Je mawaziri wetu wana mgomo baridi?

Wangepinga wangejiuzuru tu,otherwise hayo ni maneno tu ya kwenye kisutu cha kanga,maiti anakoshewa na biharusi anapambiwa hizo hizo na mtoto hubebewa.
 
Naanza kuitafakari hofu yangu niliyokuwa nayo wiki kadhaa zilizopita, maana nilikuwa nahisi kuwepo Kwa mgomo baridi wa Baraza la Mawaziri, ama kile kinachoitwa 'Mawaziri kususa', ambacho hivi sasa nakiona wazi wazi.

Ari na kasi waliyokuwa wameanza nayo Mawaziri ilikuwa ni kubwa sana, ilikuwa waziri akiingilia mlango huu, naibu waziri anatokea Kwa huku, yaani ofisi za umma zilichangamka na kila mtumishi wa umma alikuwa anasema "sasa hivi kazi tu, anaweza akaja waziri wakati wowote" yaani Waziri yupo mmoja, nchi ina mikoa zaidi ya 28, kila mtumishi katika kila mkoa alikuwa anadhani waziri anaweza kufika hapo Kwa muda huo huo, Kwa ufupi taifa liliingiwa na hofu kwamba awamu hii ssio ya mchezo, inachunguza na inafahamu kila kitu, wakati wote ukikosea unaonekana na utachukuliwa hatua papo Kwa papo..

Lakini, katika awamu zote, awamu hii imekuwa ndiyo awamu ya kwanza kuingia madarakani na kuanza kuzodolewa na wananchi ndani ya muda mfupi sana. Ile mihemuko yote imepotea, matumaini yamekufa, ndoto ya mabadiliko imeyeyuka, Kwa ufupi ni kwamba Tanzania mpya iliyozungumzwa imeota mbawa na kupeperukia kusikojulikana.

Mawaziri wamerudi nyuma, wamegundua kwamba wanafanya kazi ya MTU na sio ya nchi tena. Mawaziri wengi wamejisikia vibaya kudharauliwa nanushauri wao kupuuzwa, ilhali Mawaziri wetu wengi wao ni wasomi wazuri, wanauzoefu Mkubwa wa kiuongozi na hata baadhi yao walijiandaa kuongoza nchi, walichukua fomu za kugombea urais na kampeni za awali walifanya, hivyo watu Hawa wanapojihisi kudharauliwa na kupuuzwa, kwamba waendeshwe wote Kwa akili ya MTU mmoja, imewawia vigumu sana. Ndiyo maana tunasikia kwamba kuna masuala yanaamuliwa na Mawaziri mmoja mmoja bila kupitia kwenye vikao vya baraza la Mawaziri.

Leo nchi inaendeshwa na watu wawili: yaani Rais wa nchi na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, katika shughuli za maendeleo anayeonekana ni Rais na Mkuu wa mkoa wa DSM, hata katika uzinduzi wa miradi ya maendeleo, ni Rais mwenyewe na mkuu wa mkoa was DSM, hata waziri akiwepo, uwepo wake hautambuliki, Bali wanaoonekana nankusikika vizuri ni Rais na mkuu wa mkoa wa DSM. Hii inawavunja mioyo Mawaziri ambao ndiyo wasimamizi wa Sera katika mawizara yote, na watendahi wao makatibu wakuu.

Nikirejea aya iliyotangulia, ni kwamba utendaji kazi wa Mawaziri umedhoofika na umeshuka Kwa kiwango kikubwa sana, mshawasha waliokuwa nao kuhusu Tanzania mpya haupo tena, ziara za kushitukiza zimeonekana ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu, siasa za ukali na visasi zimetawala, Mawaziri kama chombo cha kumshauri Rais kimegeuka na kuwa chombo cha kuelekezwa na kushauriwa na Rais.

Waziri mkuu kama mtendaji mkuu wa shughuli za serikali Kwa mujibu wa katiba, na kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, amekuwa akifanya shughuli zake kama kivuli cha Rais, haonekani kutekeleza majukumu yake kama Mawaziri wakuu waliotangulia, Kwa ujumla sasa nchi inaendeshwa Kwa akili moja.

Watanzania ninawashauri kuwa wavumilivu lakini wenye kuitazama nchi inaelekea wapi na sio serikali inaelekea wapi, watanzania wafahamu kwamba sio hasara serikali ikianguka, Bali ni hasara nchi ikianguka, kwani serikali kuwepo madarakani ni Kwa makusudi ya wananchi wenyewe na wanao uwezo wa kuiweka madarakani serikali yoyote ile madhali wao wameamua, kwani Umma ndiyo wenye mamlaka ya mwisho katika nchi.

