ya kwamba yanao uwezo wa kuondoa sumu ya nyoka yananipa maswali kadhaa ikiwayo:
- je ni kweli yanaondoa sumu ya nyoka?;
- je yanaondoa aina zote za sumu za nyoka?
Naomba kupata elimu kadiri ya uelewa wako.

Hayo mawe usiyaamini, kwa sababu na feki pia yapo na kuyatofautisha ni ishu.
Theory ya ufanyaji kazi wake ni kwamba yanafyonza sumu ya nyoka, tandu,au nnge likiwekwa sehemu ambayo imen'gatwa na hao wajamaa.
Mtazamo wangu ni kwamba ikitokea umen'gatwa kwenye mshipa mkubwa wa damu, hilo jiwe sidhani kama litaweza kufyonza hiyo sumu.
Kipindi kile walikuwa wanawekewa hayo mawe wakati wanakimbizwa hospitali, kisaikolojia yanasaidia kumpa mtu matumaini hivyo moyo unapiga mapigo ya kawaida hivyo sumu haisambai kwa kasi mwilini. Mtu akingatwa na nyoka huwa ana-panic na mapigo ya moyo yanaongeza speed.
 
Kuna ukweli kama utapata kiwe halisi...nilishuhudia bibi yangu aling'atwa na nyoka na babu akamchanja alipoweka lile jiwe likanasa hadi lilipoanguka akajaribu kurudisha halikunasa na bibi hakulalamika 'alipona'. Hata nasikia wengine wanatumia sarafu sijui kama kweli.
 
Inawezekana yakawa ni tiba Mbadala,kwani hapo zamani huduma hizi za hospitali hazikuwepo katika maeneo mengi ya nchi yetu.na tujiulize kipindi hicho wazee wetu walikuwa wanajitibia na kitu gani kabla ya hizi hospitali?jibu ni moja tu kulikuwepo na dawa hizo za asili ikiwemo hayo mawe!ila kuweni waangalifu kuna watu si waaminifu!
 
Ni kweli mawe haya yanafanya kazi japo siku hizi usanii mwingi yapo ya "kichina" ila mara zoote ni kwa ajili ya huduma ya kwanza tu ... mengi yake yanapatikana naturally hayatengenezwi ila theory behind the contents sijui kwa kweli............
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom