Je, kwa mshahara wa Shilingi 310,000 unaweza kuishi Dar es Salaam?

Maisha yako ndio yataamua.

Mimi kipato changu kwa mwezi hakizidi laki 3 kwasasa ila mahitaji yangu yote nafanya ikiwemo kumsaidia mama, kulipa kodi, kula, maji, nauli, SACCOS, kuwekeza, kuhonga, kuwapa wapiga mizinga.

Na hii ni kwasababu binafsi,
  • Sinywi pombe
  • Sivuti sigara wala chochote
  • siyo mtu wa mambo mengi sijui parties, birthday
  • Huwa natoka mara moja moja sana nikiwa stressed.
  • Mara nyingi mimi ni mtu wa kukaa ndani tu, na sio kwamba najitesa au najinyima hapana. I just enjoy being alone

Kwahiyo lifestyle yako ndio ita determine kama kipato hicho kinatosha amma la.
Hebu weka mchanganuo wa gharama za usafiri na chakula kwa siku.

Hivi vipato vya watu vingi mtu hutoboi bila kujiongeza. Hata hao walinzi na wafanya usafi maofisini wana namna nyingine ya kupata hela. Mfano wafanya usafi wanakubali kutumwa huku na kule. Ukimtuma unamlipa elfu 1. Kwahiyo ana uhakika wa kuongeza kipato na kupunguza makali ya maisha kwa kutumwa tumwa. Yani kila mmoja ana namna yake ya kuongeza kipato. Sasa watu huwa wanasahau kupigia mahesabu hizi hela wanazopata kila siku hata kama ni elfu 2 ndio maana watu wanasema kwamba mimi kipato changu 150,000 na nimejenga.

Mkiwaambia watu muwaambie na zile namna nyingine mmejiongeza kupunguza ukali wa maisha.
 
Maji kwa mwenzi Dar bill imezd sana 20k labda kama unaongelea Masaki na ostabay uko
Unaongelea bill ipi? Make situmii maji ya dawasco (hayajafika huku)... Kuna yale maji ya visima yaliyounganishwa mabomba, nilikua nalipa bill elf10 hadi 25 per month, ambayo nayo yamekata sijui wenye mradi wana migogoro na Tanesco hivo kwa sasa ni ya kununua...
5000 kila baada ya siku tatu. Piga hesabu kwa mwezi ni zaidi ya hiyo 50
Bila kusahau matumizi ya maji yanategemea na idadi ya watumiaji , ukiishi mwenyewe tofauti na familia, nguo za watoto kufua ni sana.
 
2014 nilikua nalipwa 250,000/= kwa mwez nikawa naish tu nina mke na mtoto hata sijui nilikua naishije...Leo hii nalipwa 2,500,000/= hata bado sijui naishije yan naona siku zinaenda tu.Nadhan Mungu ndio wa kunisaidia nitoke hapa
Kaka mapato huwa yanaenda na matumizi, enzi zile unalipwa 250k ulikua unaenda kula kwa mamantilie. Siku hizi huo msosi unaona kama matusi fulani.


Kingine ni pisi na bia dah.
 
Kaka mapato huwa yanaenda na matumizi, enzi zile unalipwa 250k ulikua unaenda kula kwa mamantilie. Siku hizi huo msosi unaona kama matusi fulani.


Kingine ni pisi na bia dah.
Kaka sinywi bia.Nikila lunch ya ghali sana labda 10k na sometimes nakula kawaida tu ya 3k usafir natumia daladala gar yangu natumia kwa matumiz ya kawaida tu.Tar 1/01/2020 ndio ilikua mara ya mwisho kuchepuka...Kwa kifup naish a very average life sasa sijui shida iko wap mkuu.Heb nishaur natokaje hapa.
 
Kaka sinywi bia.Nikila lunch ya ghali sana labda 10k na sometimes nakula kawaida tu ya 3k usafir natumia daladala gar yangu natumia kwa matumiz ya kawaida tu.Tar 1/01/2020 ndio ilikua mara ya mwisho kuchepuka...Kwa kifup naish a very average life sasa sijui shida iko wap mkuu.Heb nishaur natokaje hapa.
Labda kuna chuma ulete anakutumia 😂😂😂
 
Habari wadau!

Ebu nisaidieni hivi kweli 310,000/= inatosha mtu kufanya kazi na kuishi DAR au unatakiwa kuwa na miundombinu mingine?
Sema jitahidi usiwe unaishi mbali na eneo LA kazi, ikiwezekana unatembea kwa mguu kabisa mpaka kazini , maisha yataenda hivyo hivyo Mdogo mdogo
 
Kwenye taasisi ninayofanyia kazi wafanya usafi wote ni vibarua walioko chini ya kampuni binafsi,kuna kampuni nyingi ila mishahara yao ni kati ya 100,000tsh hadi 150,000tsh na kipindi kingine wanakata hata miezi 2 hawajalipwa na wanakuja kila siku bila kukosa, kuna mmoja alinambia anakaa mbagara charambe na ofisi ipo mjini
 
Kaka sinywi bia.Nikila lunch ya ghali sana labda 10k na sometimes nakula kawaida tu ya 3k usafir natumia daladala gar yangu natumia kwa matumiz ya kawaida tu.Tar 1/01/2020 ndio ilikua mara ya mwisho kuchepuka...Kwa kifup naish a very average life sasa sijui shida iko wap mkuu.Heb nishaur natokaje hapa.
Una mkopo benki? SACCOSS je? Unasomesha? Umejenga au bado unalipa kodi?

Nijibu hayo mkuu nipate mwanga wa kukushauri.
 
2014 nilikua nalipwa 250,000/= kwa mwez nikawa naish tu nina mke na mtoto hata sijui nilikua naishije...Leo hii nalipwa 2,500,000/= hata bado sijui naishije yan naona siku zinaenda tu.Nadhan Mungu ndio wa kunisaidia nitoke hapa
Bora wewe umejitokeza, ndiyo watu waelewe kuwa matumizi yaendane na kipato. Ukishindwa kujibana kwa kidogo unachopata, hata ukipata kikubwa utafeli tu.
 
2014 nilikua nalipwa 250,000/= kwa mwez nikawa naish tu nina mke na mtoto hata sijui nilikua naishije...Leo hii nalipwa 2,500,000/= hata bado sijui naishije yan naona siku zinaenda tu.Nadhan Mungu ndio wa kunisaidia nitoke hapa
Mkuu angalia utafika hadi mshahara wa 10m kwa mwezi na hautakutosha.
 
Kwenye taasisi ninayofanyia kazi wafanya usafi wote ni vibarua walioko chini ya kampuni binafsi,kuna kampuni nyingi ila mishahara yao ni kati ya 100,000tsh hadi 150,000tsh na kipindi kingine wanakata hata miezi 2 hawajalipwa na wanakuja kila siku bila kukosa, kuna mmoja alinambia anakaa mbagara charambe na ofisi ipo mjini
Wengi ni mabinti,it is possible hata wasipolipwa 4 months wanasurvive ila sio kwa mwanaume
 
Una mkopo benki? SACCOSS je? Unasomesha? Umejenga au bado unalipa kodi?

Nijibu hayo mkuu nipate mwanga wa kukushauri.
Sina mkopo wa bank labda vicoba vya wife huko huwa nam boost mara moja moja, u know women.Nina watoto wawili naosomesha .
Sijapanga naishi kwangu hivyo silipi kodi mkuu..Nisaidie kwa hapo
 
Hebu weka mchanganuo wa gharama za usafiri na chakula kwa siku.

Hivi vipato vya watu vingi mtu hutoboi bila kujiongeza. Hata hao walinzi na wafanya usafi maofisini wana namna nyingine ya kupata hela. Mfano wafanya usafi wanakubali kutumwa huku na kule. Ukimtuma unamlipa elfu 1. Kwahiyo ana uhakika wa kuongeza kipato na kupunguza makali ya maisha kwa kutumwa tumwa. Yani kila mmoja ana namna yake ya kuongeza kipato. Sasa watu huwa wanasahau kupigia mahesabu hizi hela wanazopata kila siku hata kama ni elfu 2 ndio maana watu wanasema kwamba mimi kipato changu 150,000 na nimejenga.

Mkiwaambia watu muwaambie na zile namna nyingine mmejiongeza kupunguza ukali wa maisha.
Matumizi muhimu: Tsh 80,000 chakula, Nauli Tsh 30,000.

Maji Tsh 5000, Umeme 10,000.
 
Kwa mjini Kodi za nyumba ndio zinawafanya watu wengi wasiendelee mbele.

Wapo wanaoshindwa kutafuta nyumba za kupanga zinazoendana na kipato chao,mtu unalipwa laki 3 unakaa nyumba ya 100k kwa mwezi hapo lazima ukwame kodi ya nyumba lazima hiwe chini ya asilimia 10 ya mshahara wako.
 
Back
Top Bottom