Je kuna umuhimu wowote kumuandalia Chakula mumeo wakati housegirl yupo?

Mh! Jamani, sasa wengine wanafanya ionekane kama huyo mume ni mtoto wa 2yrs au mlemavu! Afuliwe, apangiwe nguo, awekewe maji. Mh!
 
Yessssss ni muhimu kwa mwanamke kumwandalia mme chakula. Inaonyesha mapenzi. House girl ni kwa watoto na nyumba. Wanawake wa kizungu pia wanafanya hio, esp east europe.

Mapenzi ni zaidi ya kufanyiwa hiki na kile maana hiyo ni conditional love. Mfano wengine waume zetu hawapendi mikono yetu iwe migumu na sura ziharibike maana mama ndo pambo la nyumba. Kuepusha hayo wao pia husaidia kufanya kazi, so twafanya kwa kusaidiana na kurahisisha baadhi ya mambo kwa ku mechanise nyumba through various machine pale uwezo unaporuhusu. Mama na baba huwa viongozi kwa nyakati tofauti na wakati mwingine kwa pamoja pale wawapo nyumbani. Housegirl ni part ya watoto wetu ila yeye huwa mkubwa wa watoto maana yu mkubwa ki umri na wote hufanya haya kwa upendo bila one kuwa mtumwa na wengine kuwa mabwana.
 
Mhh Jamani..
LOVE HAS TO BE BOTHWAYS and it has to be unconditional.
Mke unachoona unaweza mfanyia mumeo unconditional mfanyie na Mume vile vile unachoona unaweza mfanyia mkeo pia umfanyie.

One sided love huo sasa ni utumwa...ndio maana jamii nyingi za kiafrika hasa enzi za mababu wanawake seem not be happy. Kwa sababu kuolewa ilikuwa ni kutumikishwa..Na wengi huishi maisha yaliyojaa kusononeka..Uzae (achia taabu ziambatanazo na ujauzito), ulee watoto...etc

Mume ukiona siku na wewe umwandalie mke wako nguo za kuvaa fanya hivyo..tatizo liko wapi. Ukiona msuprise mkeo kwa mahunjamati pia fanya hivyo..
Maisha sasa hivi "mke na mume" wote wanahangaika kutafuta kipato..so hata ndani ya nyumba kuwepo kusaidiana unconditionally...and thats how love grows strongly
 
Mapenzi ni zaidi ya kufanyiwa hiki na kile maana hiyo ni conditional love. Mfano wengine waume zetu hawapendi mikono yetu iwe migumu na sura ziharibike maana mama ndo pambo la nyumba. Kuepusha hayo wao pia husaidia kufanya kazi, so twafanya kwa kusaidiana na kurahisisha baadhi ya mambo kwa ku mechanise nyumba through various machine pale uwezo unaporuhusu. Mama na baba huwa viongozi kwa nyakati tofauti na wakati mwingine kwa pamoja pale wawapo nyumbani. Housegirl ni part ya watoto wetu ila yeye huwa mkubwa wa watoto maana yu mkubwa ki umri na wote hufanya haya kwa upendo bila one kuwa mtumwa na wengine kuwa mabwana.

You are right madam.
 
Swadaktaaaaaaa!
1.Na kazi ya mume ni ipi?

2.Je wanaokaa majuu huko mnafanyaje maana kila mtu anaenda kwenye mihangaiko kwa faida ya familia na hakuna cha hausigeli kwa walio wengi.

3.Je mke akisafiri, ina maana mume hali, haogi, hatandiki kitanda, wala hafanyi usafi chumbani hadi mke arudi?