Sijaona bado tatizo la Rais wetu Mpendwa Magufuli na Mkuu wetu wa Mkoa Kipenzi cha wengi Paul Christian Makonda na nadhani utendaji wao ni mzuri mno na kama ikiwezekana Wote wanaweza kutuongoza maisha Watanzania.
 
Ukweli upo mkuu, mawaziri ni kama wapo wapo tu, hakuna hats wanalofanya likathaminika.
Katika mazingira ya sipangiwi fomu nilienda kuchukua mwenywe,na ukiniingilia ndio umepoteza kabisa waziri mwenye tafakuri sahihi anajua hii ngoma ina mwenywe, tu mwache aicheze, lakini siku zote ngoma ya mtu mmoja haidumu na wala hainogi.
 
Raisi bado anaimani na rc wa DSM, Hivo atuna budi kumusupoti. Hakuna namna nyingine.
 
Bashite ana nguvu zaidi ya PM....shangaa pia ana nguvu zaidi ya Mama wa Kwanza!!! Kijana wa kwanza amzidi Mama wa Kwanza!!!

Nadhani wale jamaa walioenda kolomije mganga kawaambia mkifika tu mkuu anawachamba wananchi maana baada ya kurudi south kawa na nguvu mpya
 
Naanza kuitafakari hofu yangu niliyokuwa nayo wiki kadhaa zilizopita, maana nilikuwa nahisi kuwepo Kwa mgomo baridi wa Baraza la Mawaziri, ama kile kinachoitwa 'Mawaziri kususa', ambacho hivi sasa nakiona wazi wazi.

Ari na kasi waliyokuwa wameanza nayo Mawaziri ilikuwa ni kubwa sana, ilikuwa waziri akiingilia mlango huu, naibu waziri anatokea Kwa huku, yaani ofisi za umma zilichangamka na kila mtumishi wa umma alikuwa anasema "sasa hivi kazi tu, anaweza akaja waziri wakati wowote" yaani Waziri yupo mmoja, nchi ina mikoa zaidi ya 28, kila mtumishi katika kila mkoa alikuwa anadhani waziri anaweza kufika hapo Kwa muda huo huo, Kwa ufupi taifa liliingiwa na hofu kwamba awamu hii ssio ya mchezo, inachunguza na inafahamu kila kitu, wakati wote ukikosea unaonekana na utachukuliwa hatua papo Kwa papo..

Lakini, katika awamu zote, awamu hii imekuwa ndiyo awamu ya kwanza kuingia madarakani na kuanza kuzodolewa na wananchi ndani ya muda mfupi sana. Ile mihemuko yote imepotea, matumaini yamekufa, ndoto ya mabadiliko imeyeyuka, Kwa ufupi ni kwamba Tanzania mpya iliyozungumzwa imeota mbawa na kupeperukia kusikojulikana.

Mawaziri wamerudi nyuma, wamegundua kwamba wanafanya kazi ya MTU na sio ya nchi tena. Mawaziri wengi wamejisikia vibaya kudharauliwa nanushauri wao kupuuzwa, ilhali Mawaziri wetu wengi wao ni wasomi wazuri, wanauzoefu Mkubwa wa kiuongozi na hata baadhi yao walijiandaa kuongoza nchi, walichukua fomu za kugombea urais na kampeni za awali walifanya, hivyo watu Hawa wanapojihisi kudharauliwa na kupuuzwa, kwamba waendeshwe wote Kwa akili ya MTU mmoja, imewawia vigumu sana. Ndiyo maana tunasikia kwamba kuna masuala yanaamuliwa na Mawaziri mmoja mmoja bila kupitia kwenye vikao vya baraza la Mawaziri.

Leo nchi inaendeshwa na watu wawili: yaani Rais wa nchi na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, katika shughuli za maendeleo anayeonekana ni Rais na Mkuu wa mkoa wa DSM, hata katika uzinduzi wa miradi ya maendeleo, ni Rais mwenyewe na mkuu wa mkoa was DSM, hata waziri akiwepo, uwepo wake hautambuliki, Bali wanaoonekana nankusikika vizuri ni Rais na mkuu wa mkoa wa DSM. Hii inawavunja mioyo Mawaziri ambao ndiyo wasimamizi wa Sera katika mawizara yote, na watendahi wao makatibu wakuu.

