Je, mahakama zetu zimegoma kutumia lugha yetu ya Kiswahili kutoa haki za wananchi?

zandrano

JF-Expert Member
Jan 24, 2017
7,120
7,702
Katika pita pita yangu mahakamani, pamoja na sheria kurekebishwa bado nimegundua matumizi ya lugha ya Kingereza katika kutoa hukumu za wananchi yanaendelea kama kawaida huku lugha ya Kiswahili ikipuuzwa!!

wananchi wengi wanashangazwa sana na kinachoendelea bila kujua nini kinaendelea, maswali mengi wanajiuliza, je, dhamira iliyo kusudiwa na Bunge kwa kubadilisha sheria imepuuzwa!!

Je mahakama zetu haswa mahakama za wilaya, mikoa hadi mahakama kuu kwa nini hazitilii mkazo matumizi ya lugha ya kiswahili? Haki wanazo zitoa ni za watanzania au wazungu?

Je, ni kweli kuwa wizara ya katiba pamoja na mamlaka zingine zimeshindwa kutafasiri sheria mbalimbali kutoka kiingereza kwenda katika lugha ya Kiswahili?

Uzito unatoka wapi?! uzito wa jambo hili uko wapi? wananchi wanahitaji ufafanuzi, sio kukaa kimya na kuwapuuza.

Waziri wa Katiba na Sheria halioni hili?

Tunaomba ufafanuzi maana wananchi tunao enda kutafuta haki zetu Mahakamani tumeachwa njia panda!!
mara sijui unatafasiriwa kizungu kwa kiswahili!! mara sijui andika kiswahili na kizungu!! yaani ni vurugu tupu na kero kwa wananchi.

kesi imeamuliwa mahakama ya mwanzo kwa lugha ya kiswahili, unaamua kukata rufaa mahakama za juu unakutana na kizungu kuhusu jambo lililo amuliwa kwa kiswahili!!!
huku ni kuwababaisha wananchi katika kutafuta haki.


Kama Lugha ya Kiswahili imeshindikana kutumika kwenye Mahakama zetu basi ni bora jambo hilo lifahamike tu kuliko kuwasumbua wananchi na kutafasiri sijui kutoka kizungu kwenda kiswahili!! huu ni usumbufu mkubwa na utumwa!!

Amueni moja, kama ni kizungu basi twendeni na kizungu kuanzia mwanzo hadi mwisho, kama ni kiswhili vivihivyo, lakini sio kuchanganya, mara kizungu na kichina!! mnatubabisha, sisi sote ni waswahili wa kitanzania mnasumbuka kwa nn?! mnataka kumridhisha muwekezaji au mfadhili?!! badala ya mwananchi!!!
 
Katika pita pita yangu mahakamani, pamoja na sheria kurekebishwa bado nimegundua matumizi ya lugha ya Kingereza katika kutoa hukumu za wananchi yanaendelea kama kawaida huku lugha ya Kiswahili ikipuuzwa...

Siasa siasa siasa
 
Watanzania wengi ni watu waajabu sana.

Toka mwaka 1977, Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo na imeandikwa kwa Kiswahili rahisi sana;lakini cha ajabu kabisa bado Watanzania hawa 'Waswahili' hawajui haki zao za kikatiba kwa sababu aidha hawaisomi hiyo katiba ama wanasoma na hawawezi kutafsiri Katiba hiyo iliyoandikwa kwa Kiswahili fasaha.

Bado, kuna Sheria ya Mirathi ya Kimila ambayo nayo imeandikwa kwa Kiswahili: swali; je, ni kweli kwamba Watanzania ni weledi kwenye mirathi kwa kuwa sheria ipo kwa Kiswahili? Jibu ni hapana!

Mimi ninavyofahamu, Sheria ni taaluma, na ili uweze kuitafsiri ni lazima mtaalamu akusaidie; kufahamu Kiingereza siyo kigezo cha kuijua sheria, na wala kufahamu Kiswahili siyo kigezo cha kuimudu sheria.

Halafu jambo moja la hakika ni kwamba, Sheria nyingi hazijaandikwa kwa Kiingereza pekee, bali zimeandikwa kwa lugha ya sheria ambayo ni mchanganyiko wa Kilatin, Kifaransa na Kiingereza
 
Umeongea Jambo la mbolea Sana,huu ni upuuzi kama upuuzi mwingine, tumeamua kama Taifa tutumie lugha yetu adhimu ya Kiswahili lkn kuna wapuuzi wachache wakwamisha hizi juhudi.

Ifikie kipindi tuwe na ufahari WA kutumia lugha yetu katika mambo rasmi kama hayo
Hayo mambo waachieni wachina, warusi, waarabu, lugha zao wanazifaidi.
 
Katika pita pita yangu mahakamani, pamoja na sheria kurekebishwa bado nimegundua matumizi ya lugha ya Kingereza katika kutoa hukumu za wananchi yanaendelea kama kawaida huku lugha ya Kiswahili ikipuuzwa...
Kiswahili hakina reference(rejea) na precedents(mifuano au matukio) na misamiati ya kutosha ya lugha ya kisheria, hatuna literatures, waswahili hawana vitabu vya kutosha, lugha ya kiswahili ilikua over rated na Nyerere ingepaswa kutumika kwenye biashara tu na jeshini haijitoshelezi sana hata kwenye sayansi tekonolojia 80% ni kiingereza.

