Je, laana ya rasilimali ni nini? (Resource curse).

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
0001-15435118420_20210112_131900_0000.png


Hii ni dhana inayotolewa na ushahidi dhidi ya Nchi zenye Rasilimali na Maliasili nyingi kushindwa kuendelea kiuchumi ukilinganisha na nchi zisizokuwa na Rasilimali nyingi.

Dhana hii ya Laana ya Rasilimali ina nadhalia kubwa tatu:-

1. Nchi zenye utajiri mkubwa katika Rasilimali na Maliasili zinakuwa taratibu kiuchumi kushinda nchi zisizokuwa tajiri katika Rasilimali na Maliasili.

2. Nchi zisizo kuwa tajiri kwenye maliasili zina uchumi mkubwa kushinda Nchi zenye utajiri wa Maliasili.

3. Nchi zenye Rasilimali nyingi zinaongoza kwa umaskini na Rushwa kushinda Nchi zisizokuwa na utajiri wa Rasilimali na Maliasili.

Hivyo dhana hii inasema kwamba Kuwa na Utajiri wa Rasilimali ni Laana ya Maendeleo katika Nchi. Katika Dhana hii kwenye ushahidi zinatajwa Nchi kama DRC, Equatorial Guinea, Sierra Leone, Liberia, Venezuela n.k.
 
Wanatudanganya. Kuna nchi nyingi zenye rasilimali. Marekani hawana tanzanite. Wana madini mengi. Wana ardhi kubwa kuliko sisi. Wana bahari pande mbili. Wana maziwa makubwa na mito mikubwa. Kwa nini wao wasiwe na resource curse?

Urusi ni nchi kubwa kuliko zote. Wana gesi nyingi wanasambaza ulaya nzima. Kwa nini wao wasiwe na resource curse.

Rasilimali ya muhimu duniani ni watu? Watu wenye utashi, weledi na jamii yenye mifumo ya uzalishaji ya kueleweka.

Sisi tushukuru hizo mali vinginevyo tungekuwa kama Burundi.
 
China ina rasilimali nyingi sana, Russia ana rasilimali nyingi pia, Hata Marekani anazo...bila kumsahau India. Kwa hiyo, hiyo dhana ina mushikeli tena mkubwa tu!!! Inabidi jina la dhana libadilishwe ili kuendana na uhalisia.
 
Kama ulivyosema hizo ni nadharia (Theories) tu: Tatizo la mwafrika liko kichwani kwake.
Wewe angalia tu, mtu kaamua kukwapua rasilimali na kwenda kujenga kijijini kwao Chato.
Heri sasa akafanya hata Strategic Investment basi, lakini vyote hivyo ni White Elephants.

Hapohapo nchi nzima iko kimya na vyombo vya usalama ndiyo vinasaidia huu upumbavu.
Halafu mwisho kabisa tunasema laana, laana gani bwana wakati mwafrika hatumii akili.
 
Laana ya rasilimali inahusisha demokrasia finyu na ukandamizaji mkubwa pia.
China ina rasilimali nyingi sana, Russia ana rasilimali nyingi pia, Hata Marekani anazo...bila kumsahau India. Kwa hiyo, hiyo dhana ina mushikeli tena mkubwa tu!!! Inabidi jina la dhana libadilishwe ili kuendana na uhalisia.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom