Kwa hiyo wangesikiliza muda huu ingekua....Wanabodi,
Tanzania ni nchi ya Jamhuri ya Muungano, yenye watu kutoka iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, na kuunda nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao rais wake wa pande zote mbili, wako sawa na wana uhuru kamili wa kila kitu ikiwemo kugombea na kushika madaraka ya nafasi juu kabisa ya uongozi kwenye JMT, hii ni nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Baada ya Nyerere kutoka Bara, alifuatiwa na Mwinyi kutoka Zanzibar.
Wakati wa kipindi cha Mwinyi, makamo wa rais ndiye pia alikuwa Waziri Mkuu wa JMT na Mwinyi alihudumiwa na ma Makamu watatu, Joseph Sinde Warioba, John Samwel Malecela na Cleopa David Msuya, na kipindi hiki cha Mwinyi, 1992, ndipo Tanzania tukaingia kwenye mfumo wa vyama vingi, na CCM kwa kuogopa, wa urais wa Zanzibar kushikwa na mtu wa chama kingine, wakati ndio set up ya muungano kuwa rais akitoka Bara, makamo lazima atoke Zanzibar, iwapo Zanzibar itashikwa na chama kingine, itakuwaje?, ndipo wakaamua kubadili katiba na kumfanya rais wa Zanzibar ni nothing ndani ya set up ya muungano!, na huu ndio ukawa mwisho rasmi wa mtu kutoka Zanzibar kuwa rais wa JMT!.
Baada ya Mwinyi, akaja Mkapa kutoka Bara, ilibidi Mkapa kufuatiwa na mtu kutoka Zanzibar, lakini yalifanyika mambo ( refer uzi huu JK, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza ..
Hivi ndivyo zamu ya Zanzibar ilivyopokwa!) hivyo akafuatiwa na Jakaya Kikwete pia kutoka Bara, na sasa tukiwa tunaelekea 2015, sijabahatika kusikia sikia majina yoyote ya possibility ya Mzanzibari yakitajwa tajwa au any possibility ya mgombea yoyote wa nafasi ya urais wa JMT kutoka tena Zanzibar!.
Naomba kukiri, ninaandika uzi huu kufuatia inspiration niliyoipata toka kwa mwana jf huyu
Jee inawezekana sababu halali kwa nini Mzanzibari hawezi tena kuwa ni rais wa JMT?.
Naomba tuanze kwa kuweka facts mezani!.
Natanguliza samahani msinione mbaguzi, hizi zinaweza kuwa ndizo sababu halisi zinazosimama kama facts zinazopelekea Mzanzibari, asipate tena nafasi ya kuwa rais wa JMT!, Hamdhani kwamba sasa umefika wakati, kunahitajika some specific measures kama some kind of affirmative action, kuhakikisha, rais wa JMT pia apatikane kutoka upande wa pindi wa muungano?, yani kwa wapenda haki, hatuwezi kuacha ,rais wa JMT , andelee tuu kuchaguliwa by chance, kutoka upande wowote wa JMT wakati kuna kila dalili za kuonyesha kamwe rais wa JMT, hawezi tena kutoka Zanzibar by chance, hivyo marais wote wa Tanzania ya vyama vingi ni kutoka upande mmoja tuu wa Muungano huku bara!. Is this fair kwa wenzetu Wazanzibari?!. Hamdhani huu ni wakati muafaka tuwe na affirmative action ili Mzanzibari aweze tena kuwa rais wa JMT?.
- Eneo lote la Zanzibar lilikuwa ni sehemu ya Tanganyika, hivyo Zanzibar ni sehemu halali ya Tanganyika!.
- Kufuatia Zanzibar kuwa ni sehemu ya Tanganyika, wakaazi wake wa asili ni Wamatumbi kutoka Tanganyika!.
- Kuna miaka fulani, wavamizi fulani wa Kiarabu kutoka nchi ya Oman, waliivamia Zanzibar, wakajifanya ni nchi yao na kuuhamishia ufalme wao kutoka Oman na kuja Zanzibar, wakazaliana, sasa wanajidhania hapo ni kwao, kiukweli hapo kwao kwa kuzaliwa tuu, lakini kiasili, sio kwao, bali mahali tuu walipozaliwa na kukulia!. Ukizaliwa India, ukakulia India, hakukufanyi uwe Mhindi, wewe utabaki ni Mmatumbi tuu!.