Ila sisi watu wakawaida tumesha pewa propaganda kwamba ni lugha ya taifa wakati inatumika tu kututawala kisiasa wenyewe watoto wao wanajifunza English hata nyumbani wanatumia kiingereza ila watoto wao wapate kuijua vzri. Sisi walala hoi tuna komaa na kiswahili, mwisho wa siku tunakosa ajira kwasbb hatuna connection (wasoma na nini na shule gani)
 
Kiswahili hakina reference(rejea) na precedents(mifuano au matukio) na misamiati ya kutosha ya lugha ya kisheria, hatuna literatures, waswahili hawana vitabu vya kutosha, lugha ya kiswahili ilikua over rated na Nyerere ingepaswa kutumaka kwenye biashara tu na jeshini haijitosherezi sana hata kwenye sayansi tekonolojia 80% ni kiingereza.

Ila sisi watu wakawaida tumesha pewa propaganda kwamba ni lugha ya taifa wakati inatumika tu kututawala kisiasa wenyewe watoto wao wanajifunza English hata nyumbani wanatumia kiongereza ila watoto wao wapate kuijua vzri.
Kama kuna hayo mapungufu si yanafanyiwa kazi Tu

Ila tusiseme haiwezekani huo utakuwa ni uongo
 
Katika pita pita yangu mahakamani, pamoja na sheria kurekebishwa bado nimegundua matumizi ya lugha ya Kingereza katika kutoa hukumu za wananchi yanaendelea kama kawaida huku lugha ya Kiswahili ikipuuzwa!!

wananchi wengi wanashangazwa sana na kinachoendelea bila kujua nini kinaendelea, maswali mengi wanajiuliza, je, dhamira iliyo kusudiwa na Bunge kwa kubadilisha sheria imepuuzwa!!

je mahakama zetu haswa mahakama za wilaya, mikoa hadi mahakama kuu kwa nini hazitilii mkazo matumizi ya lugha ya kiswahili?!!
haki wanazo zitoa ni za watanzania au wazungu?

Je, ni kweli kuwa wizara ya katiba pamoja na mamlaka zingine zimeshindwa kutafasiri sheria mbalimbali kutoka kiingereza kwenda katika lugha ya Kiswahili?!

Uzito unatoka wapi?! uzito wa jambo hili uko wapi?! wananchi wanahitaji ufafanuzi, sio kukaa kimya na kuwapuuza.

Waziri wa Katiba na Sheria halioni hili?
Tunaomba ufafanuzi maana wananchi tunao enda kutafuta haki zetu Mahakamani tumeachwa njia panda!!
mara sijui unatafasiriwa kizungu kwa kiswahili!! mara sijui andika kiswahili na kizungu!! yaani ni vurugu tupu na kero kwa wananchi.

Kama Lugha ya Kiswahili imeshindikana kutumika kwenye Mahakama zetu basi ni bora jambo hilo lifahamike tu kuliko kuwasumbua wananchi na kutafasiri sijui kutoka kizungu kwenda kiswahili!! huu ni usumbufu mkubwa na utumwa!!
Uelewe ulete shida hujui wanafanya makusudi ili usielewe na vile tunaogopa kizungu wengi wetu basi ni ile system wachanganye wasikuelewe. Tuna sheria mbunge ajue kuandika na kusoma tu sasa hata sheria ukizipeleka kupitishwa ni rahisi tu hakuna wa kuhoji kila mtu anaogopa lugha. Ukienda kuchukuwa mkopo bank mkataba kizungu wanajuwa madhaifu yetu na hii inawasaidia wao kutawala bila sisi kujuwa haki zetu.
 
Unaona wa Tanzania dani ya mwaka au miaka kubadilika waanze kuandika vitabu kua na tamaduni ya kusoma vitabu, sio rahisi chawa ni nyingi sanaa hapa.
Ni kweli utamaduni WA kusoma ni mtihani

Lakini je,unataka kuniambia lugha ya kisheria haiwezi kabisa kueleweka kwakuwa Tu lugha yetu haina misamiati ya kutosha?
 
Kiswahili hakina reference(rejea) na precedents(mifuano au matukio) na misamiati ya kutosha ya lugha ya kisheria, hatuna literatures, waswahili hawana vitabu vya kutosha, lugha ya kiswahili ilikua over rated na Nyerere ingepaswa kutumaka kwenye biashara tu na jeshini haijitosherezi sana hata kwenye sayansi tekonolojia 80% ni kiingereza.

Ila sisi watu wakawaida tumesha pewa propaganda kwamba ni lugha ya taifa wakati inatumika tu kututawala kisiasa wenyewe watoto wao wanajifunza English hata nyumbani wanatumia kiongereza ila watoto wao wapate kuijua vzri.
Wacha kudharau Kiswahili.
kiswahili ni Tunu yetu, ndio kitambulisho chetu.

