Je, Mama Samia Suluhu Hassan ni Abdu Jumbe wa zama hizi?

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,458
17,282
Nawasalimia ndugu zangu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Moja kati ya salamu bora kabisa ya nyakati zetu.

Mama tangu ashike madaraka amekuja na surprise nyingi sana mojawapo ni uteuzi wa Makamu wa Rais ndugu Philip Mpango,tulitarajia uteuzi wa mtu mkongwe kwenye chama tena mwenye sauti ndani na nje ya chama lakini mama kamteua Mpango ambae hana mizizi ndani ya chama tena hana mtandao. Kwa jicho la tatu Mama kaogopa kumezwa na wanamtandao wa chama Tz Bara, ili awe na sauti ndani na nje ya chama kama kiongozi wa nchi.

Katika moja ya hotuba zake Mama alikosea kwa kusema Bunge la Katiba badala ya Bunge la Bajeti. Kwa mtazamo wa kawaida mama hakukosea kabisa bali amefikisha ujumbe anafikiria Katiba Mpya tena ya Serikali tatu ili kuipa mamlaka kamili Zanzibar.

Ikumbukwe vigogo wa CCM wameondolewa na mwendazake pale Bungeni hivyo basi itamsaidia mama kuleta mjadala wa Katiba Mpya tena rasimu ya Warioba ndani Bunge ambayo itapitishwa na kundi la wabunge wengi wachanga wa CCM wasio na mizizi na sioni kikwazo kwa Mama kwenye hili kwani kina Chenge, Sitta na vigogo wengi wa CCM hawamo Bungeni.

Naiona rasimu ya Warioba ikiwa Katiba Mpya na Mamlaka kamili ya Serikali ya Zanzibar.

Je, kama Zanzibar ikipewa mamlaka kamili itakubali kuburuzwa na Tanganyika?

Je, itakubali Majeshi ya Bara kuikalia Zanzibar tangu mapinduzi hadi leo?

Zama hizi hazina Maalim Seif wa kumfitini mama wala hakuna Baba wa taifa wa kumuweka mama kizuizini.

Nadhani kilio cha muda mrefu cha mamlaka kamili kitajibiwa na Mama yetu na adhma ya siri ya kifua cha Aboad Jumbe cha kuifanya Zanzibar kama Serikali yenye mamlaka kamili itatekelezwa katika awamu ya sita ya Mama yetu.
 
Simuoni wa kufanya hivyo ndani ya ccm; hata mama anapenda sana serikali tatu but nafsi yake haiwezi mruhusu kufanya hicho unacho kipendekeza; mfano serikali 3 zikipita kipindi cha utawala wake, maanake na yeye automatic anaachia urais; yaani rais wa muungano atoke Zanzibar? Halafu huyu raisi wa bara akubali kutoa pesa za kwenda Zanzibar au hata kumlipa yeye mshahara? Sidhani; tutaendelea hivi hivi.
 
Nawasalimia ndugu zangu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Moja kati ya salamu bora kabisa ya nyakati zetu.

Mama tangu ashike madaraka amekuja na surprise nyingi sana mojawapo ni uteuzi wa Makamu wa Rais ndugu Philip Mpango,tulitarajia uteuzi wa mtu mkongwe kwenye chama tena mwenye sauti ndani na nje ya chama lakini mama kamteua Mpango ambae hana mizizi ndani ya chama tena hana mtandao. Kwa jicho la tatu Mama kaogopa kumezwa na wanamtandao wa chama Tz Bara, ili awe na sauti ndani na nje ya chama kama kiongozi wa nchi.

Katika moja ya hotuba zake Mama alikosea kwa kusema Bunge la Katiba badala ya Bunge la Bajeti. Kwa mtazamo wa kawaida mama hakukosea kabisa bali amefikisha ujumbe anafikiria Katiba Mpya tena ya Serikali tatu ili kuipa mamlaka kamili Zanzibar.

Ikumbukwe vigogo wa CCM wameondolewa na mwendazake pale Bungeni hivyo basi itamsaidia mama kuleta mjadala wa Katiba Mpya tena rasimu ya Warioba ndani Bunge ambayo itapitishwa na kundi la wabunge wengi wachanga wa CCM wasio na mizizi na sioni kikwazo kwa Mama kwenye hili kwani kina Chenge, Sitta na vigogo wengi wa CCM hawamo Bungeni.

Naiona rasimu ya Warioba ikiwa Katiba Mpya na Mamlaka kamili ya Serikali ya Zanzibar.

Je, kama Zanzibar ikipewa mamlaka kamili itakubali kuburuzwa na Tanganyika?

Je, itakubali Majeshi ya Bara kuikalia Zanzibar tangu mapinduzi hadi leo?

Zama hizi hazina Maalim Seif wa kumfitini mama wala hakuna Baba wa taifa wa kumuweka mama kizuizini.

Nadhani kilio cha muda mrefu cha mamlaka kamili kitajibiwa na Mama yetu na adhma ya siri ya kifua cha Abdu Jumbe cha kuifanya Zanzibar kama Serikali yenye mamlaka kamili itatekelezwa katika awamu ya sita ya Mama yetu.
Katika uongozi wa Samia kuna dalili ya:
1. Mamlaka ya serikali ya muungano kupunguzwa sana
2. Tanzania bara kukamuliwa (fedha)
3. Zanzibar kupendelewa (ki mamlaka na fedha)
 
Katika uongozi wa Samia kuna dalili ya:
1. Mamlaka ya serikali ya muungano kupunguzwa sana
2. Tanzania bara kukamuliwa (fedha)
3. Zanzibar kupendelewa (ki mamlaka na fedha)
Ni vizuri tunafuata urithi wa Jiwe kupendelea Chato
 
Siku akitamka anataka serikali tatu, ndani ya muda mfupi atalazimishwa kujiuzuru.
Kuna watu hata katiba ya sasa hawaijui halafu wanapiga kelele za kutaka katiba mpya lakini pia wamesahau rais wa sasa alikuwa mwenyekiti mwenza wa bunge la katiba.
Wamekuwa wakimjazq mama maneno ambayo hata mwwnyewe hajayafikiria.
Mamlaka kamili ya Zanzibar sio tamko la rais bali mchakato inabidi uanzie ndani ya ccm kqbla ya kupelekwa bungeni na inabidi upate theruthi mbili ya kila upande bara na visiwani ndipo upitishwe
 
ItSiku akitamka anataka serikali tatu, ndani ya muda mfupi atalazimishwa kujiuzuru.
Ni nani mwenye ubavu huo? kwa uzuri wa katiba hii tuliyo nayo? Mh hayupo!
Kwa uzuri wa katiba hii rais ana mamlaka ya kumfifisha yeyote katika jamuhuri hii bila tabu yoyote ni tamko tu moja unakwisha habari yako! Je yupo shujaa?
Mtaje!
 
Mpango ulikalia hili suala, sasa Mwanga mpe mwana akulelee; Mnajua rais alimaanisha nini?
 
Kwahili la dp world na TANGANYIKA kutajwa tajwa kama nchi na Zanzibar !ni dhahiri shahiri muungano upo mashakani!!

Je Abdu jumbe wa zama hizi anaupiga mwingi kwenye Muungano!!!?
 
Back
Top Bottom