Haya maswali ni mazuri. Imenikumbusha last week, nilikuwa nasikiliza mahubiri ya Dr Myles Munroe. Nitajaribu kujibu maswali yako kutokana na uelewa wangu wa point zake.
1. Kazi ya mume ni ipi?
Kazi ya mume imebadilika kutokana na jinsi hali ya dunia ilivyobadilika. Ukiangalia historia ya mwanadamu na hata physical appearance ya mwanadamu, mwanaume alikuwa ndo mfanyakazi. Na hichi kilifanya marriage kuwa rahisi. Kila mmoja alitambua role yake, na kuitekeleza ipasavyo. Mwanaume alienda alienda kazini au kuwinda (yaani kutafuta mlo), na mwanamke alibaki nyumbani na kutunza watoto na nyumba. Hii ndo ilikuwa hali ya maisha iliyofuatwa kwa muda mrefu sana.
Lakini vita vya pili vya dunia, vilibadilisha huu mfumo. katika vita vyovyote wanaume ndo walienda kupigana. Lakini kutokana na urefu na kusambaa kwa vita hivi kulisababisha kusombwa kwa wanaume wengi zaidi kwenda vitani na hivyo kuacha viwanda, mashamba, nk bila wafanyakazi. Hali hii iliwabidi wanawake waingie na kuchukua sehemu ya wanaume katika jamii kwa madhumuni ya kuendeleza production.
Tatizo lilianza baada ya vita kuisha. Wanaume kurudi nyumbani wakakuta kazi yao inafanywa na wanawake. Na wanawake pia wakabutuka kuwa na wao pia wanaweza. Basi kwa ufupi, hii ndo ime-distort mfumo mzima, na kusababisha high divorce rates, nk.
Kwa hiyo sasa inabidi wanaume ku-adopt katika huu mfumo mpya, na hivyo kutambua role yao mpya katika marriage. Na kujua hiyo role yao mpya - inabidi tuwaulize nyie - What do you want from your man? Kwa hiyo wewe unatafuta mwanaume, tafuta yule atakayekupa jibu utakalo wewe. Kama ni chai asubuhi kitandani, nk. Sio unatafuta mwanaume alafu ndo unajaribu kumfanya awe kile unachotaka. Sidhani kama inafanya kazi hivyo. Unatakiwa kumpata yule anayefit mahitaji yako.

2. Je wanaokaa majuu huko mnafanyaje maana kila mtu anaenda kwenye mihangaiko kwa faida ya familia na hakuna cha hausigeli kwa walio wengi.
Kwa ufupi, mimi ninavyoona, wanawake wengi huolewa kwa ajili ya kupata watoto. Na wakati mwanamke akiwa na mimba na hata kitoto kichanga, huweza kuchukua muda off kazini kwa ajili ya kumhudumia mtoto. Tatizo linakuja hapo baadae, na ndio ukiangalia stats utaona ndipo palipo na divorce nyingi. Mwanamke anapomaliza maternity yake na kurudi kazini, basi msuko-suko wa maisha unawazidi nguvu wana-ndoa na kusababisha divorce.
Lakini pia kumbuka huku majuu kazi za ndani zimerahisishwa kidogo kwa vitu kama washing machines, dryers, dish-washers, vacuum cleaners - maana nyumba nzima ni carpet hivyo hakuna kupiga deki, rice cooker, frozen foods, nk. Hivyo maisha ya kutunza nyumba sio magumu kama ya bongo. Kutengeneza chai ni kitu cha muda mfupi sana. Vitafunio ni vya kununua. Hivyo maisha yanaenda tu. Na labda ndo maana huku hakuna nyumba ndogo, maana hakuna mtu wa kukuogesha, au sijui hivi na vile. Huku ninachoona zaidi ni one-night stands.

3. Je mke akisafiri, ina maana mume hali, haogi, hatandiki kitanda, wala hafanyi usafi chumbani hadi mke arudi?
Hivi vinaendelea kama kawaida kutokana na maelezo yangu ya huko juu. Maisha yamekuwa simple sana, kuishi kama bachelor ni rahisi.

Sina uhakika kama nimekujibu swali lako kisahihi, lakini nimeandika kwa mtazamo wangu tu.
 