Kiswahili ni Lugha Kongwe yenye misamiati ya kutosha, inayo kuwa kila kukicha.

Tuna wataalamu wa kiswahili walio bobea, tuna vyombo kama TUKI, TUKTA na maabara za kutosha, ambazo kila kukicha wana zalisha misamiati. tuna kamusi/dectationary za kizungu kwenda kiswahili.

Tatizo ni Utashi wa kukitumia kiswahili, visingizio vinavyo tolewa havina uzito wowote ni ulevi tu wa kujiona na kujigamba, lkn wanao umia ni wananchi.

Laiti JPM ange kuwa hai hadi leo Kiswahili Mahakamani Kingetumika kikamilifu na pasingekuwa na hizi ngojera.
 
Wacha kudharau Kiswahili.
kiswahili ni Tunu yetu, ndio kitambulisho chetu.

Kiswahili ni Lugha Kongwe yenye misamiati ya kutosha, inayo kuwa kila kukicha.

Tuna wataalamu wa kiswahili walio bobea, tuna vyombo kama TUKI, TUKTA na maabara za kutosha, ambazo kila kukicha wana zalisha misamiati.

Tatizo ni Utashi wa kukitumia kiswahili, visingizio vinavyo tolewa havina uzito wowote ni ulevi tu wa kujiona na kujigamba, lkn wanao umia ni wananchi.
Mkuu hizo ni propaganda za Chama tawala kiswahili bado sana, acha hiki kiwahili cha kuongea mitaani, ukweli kiswahili hakina literature, naomba unitajie vitabu 10 ulivyo soma vya kiswahili "O" na "A" kama sio kile cha "wasakatonge" chenye kurasa 40 tu........
Wataalamu wa kiswahili TuKu ni wakisiasa hawana publication yoyote yamaana kiswahili hakina kitabu cha computer abayo ni basic ya sayansi na tekinolojia
 
Watanzania wengi ni watu waajabu sana.

Toka mwaka 1977, Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo na imeandikwa kwa Kiswahili rahisi sana;lakini cha ajabu kabisa bado Watanzania hawa 'Waswahili' hawajui haki zao za kikatiba kwa sababu aidha hawaisomi hiyo katiba ama wanasoma na hawawezi kutafsiri Katiba hiyo iliyoandikwa kwa Kiswahili fasaha.

Bado, kuna Sheria ya Mirathi ya Kimila ambayo nayo imeandikwa kwa Kiswahili: swali; je, ni kweli kwamba Watanzania ni weledi kwenye mirathi kwa kuwa sheria ipo kwa Kiswahili? Jibu ni hapana!

Mimi ninavyofahamu, Sheria ni taaluma, na ili uweze kuitafsiri ni lazima mtaalamu akusaidie; kufahamu Kiingereza siyo kigezo cha kuijua sheria, na wala kufahamu Kiswahili siyo kigezo cha kuimudu sheria.

Halafu jambo moja la hakika ni kwamba, Sheria nyingi hazijaandikwa kwa Kiingereza pekee, bali zimeandikwa kwa lugha ya sheria ambayo ni mchanganyiko wa Kilatin, Kifaransa na Kiingereza
tatizo sio kuelewa lugha za kisheria bali ni kuelewa kile kilicho amuliwa na mahakama.
kwa kutumia lugha ya kiswahili mwananchi wa kawaida anaweza kusoma maamuzi na kuelewa kilicho amuliwa, lakini hukumu inapo andikwa kwa kizungu hakuna hata jambo moja analo weza kuambulia.

Bado kuna fikira za kitumwa! tunadhani kujua kuandika kizungu ndio weledi na akili!!! na kutokujua ni ujinga!!.
 
Mkuu hizo ni propaganda za Chama tawala kiswahili bado sana, acha hiki kiwahili cha kuongea mitaani, ukweli kiswahili hakina literature, naomba unitajie vitabu 10 ulivyo soma vya kiswahili "O" na "A" kama sio kile cha "wasakatonge" chenye kurasa 40 tu........
Wataalamu wa kiswahili TuKu ni wakisiasa hawana publication yoyote yamaana kiswahili hakina kitabu cha computer abayo ni basic ya sayansi na tekinolojia
Labda hakuelewi unaposema Kiswahili hakina Literature,mueleweshe vizuri!! Kiswahili kinapungukiwa mambo mengi sana
 
Labda hakuelewi unaposema Kiswahili hakina Literature,mueleweshe vizuri!! Kiswahili kinapungukiwa mambo mengi sana
kiswahili hakijapungukiwa, bali sisi wenyewe ndio tulio pungukiwa.
angalia katika orodha ya ulimwengu, lugha ya Kiswahili inatafasiriwa katika teknolojia.

Lakini swali la kujiuliza, iweje mahakama za mwanzo zote zinaweza kutumia lugha ya kiswahili, sheria zote zipo kwa lugha ya Kiswahili lakini unapo kwenda mahakama za wilaya, mikoa, mahakama kuu hadi mahaka za rufaa wanashindwa kutumia lugha ya kiswahili?!

hapa kuna tatizo.
 
Back
Top Bottom