Ndugu wana JF, mara nyingi nimekuwa nikijiuliza majini ni kitu gani. Na najiuliza hivi kwa vile sijawahi kusikia mtoto au mke wa waziri, mbunge au rais fulani ana majini. Bali wote wanaokuwa na majini mara nyingi ni watu wa kawaida na maskini.
Mtoto (binti) wa mdogo wangu kaenda huko Kimanzichana (Mukuranga) kwa mwezi hivi na aliporudi nikaambiwa amepata majini. Sikuamini. Leo (10/02/2010) alianza kupiga kelele kwa sauti ya juu sana na wakati huo akiwa anaongea kama Kiarabu hivi (sijui kama ni correct Kiarabu au la). Kwa kweli nilishindwa cha kufanya.
Mke wangu akawa ananishauri nimwite sheikh ili ayatulize lakini kwa imani yangu sikufikiria kama kufanya hivyo ni sahihi.
Basi mama akaleta maji ya baraka kutoka kanisani na alipomumwagia akacharuka na kutaka kumpiga mama. Akawa anasema anataka kubadili dini. Basi nilichukua yale maji nikamumwagia zaidi na kisha "hilo jini" likasema linaondoka ila litarudi kumtembelea tena.
Kisha akaonekana kama mtu anayetoka usingizini na amechoka. Nikamwuliza: unataka kubadili dini? Akajibu hapana. Nikamwuliza tena, unafahamu Kiarabu? Akajibu hapana.
Hii ni phenomenon ambayo nataka niifanyie research. Ila kwa imani yangu nadhani inatokana na mtu kuwa na mlundikano wa mawazo (unfinished business) ya kusononesha na hivyo ni mojawapo ya 'effects' zake. Yaani, it's more psychological than real. Je, wan JF mnasemaje?
Mtoto (binti) wa mdogo wangu kaenda huko Kimanzichana (Mukuranga) kwa mwezi hivi na aliporudi nikaambiwa amepata majini. Sikuamini. Leo (10/02/2010) alianza kupiga kelele kwa sauti ya juu sana na wakati huo akiwa anaongea kama Kiarabu hivi (sijui kama ni correct Kiarabu au la). Kwa kweli nilishindwa cha kufanya.
Mke wangu akawa ananishauri nimwite sheikh ili ayatulize lakini kwa imani yangu sikufikiria kama kufanya hivyo ni sahihi.
Basi mama akaleta maji ya baraka kutoka kanisani na alipomumwagia akacharuka na kutaka kumpiga mama. Akawa anasema anataka kubadili dini. Basi nilichukua yale maji nikamumwagia zaidi na kisha "hilo jini" likasema linaondoka ila litarudi kumtembelea tena.
Kisha akaonekana kama mtu anayetoka usingizini na amechoka. Nikamwuliza: unataka kubadili dini? Akajibu hapana. Nikamwuliza tena, unafahamu Kiarabu? Akajibu hapana.
Hii ni phenomenon ambayo nataka niifanyie research. Ila kwa imani yangu nadhani inatokana na mtu kuwa na mlundikano wa mawazo (unfinished business) ya kusononesha na hivyo ni mojawapo ya 'effects' zake. Yaani, it's more psychological than real. Je, wan JF mnasemaje?