- Wavamizi hawa wakaanzisha biashara haramu ya Utumwa, ambapo Watumwa waliokuwa hawana soko, waliachwa Zanzibar. Biashara ya utumwa ulipopigwa marufuku, wengi wa watumwa hawa, walibaki Zanzibar kama watu huru na wao pia kujihesabu ni Wazanzibari!.
- December 1963, wavamizi hawa wakapewa uhuru wa bandia na Waingereza!, Wamatumbi hawakukubali, mwezi mmoja baadae, ile Januari 12, 1964, wakiongozwa na Mmatumbi John Okello kutoka Uganda, walifanya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na kumfurusha "mvamizi yule!" na kujitwalia Uhuru ambapo mtu mwenye asili ya Malawi, Abedi Amani Karume alitangazwa ndie Rais wa Zanzibar na M/Baraza la Mapinduzi.
- Aprili 26, 1964, Rais Nyerere na Karume waliziunganisha nchi hizi mbili, na kuunda Tanzania. Rais wa Tanzania siku zote lazima atakuwa ni Mtanzania kutoka upande wowote wa Muungano.
- Nyerere alitoka Bara, Mwinyi alitoka Zanzibar, japo alizaliwa bara pale Mkuranga, na ndio maana anaishi Bara! hadi sasa!. Mkapa alitoka Bara japo alizaliwa "Nchumbiji!" JK pia ni kutoka Bara, anayefuatia pia atatoka Bara "Ule Mwamba wa Kaskazi", na atafuatiwa na Bara, na Bara, na Bara tena!, hakuna wakati mwingine wowote ambao Rais wa JMT, atatoka nje ya Bara!.
- Kufuatia Zanzibar kukosa tafsiri rasmi ya Mzanzibari ni nani, Mzanzibari wa asili ni Mmatumbi kutoka Tanganyika, lakini sasa "wale wavamizi!", nao wanajiita Wanzanzibar!, vizalia vya masalia ya Watumwa, nao kwa vile wamezaliwa Zanzibar, nao wanajiita Wazanzibar, hivyo its very risk kukubali mtu kutoka Zanzibar kuwa rais wa JMT, wao mwisho wao ni kututolea Makamo wa Rais tuu.
- Be ware, wale ambao sio Wanzanzibari wa asili, na haswa vizalia vya "wavamizi" ndio wenye kelele sana!, tuwe waangalifu sana na kila kelele kwa kumuangalia vuzuri kwa jicho chunguzi, kila anayeupigia kelele zamu ya Uzanzibari kwenye urais wa JMT, kwa kujiuliza kama jee ni Mzanzibari kweli au ni wale "wavamizi!.
- Tanzania ni kwa Watanzania asili itatawaliwa na Watanzania asili, na sio "wavamizi", "walowezi", au watu wa kuja!.
Hii sio mara yangu ya kwanza kuizungungumzia nafasi ya Zanzibar kwenye urais wa JMT, pia niliizungumza hapa!.
Japo hakuna kupokezana: Kiukweli, kihaki, kihalali na ki Kudumisha Muungano, 2015 Urais wa JMT ni Zamu ya Zanzibar!.
Wawakilishi wa Zanzibar mlioko Dodoma, lipiganieni hili nalo liingizwe rasmi kwenye Katiba kuwa urais wa JMT, wa kupokezana!.
Asante.
Paskali
Paskali,Zanzibar ni ya wazanzibari,kuna wazanzibari wenye asili ya Kiafrika,kuna wazanzibari wenye asili ya kihindi,kuna wazanzibari wenye asili ya kichina,kuna wazanzibari wenye asili ya kiarabu,kuna wazanzibari wenye asili ya kishirazi(Iran) na kadhalikaMkuu Chabuso, kwanza asante kwa hii, nimeguswa!, najitafakari!, ila pia hii iisue ya ubaguzi wa kuwabagua Wanzanzibari kwenye urais wa muungano, haiwezi kuisha kwa kuikalia kimya!, jee kipi ni afadhali, bora tukae kimya Zanzibar iendelee kubaguliwa au ni afadhali kuufichua ubaguzi, ili uwe adressed affirmatively hata kama ufichuzi wenyewe nao ni ubaguzi?.
Tulipoungana, makubaliano ya Nyerere na Karume ilikuwa "wewe rais, mimi makamo!", lakini kufuatia uwezekano wa "mvamizi" kuwa rais wa Zanzibar, hivyo kumpelekea kuwa Makamo wa rais wa JMT na if anything happen to rais wa JMT, then automatically, Makamo anakuwa rais, hivyo URT nayo kutawaliwa na "mvamizi", yale mabadiliko ya katiba ya 1992, yalimuengua rais wa Zanzibar kwenye structure ya muungano, he is nobody now!, just to rule out the posibility ya "mvamizi" kuwa rais wa JMT!, huo nao sio ubaguzi?, umepenyezwa mpaka kwenye katiba!, huko hamuusemi!, ila Pasco kausema ndio tunanyoosheana vidole vya ubaguzi?!.
Wanzanzibari wepi hao unaowazungumzia wanataka nchi yao?, wakati kiukweli wanaojidai kuitaka nchi yao ni "vizalia" vya "wavamizi", Wanzanzibari wenyewe halisi, tuko nao hapa Dodoma, wakihuidhuria BMK ambaolo litaibuka na katiba ya serikali mbili kuelekea serikali moja!.
Pasco
Mkuu Dustman, hili jambo niliwahi kulizungumza hapa.Hawa watu wamegundua kuwa kile chama cha njano na kijani kimejenga kasumba ya kupitisha wagombea wa urais wa Muungano kutokea bara kwa kutumia wingi wa wajumbe.Nawaunga mkono,wssikate tamaa kutafuta haki.
P.Wanabodi,
Tanzania ni nchi ya Jamhuri ya Muungano, yenye watu kutoka iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, na kuunda nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao raia wake wa pande zote mbili, wako sawa na wana hadhi sawa na uhuru kamili wa kila kitu ikiwemo kugombea na kushika madaraka ya nafasi juu kabisa ya uongozi kwenye JMT, hii ni nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hamdhani kwamba sasa umefika wakati, kunahitajika some specific measures kama some kind of affirmative action, kuhakikisha, rais wa JMT pia apatikane kutoka upande wa pili wa muungano?, yaani kwa wapenda haki, hatuwezi kuacha ,rais wa JMT , andelee tuu kuchaguliwa by chance, kutoka upande wowote wa JMT wakati kuna kila dalili za kuonyesha kamwe rais wa JMT, hawezi tena kutoka Zanzibar by chance, hivyo marais wote wa Tanzania ya vyama vingi ni kutoka upande mmoja tuu wa Muungano huku bara!. Is this fair kwa wenzetu Wazanzibari ambao ni raia wenye haki sawa ndani ya JMT?!. Hamdhani huu ni wakati muafaka tuwe na affirmative action ili Mzanzibari aweze tena kuwa rais wa JMT?.
Hii sio mara yangu ya kwanza kuizungungumzia nafasi ya Zanzibar kwenye urais wa JMT, pia niliizungumza hapa!.
Japo hakuna kupokezana: Kiukweli, kihaki, kihalali na ki Kudumisha Muungano, 2015 Urais wa JMT ni Zamu ya Zanzibar!.
Wawakilishi wa Zanzibar mlioko Dodoma, lipiganieni hili nalo liingizwe rasmi kwenye Katiba kuwa urais wa JMT, wa kupokezana!.
Asante.
Paskali
Sawa kabisa mkuu,tutegemee bomu kulipuka muda wowote baada ya umoja wa Mataifa kugundua mchawi wa amani ndani ya nchi hizi zenye Muungano feki.Mkuu Dustman, hili jambo niliwahi kulizungumza hapa
P.
There is nothing the UN can do to a sovereign state, mbele ya UN, Zanzibar sio nchi, nchi ni URT!.Sawa kabisa mkuu,tutegemee bomu kulipuka muda wowote baada ya umoja wa Mataifa kugundua mchawi wa amani ndani ya nchi hizi zenye Muungano feki.
Wewe jamaa hii ni lugha ya maudhi🤣🤣🤣🤣... tafadhali futa kauli ndugu Mjumbe!Kubali, kataa, ukweli ndio huo!, ukiwaondoa "wavamizi" waliotoka walikotoka, wakajifanya pale ni kwao!, then, wale waliowakuta walipoleta uvamizi wao ni Watanganyika, na ndio maana sasa tumewaoa kama wake zetu tuu, tunawalisha, tunawavisha na pesa za matumizi juu, wao kazi yao, kula bure, kulala bure!.