Nikirejea aya iliyotangulia, ni kwamba utendaji kazi wa Mawaziri umedhoofika na umeshuka Kwa kiwango kikubwa sana, mshawasha waliokuwa nao kuhusu Tanzania mpya haupo tena, ziara za kushitukiza zimeonekana ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu, siasa za ukali na visasi zimetawala, Mawaziri kama chombo cha kumshauri Rais kimegeuka na kuwa chombo cha kuelekezwa na kushauriwa na Rais.

Waziri mkuu kama mtendaji mkuu wa shughuli za serikali Kwa mujibu wa katiba, na kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, amekuwa akifanya shughuli zake kama kivuli cha Rais, haonekani kutekeleza majukumu yake kama Mawaziri wakuu waliotangulia, Kwa ujumla sasa nchi inaendeshwa Kwa akili moja.

Watanzania ninawashauri kuwa wavumilivu lakini wenye kuitazama nchi inaelekea wapi na sio serikali inaelekea wapi, watanzania wafahamu kwamba sio hasara serikali ikianguka, Bali ni hasara nchi ikianguka, kwani serikali kuwepo madarakani ni Kwa makusudi ya wananchi wenyewe na wanao uwezo wa kuiweka madarakani serikali yoyote ile madhali wao wameamua, kwani Umma ndiyo wenye mamlaka ya mwisho katika nchi.
Acha hizo propaganda zisizo na Msingi mfano tu Jana pale Ubungo Prof Mbarawa ametoa maelezo mengi kuhusu mradi wakati Rais akiweka jiwe la msingi na ndiye aliyemkaribisha Mkuu wa Nchi.

Na hata ziara ya Rais kusini mwa nchi mikoa ya Lindi na Mtwara mawaziri zaidi ya 6 waliongoza na Rais na ndiyo walikuwa wakitoa Maelezo ya miradi mbalimbali,mfano maji,umeme,barabarani n.k

Tusiandike tu mradi tunataka kumkosoa Rais basi ni kulaumu tu kila kitu wakati si kweli na ndiyo maana sometimes tunaweza kuwa na vitu vya maana ktk mitandao lakini kwasababu tunabase ktk kubeza tu basi kila mada zinaonekana haina maana.

Mawaziri wapo na wanafanya kazi zao kama kawaida ktk Wizara zao.
 
Lazima mkubali kwamba kuna makabila si ya kupewa madaraka makubwa na nyerere aliliiona hilo lakin ccm wakalipuuza maana hawajui hulka za makabila .wengine wanatakiwa waachwe waendelee kuwa wa majarubani tu.
Hakuna cha kabila wala nini - ni hulka ya mtu binafsi. Kwanza huyu amejipachika kabila kubwa wakati kakabila walikofikia wazazi wake walipokimbia vita ya Burundi ni kadogo sana, kama sio wazinza ni wasubi hapo Biharamulo. Kwa hivyo, akili ndogo na elements za udikteta havina mahusiano na kabila. In fact, wasomi wa Kisukuma wangefanya utafiti na kuuweka kwa uwazi kuwa huyu sio msukuma bali anawaharibia tu sifa nzuri waliyo nayo ya upendo na usikivu.
Kutetea vitendo vya Bashite kukosa maadili, sijonze amethibitisha kuwa ni a notorious abuser of power!
 
Rc kawaficha mawazir wote....hadi ipg!
Kimya.....rc ni kilaka

OvA
 
Wanapata mishahara ya bure. .kz zote kuna anae wafanyia so mmeona bw, nape kaunda tume asubuhi saa 4.majibu tayari. Mwakyela kapiga marufuku ndoa bila cheti akapewa za uso. Sasa yupi tena. Wa chakula kasemewa kipo tatizo nn tena ?
Leo(jana 20-3-2017),nmeshuka stendi nikakuta watu yaani normal people ambao ungehisi wana upeo mdogo kabisa walikua wanaongelea issue ya Dr Mwakyembe na hii ya pale Ubungo. Walisema hata nyumbani kwenye familia mambo ya ndani hayafanyiki kwa style ile hasa kama ilivyotokea kwa Dr Mwakyembe. Wakalaumu aina hii ya utendaji. Kwa kweli Watanzania hawa hawa wa kawaida kumbe wako makini kufuatilia mienendo. Natabiri 2020 kipute kuwa kigumu mno.
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom