Hiyo ni mbinu ya serikali kutaka kuwazuia wananchi kujua ukweli wa kinachoendelea muhimbili ili kupunguza kelele za kukosa huduma km huduma za dharura ingawa sidhani kama ni kwa kiwango kinachotakiwa
Viongozi wa Govt ya JK, wana akili ya mbuni, ya kuficha kichwa katika mchanga, huku maadui wakiendelea kuona kiwiliwili chote!
Ni kama mchezo wa kuigiza vile! Huko Jeshini walikotoka madaktari hao, kwa sasa nako uhaba wa madaktari, umeongezeka. Lengo ni kujaribu "kuficha" aibu ya Muhimbili, "inayoonekana zaidi kwa watu wa media", kuliko ya hospitali za Lugalo n.k! Na vilevile kuwaonesha madaktari waliogoma, "nguvu za Serikali"! This is Leadership, at the lowest decision making capability!
:canada:Taarifa zilonifikia, za uhakika kuwa kesho saa 1:30 asubuhi Star Tv watarusha mjadala wa Mgogoro wa Madaktari. Wataokuwepo ni pamoja na Dr. Ulimboka , Mwakilishi wa Serikali na Marcossy Albaine wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). Tarajio langu watatuchambulia kwa kina tatizo liko wapi?:lol:
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.