Chaku kwani hujui kazi ya mwanamke ni nini?
Chakula kikiwa kitamu unataka mmeo amsifie nani house girl? We utajiskiaje? Nimeshuhudia ndugu yangu akimpa talaka mke wake na housegirl akachukua nafasi ya mywaifu hivi hivi mtoto alikuwa anakaanga jamani.
 
Chaku kwani hujui kazi ya mwanamke ni nini?
Chakula kikiwa kitamu unataka mmeo amsifie nani house girl? We utajiskiaje? Nimeshuhudia ndugu yangu akimpa talaka mke wake na housegirl akachukua nafasi ya mywaifu hivi hivi mtoto alikuwa anakaanga jamani.

hahahahaa..ndivyo itavokuwa endapo mai waif anamwachia kila kitu housegirl.....
 
hahahahaa..ndivyo itavokuwa endapo mai waif anamwachia kila kitu housegirl.....

Ndo maana mimi nasema wanawake hawapaswi kutulaumu sisi wanaume pindi unapo amua kuchukua mtu mwingine azibe nafasi yaani utakuta housegirl ndie anae fua na kukunyoshea,anakuwekea maji bafuni,anakuandalia chai nzito, anakuandalia msosi bab kubwa,ndie anae ratiba shughuli zote za home pale usafi kumwagilia maua, ana wabembeleza watoto na kushinda nao kazi ya wife nini hapo kama sio bed room tu.
Jamaa nilimpongeza sana kwa kuchukua house girl na kumtimua wife maana wife alionekana hakuna kazi anayo ifanya nyumbani hata kuosha vyombo anashindwa kila kitu house girl yeye ni kugombeza tu house girl kwa nini umevunja glass kwa nini kochi kitambaa kimedondoka aaah akapigwa chini chini.
 
Chaku kwani hujui kazi ya mwanamke ni nini?
Chakula kikiwa kitamu unataka mmeo amsifie nani house girl? We utajiskiaje? Nimeshuhudia ndugu yangu akimpa talaka mke wake na housegirl akachukua nafasi ya mywaifu hivi hivi mtoto alikuwa anakaanga jamani.

Duh hiyo kali sasa huyo mume siku akila kwa mama ntilie siatamfukuza housegirl na kumleta huyo mama ndani? mke ni zaidi ya chakula yeye tu ladha yake ukiijua vizuri chakula utakua unakihitaji kujaza tumbo tu lakini flavour yake inaongezeka mama akiwa tu hapo karibu yako. Nikwavile waume hawajajua kutunza wake zao inavyotakiwa ndo maana anaweza linganisha mkewe na mtoto yaani housegirl. Huyo mume wa hivyo hata upikeje bado tu macho yake yanaona kinyume nyume. Kwa ufupi mme kumfanya housegirl substutute ya mke ni kutojua who he is and what is his purpose in this world, hizo nyingine ni justifications tu ili society imuelewe.
 
Nyumba ni ya mama, siku zote. Mwanamke jiulize hivi mgeni akija kwako akakuta mume kavaa nguo imejikunja kama imetoka mdomoni kwa ng'ombe au nyumba iko hovyo hovyo tu, unadhani nani atachekwa? wewe, mumeo au housegirl? Je ulivyokubali kuolewa hukujua position yako kama mwanamke?
mimi ni mwanamke, am sorry to say this lakini wanawake tumezidi kutake advantage ya hawa ma housegirl. Enzi za wazazi wetu how many divorces have u heard compared to know? Mwanamke fikiria.. when u were young jinsi mama,shangazi,mamdogo, binamu walivyokuwa wanajali waume zao.
kuwa na fulltime job and kuwa fulltime mother hainizuii kutekeleza majukumu yangu ya nyumbani kama mama, its how u plan ur time and ur tasks.At the end of the day hata mume nae anajikuta ana adopt tabia zako, ukirudi home unakuta kaosha vyombo, au kapika n.k.
Dada ukiona hafanyi yeye sio malaika kujua kuwa ungependelea afanye hivyo, kaa nae chini mueleze jinsi unavyojisikia na jinsi ambavyo ungependelea akusaidie. Tatizo letu sometimes we just assume kuwa mwanaume atafanya tu. Communication ndani ya nyumba ni muhimu.
Housegirl wala simhitaji nyumbani kwangu coz kama mwanamke niliyekamilika I can handle tasks zangu kwa msaada wa mume wangu. Wanawake tuache uvivu sometimes,just because huyo housegirl yupo ndio unaona huwezi, je asingekuwepo?
Mumeo hawezi kumsaidia housegirl kutandika kitanda, but kama ni wewe atakuambia "honey shika kule na mimi huku tu tandike shuka".

Ujumbe: hata siku moja wanawake hatuwezi kushindana na wanaume, at the end mwanaume atashinda tu na tena ukimletea kujua utabaki unalia na wanao ndani yeye huyoooo kwa nyumba ndogo tena huko anapata full service na mgongoni anabebwa sembusi kupigiwa pasi?
 
Yessssss ni muhimu kwa mwanamke kumwandalia mme chakula. Inaonyesha mapenzi. House girl ni kwa watoto na nyumba. Wanawake wa kizungu pia wanafanya hio, esp east europe.

Watoto nilizaa mimi na mume wangu, ni responsibility yetu pia. Siwezi kumpa mume 100% attention and care wakati watoto niliowazaa mtu mwingine ndio anawashughulikia. I don't have a housegirl and i don't need one, I only have a lady who comes to help na kazi ndogo ndogo when tupo kazini na watoto shule but tukirudi home na yeye anaondoka coz that is the only time mimi, mume na watoto we get to bond as a family.

Dada ukimuachia housegirl watoto, attachment between u and them inakuwa haipo. Watamuona Housegirl ndio mama
 
Usiri wa nyumba aujua mke na mume. Heshima na upendo hujengwa na hao wawili ambao ni mwilli mmoja. Housegirl ni mfanyakazi kama wafanyakazi wengine, anatafuta kipato. Yeye hawezi kuamua tu kufanya hivyo, ni utaratibu ambao hao wawili wanakuwa wameupanga. Lakini tusiwe busy sana hadi tukaja kusabanisha vishawishi ambavyo sii vya lazima. Kila upande utambue wajibu wake-mume, mke na housegirl.

AKATAE MIZIZI YA MITI NA ASISUBIRI MATUNDA YAKE.
 
Nyumba ni ya mama, siku zote. Mwanamke jiulize hivi mgeni akija kwako akakuta mume kavaa nguo imejikunja kama imetoka mdomoni kwa ng'ombe au nyumba iko hovyo hovyo tu, unadhani nani atachekwa? wewe, mumeo au housegirl? Je ulivyokubali kuolewa hukujua position yako kama mwanamke?
mimi ni mwanamke, am sorry to say this lakini wanawake tumezidi kutake advantage ya hawa ma housegirl. Enzi za wazazi wetu how many divorces have u heard compared to know? Mwanamke fikiria.. when u were young jinsi mama,shangazi,mamdogo, binamu walivyokuwa wanajali waume zao.
kuwa na fulltime job and kuwa fulltime mother hainizuii kutekeleza majukumu yangu ya nyumbani kama mama, its how u plan ur time and ur tasks.At the end of the day hata mume nae anajikuta ana adopt tabia zako, ukirudi home unakuta kaosha vyombo, au kapika n.k.
Dada ukiona hafanyi yeye sio malaika kujua kuwa ungependelea afanye hivyo, kaa nae chini mueleze jinsi unavyojisikia na jinsi ambavyo ungependelea akusaidie. Tatizo letu sometimes we just assume kuwa mwanaume atafanya tu. Communication ndani ya nyumba ni muhimu.
Housegirl wala simhitaji nyumbani kwangu coz kama mwanamke niliyekamilika I can handle tasks zangu kwa msaada wa mume wangu. Wanawake tuache uvivu sometimes,just because huyo housegirl yupo ndio unaona huwezi, je asingekuwepo?
Mumeo hawezi kumsaidia housegirl kutandika kitanda, but kama ni wewe atakuambia "honey shika kule na mimi huku tu tandike shuka".

