Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Katika mjadala unaoendelea sasa hivi katika idhaa ya Kiswahili ya BBC, Charles Hillary amemtambulisha Magid Mjengwa kama Mwanakijiji. Magid anashiriki mjadala kuhusu mauaji yaliyotokea Norway (akiwa Sweden) na hakukanusha kwamba yeye si Mwanakijiji. Ina maana kwamba yeye kweli ni Mwanakijiji??
Labda atakuja kutupatia ufafanuzi kwanii mimi nijuavyo, Majid siyo Mwanakijiji wa JF a.k.a Mzee Mwanakijiji!
Labda atakuja kutupatia ufafanuzi kwanii mimi nijuavyo, Majid siyo Mwanakijiji wa JF a.k.a Mzee Mwanakijiji!
Ndugu yangu Mayasa,
Ahsante sana kuwaonyesha wengine njia. Uko sahihi kwa asilimia mia moja. Kwa vile Mjengwablog niliamua kuiita ' Kijiji' ambamo watembeleaji ni kama 'wanakijiji' wa Mjengwablog, basi, kuna walioamua kuniita ' Mwenyekiti' wakimaanisha Mwenyekiti wa Kijiji. Kaka yangu Charles Hillary ni mmoja wa ' Wanakijiji' wangu na alielekea huko katika kunitambulisha.
Sikuona umuhimu wa kuanza mjadala kwa kukanusha redioni ( BBC) utambulisho ule wa kuitwa ' Mwanakijiji'. Ni kwa vile yaliyokuwa mbele yetu katika mjadala ule yalikuwa ya muhimu zaidi. Kila dakika ilikuwa na umuhimu zaidi kuliko kuipoteza kwa kuwachanganya wasikilizaji juu ya "Oh, mimi sio ' Mwanakijiji' ni ' Mwenyekiti' na blah blah nyingine. Kwani kama ' Mwenyekiti' wa kijiji anaishi katika kijiji anachokiongoza kuna kosa gani kuitwa mwanakijiji?
Hivyo basi, niliyoyaandika hapa ndio yachukuliwe kuwa usahihi wa jambo zima na mengine mliyosoma yachuliwe kama ' Porojo za kuchangamsha kijiwe!"- Hata mie zimenichangamsha, ahsanteni sana!
Maggid
( 'Mwenyekiti' na 'Mwanakijiji' wa Kijiji Cha Mjengwablog. Unakaribishwa kijijini kwetu!)
PS: Mzee Mwanakijiji pia ni 'Mwanakijiji' wangu na mie ni ' Mwanakiji' wake, mwenye kubisha akamwulize!