Rudi kwenye Jiogrofia ya uumbaji, angalia visiwa vya Indian Ocean, tazama visiwa vya Indian Ocean vilitoka wapi?!.
Pasco
Moja kati ya Matamanio ya ku Utopia!Zanzibar inataka kujitoa katika huu Mungano,wazanzibari hawataki urais wa Tanzania...wanataka nchi yao
"Time will tell",kama unamtegemea Jecha ujue kuwa ameshafukuzwa kazi,...tusubiri uchaguzi mwengine tuone nini kitatokea...Moja kati ya Matamanio ya ku Utopia!
Haitawezekana.
Mkui chabuso"Time will tell",kama unamtegemea Jecha ujue kuwa ameshafukuzwa kazi,...tusubiri uchaguzi mwengine tuone nini kitatokea...
Mkui chabuso"Time will tell",kama unamtegemea Jecha ujue kuwa ameshafukuzwa kazi,...tusubiri uchaguzi mwengine tuone nini kitatokea...
Sanduku lilileta jibu la matumaini 2015 kama sio uhuni wa Jecha na chama chake hivi sasa Wazanzibar wangelikuwa wanazungumza stori nyengineMkui chabuso
Hakuna siku hata moja sanduku la kura likalete jibu la matumaini na matamanio yenu ya kujitenga nje ya Muungano.
Haitawezekana. Hategemewi Jesha kama Mtu, bali unategemewa Mfumo kuzuia matamanio yenu.
Hata huyu aliyepo leo baada ya Jecha ni Jecha yule yule katika mwili na sura tofautu. Ila kimatakwa ya watawala ni Jecha yule yule!
Viongozi wenu ni walafi, rahisi kuwa rigged na Wakubwa wa Bara na kimoyomoyo wanaupenda Muungano kwani ndio unaowahakikishia kula na usalama wao na vizazi vyao!
Mkuu Mhadzabe , sorry ni kweli nimetumia lugha kali na ya maudhi, ila sijatukana.Wewe jamaa hii ni lugha ya maudhi🤣🤣🤣🤣... tafadhali futa kauli ndugu Mjumbe!
Wazanzibari walipomosea ni pale walipoweka matamanio ya wao kujijenga wenyewe na kunufaika kisiasa kwa upande mmoja tu wa Muungano, Zanzibar.
Urekebishaji wa katiba yao na kuipata hii waluonayo yalilenga kujitanua wenyewe ndani ya visiwa na si Bara!
Ulafi huu utawakosti sana.
Kutapita miaka mingi sana kwa aina ya siasa za leo zinakoelekea kupata Rais wa JMT kutoka upande wa visiwani!
Watishia umakamu wa Rais au u PM otherwise sioni namna yeyote wahafidhina wa Bara wakampa Mzanzibar upenyo wa Kuwa Rais wa Bara kutoka Loliondo Mpaka Ntwara, Dar mpaka Kasulu na Namanyele!
Haitawezekana. Haiwezekani si kwa CCM ni bali hata kwa Upande wa Upinzani!
Hapo kwenye kuulinda nakuunga Mkono Paskali!Mkuu Mhadzabe, sorry ni kweli nimetumia lugha kali na ya maudhi, ila sijatukana.
Mtoto amebebwa mgongoni kwa mbeleko, anakula bure, analala bure, badala ya kuwa na shukrani, yeye anapiga mateke tuu kwa aliyembeba.
Mama hata apigwe vipi mateke na mtoto wake mgongoni, hawezi kumbwaga chini, hivyo ndivyo ilivyo kwa muungano, tunaubeba na kuendelea kuubeba na tutaulinda kwa gharama yoyote.
P
Kwanini msimfukuze mtoto akajipangie chumba chake kama analeta maudhi yote hayo!??Mkuu Mhadzabe, sorry ni kweli nimetumia lugha kali na ya maudhi, ila sijatukana.
Mtoto amebebwa mgongoni kwa mbeleko, anakula bure, analala bure, badala ya kuwa na shukrani, yeye anapiga mateke tuu kwa aliyembeba.
Mama hata apigwe vipi mateke na mtoto wake mgongoni, hawezi kumbwaga chini, hivyo ndivyo ilivyo kwa muungano, tunaubeba na kuendelea kuubeba na tutaulinda kwa gharama yoyote.
P