Ujumbe: hata siku moja wanawake hatuwezi kushindana na wanaume, at the end mwanaume atashinda tu na tena ukimletea kujua utabaki unalia na wanao ndani yeye huyoooo kwa nyumba ndogo tena huko anapata full service na mgongoni anabebwa sembusi kupigiwa pasi?

Nimependa ur analysis, sasa subiri wabeijing waje hapa......
 
Usiri wa nyumba aujua mke na mume. Heshima na upendo hujengwa na hao wawili ambao ni mwilli mmoja. Housegirl ni mfanyakazi kama wafanyakazi wengine, anatafuta kipato. Yeye hawezi kuamua tu kufanya hivyo, ni utaratibu ambao hao wawili wanakuwa wameupanga. Lakini tusiwe busy sana hadi tukaja kusabanisha vishawishi ambavyo sii vya lazima. Kila upande utambue wajibu wake-mume, mke na housegirl.

AKATAE MIZIZI YA MITI NA ASISUBIRI MATUNDA YAKE.

wow...quote of the week.....
 
Wakuu ebu nisaidieni kuna umuhimu wowote kumwandalia chakule mumeo wakati housegirl/houseboy yupo na analipwa kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kuanzia usafi hadi chakula kinaenda vizuri?

chaku wewe jinsia gani? maana jina kama la kike na sura ya kiume. kama wa kike naomba uweke avatar ya Maria nyerere basi
 
Yes ni muhimu kwa mke kufanya hivyo kwa mumewe labda mke awe amesafiri, anaumwa, hayupo na labda siku fulani kachoka na kumuomba housegirl amsaidie.
Anaweza pia akakusaidia usafi huyo mfanyakazi ila siyo chumbani mnapolala wanandoa, humo ni wewe tu kuwajibika.
Hayo ni kati ya majukumu ya mwanamke kwenye mji wake.

Belinda,
Ninaomba niweke msisitizo hapo katika usafi wa chumbani. Kama mke hayupo amesafiri au hata kama ana shughuli zingine, jukumu la usafi wa chumbani kwa wanandoa linabaki mikononi mwa mume. Mume anapaswa kufanya usafi mwenyewe bila ya kutaka kumshirikisha housegirl. Afterall usafi wa chumbani ni jukumu la wanandoa wote mke na mume, ningependelea zaidi kuona kuwa wanaume wanajishughulisha na usafi wa nyumbani kila mara.
 
Swadaktaaaaaaa!
1.Na kazi ya mume ni ipi?

2.Je wanaokaa majuu huko mnafanyaje maana kila mtu anaenda kwenye mihangaiko kwa faida ya familia na hakuna cha hausigeli kwa walio wengi.

3.Je mke akisafiri, ina maana mume hali, haogi, hatandiki kitanda, wala hafanyi usafi chumbani hadi mke arudi?

1. Shukrani kwa swali lako zuri, mimi naona nivizuri wasaidiane wote kwa pamoja. Hata mme naye anaweza akawa na siku zake za kuingia jikoni kupikia familia especially during weekend time.
2. Sisi wamajuu kwa kweli bila kuwa na ushirikiano kwa pamoja huo uhusiano ni rahisi sana kuvunjika...maana mmoja akiwa wakulemewa na mizigo yote kwa kweli atafika siku atachoka. Na hapo hapo anaona jinsi waume pengine wawenzake wanavyochakarika kwa kweli itakuwa ngumu kwake.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom