Je kuna umuhimu wowote kumuandalia Chakula mumeo wakati housegirl yupo?

Akili Unazo!

JF-Expert Member
Feb 18, 2009
3,930
4,893
Wakuu ebu nisaidieni kuna umuhimu wowote kumwandalia chakule mumeo wakati housegirl/houseboy yupo na analipwa kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kuanzia usafi hadi chakula kinaenda vizuri?
 
Wakuu ebu nisaidieni kuna umuhimu wowote kumwandalia chakule mumeo wakati housegirl/houseboy yupo na analipwa kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kuanzia usafi hadi chakula kinaenda vizuri?

Hakyanani, kama mi ndo mumeo, acha kuniandalia hayo uone.
 
Chaku please usiniangushe darling eh
Yote yafanya out of love sweetheart.. kama unampenda mumeo utamfanyia tu kwanza we mwenyewe unawezaukajikuta unasahau hata kama housegirl yupo!!

Ila naye asiichukulie kama ni wajibu wako mpenzi.

Everything U do, do it for LOVE!
 
Yes ni muhimu kwa mke kufanya hivyo kwa mumewe labda mke awe amesafiri, anaumwa, hayupo na labda siku fulani kachoka na kumuomba housegirl amsaidie.
Anaweza pia akakusaidia usafi huyo mfanyakazi ila siyo chumbani mnapolala wanandoa, humo ni wewe tu kuwajibika.
Hayo ni kati ya majukumu ya mwanamke kwenye mji wake.
 
Yes ni muhimu kwa mke kufanya hivyo kwa mumewe labda mke awe amesafiri, anaumwa, hayupo na labda siku fulani kachoka na kumuomba housegirl amsaidie.
Anaweza pia akakusaidia usafi huyo mfanyakazi ila siyo chumbani mnapolala wanandoa, humo ni wewe tu kuwajibika.
Hayo ni kati ya majukumu ya mwanamke kwenye mji wake.

Thank you.
 
Kumuandalia mume chakula ni kazi ya mke,kufanya usafi wa nguo za mume ni kazi ya mke,kupanga chumba na kutandika kitanda,kumpelekea maji ya kuoga bafuni ni kazi yake pia.ukitaka kusaidiwa vyote hivyo bila sababu ya msingi unamtengenezea huyo msaidizi mazingira ya kukurithi.kaa chonyo wanawake wengine wameharibu ndoa zao kwa uzembe wakarithiwa.wewe usiwe moja wao.
 
Kumuandalia mume chakula ni kazi ya mke,kufanya usafi wa nguo za mume ni kazi ya mke,kupanga chumba na kutandika kitanda,kumpelekea maji ya kuoga bafuni ni kazi yake pia.ukitaka kusaidiwa vyote hivyo bila sababu ya msingi unamtengenezea huyo msaidizi mazingira ya kukurithi.kaa chonyo wanawake wengine wameharibu ndoa zao kwa uzembe wakarithiwa.wewe usiwe moja wao.

Swadaktaaaaaaa!
1.Na kazi ya mume ni ipi?

2.Je wanaokaa majuu huko mnafanyaje maana kila mtu anaenda kwenye mihangaiko kwa faida ya familia na hakuna cha hausigeli kwa walio wengi.

3.Je mke akisafiri, ina maana mume hali, haogi, hatandiki kitanda, wala hafanyi usafi chumbani hadi mke arudi?
 
Swadaktaaaaaaa!
1.Na kazi ya mume ni ipi?

2.Je wanaokaa majuu huko mnafanyaje maana kila mtu anaenda kwenye mihangaiko kwa faida ya familia na hakuna cha hausigeli kwa walio wengi.

3.Je mke akisafiri, ina maana mume hali, haogi, hatandiki kitanda, wala hafanyi usafi chumbani hadi mke arudi?

WoS, nadhani maelezo yake hili yako hapo kwen nyekundu

Kumuandalia mume chakula ni kazi ya mke,kufanya usafi wa nguo za mume ni kazi ya mke,kupanga chumba na kutandika kitanda,kumpelekea maji ya kuoga bafuni ni kazi yake pia.ukitaka kusaidiwa vyote hivyo bila sababu ya msingi unamtengenezea huyo msaidizi mazingira ya kukurithi.kaa chonyo wanawake wengine wameharibu ndoa zao kwa uzembe wakarithiwa.wewe usiwe moja wao.
 
Kumuandalia mume chakula ni kazi ya mke,kufanya usafi wa nguo za mume ni kazi ya mke,kupanga chumba na kutandika kitanda,kumpelekea maji ya kuoga bafuni ni kazi yake pia.

MFUMO DUME huo. Mwanamke haolewi ili atumikishwe kazi. Kunatakiwa kusaidiana ama sivyo atakuwa kama Punda.
 
Nimekupata.
Naomba unijibu maswali yangu hasa la kwanza....hapo nitaelewa na nitachangia zaidi


Hahaha, hapo nilimsaidia tu kwenye hilo cause it was a bit obvious, hayo mengine sijui mtizamo wake utakuwaje mwenye aliyepost lol!
 
Ninachopingana nacho ni mazoea ya mume kuhudumiwa na h/ girl.mazingira kama hayo, huyo mdada kuwa karibu na mumeo,mara asante dada kwa chakula kizuri, wewe umelala tu,huo ni mfano.mimi mwenyewe namsaidia sana mke wangu.na akisafiri nadeki mwenyewe chumba changu,hiyo ndiyo heshima ya ndoa.mimi sitaki kukutana na mke wangu kitandani tu,upendo nikutumikiana hivo ndivo vionyo vinavyoleta ladha ktk ndoa.
 
Je kuna umuhimu wowote kumuandalia Chakula,chai mumeo wakati housegirl yupo??
NDIYO.
2.Je wanaokaa majuu huko mnafanyaje maana kila mtu anaenda kwenye mihangaiko kwa faida ya familia na hakuna cha hausigeli kwa walio wengi.
Hapa housegirl ndio anawajibika kuwaandalia wote wawili.

3.Je mke akisafiri, ina maana mume hali, haogi, hatandiki kitanda, wala hafanyi usafi chumbani hadi mke arudi?
Hapa housegirl ndio atamuandalia huyo mwanaume, kuhusu studio (Chumbani) yote mawili yawezekana yaani mume mwenyewe atandike kitanda au hata huyo housegirl.
Ila mwanaume hapo usianze mambo mengine tofauti.
 
Nimekupata.
Naomba unijibu maswali yangu hasa la kwanza....hapo nitaelewa na nitachangia zaidi

Kazi za mume katika uhusiano wenu wa ndoa Ndugu Giroy ni zipi

Hahaha, hapo nilimsaidia tu kwenye hilo cause it was a bit obvious, hayo mengine sijui mtizamo wake utakuwaje mwenye aliyepost lol!
asante ndugu

Ninachopingana nacho ni mazoea ya mume kuhudumiwa na h/ girl.mazingira kama hayo, huyo mdada kuwa karibu na mumeo,mara asante dada kwa chakula kizuri, wewe umelala tu,huo ni mfano.mimi mwenyewe namsaidia sana mke wangu.na akisafiri nadeki mwenyewe chumba changu,hiyo ndiyo heshima ya ndoa.mimi sitaki kukutana na mke wangu kitandani tu,upendo nikutumikiana hivo ndivo vionyo vinavyoleta ladha ktk ndoa.

Huu mjadala nao! Na msaidizi akiwa wa kiume inakuwaje?..utazoeana naye halafu inakuwaje maana unasema hausgeli ukimzoea basi na mengine ni possibility!
Ninachotaka kuona ni mke na mume wakiwa na uhusiano mzuri bila kufanya mwingine mtumwa kwa visingizio vizivyo na msingi.
 
Ninachopingana nacho ni mazoea ya mume kuhudumiwa na h/ girl.mazingira kama hayo, huyo mdada kuwa karibu na mumeo,mara asante dada kwa chakula kizuri, wewe umelala tu,huo ni mfano.mimi mwenyewe namsaidia sana mke wangu.na akisafiri nadeki mwenyewe chumba changu,hiyo ndiyo heshima ya ndoa.mimi sitaki kukutana na mke wangu kitandani tu,upendo nikutumikiana hivo ndivo vionyo vinavyoleta ladha ktk ndoa.
Mazoea haya yakizidi housegirl anakuwa mke msaidizi.
 
Yessssss ni muhimu kwa mwanamke kumwandalia mme chakula. Inaonyesha mapenzi. House girl ni kwa watoto na nyumba. Wanawake wa kizungu pia wanafanya hio, esp east europe.
 
Kumuandalia mume chakula ni kazi ya mke,kufanya usafi wa nguo za mume ni kazi ya mke,kupanga chumba na kutandika kitanda,kumpelekea maji ya kuoga bafuni ni kazi yake pia.ukitaka kusaidiwa vyote hivyo bila sababu ya msingi unamtengenezea huyo msaidizi mazingira ya kukurithi.kaa chonyo wanawake wengine wameharibu ndoa zao kwa uzembe wakarithiwa.wewe usiwe moja wao.
Je nakinyume chake yaani mume haruhusiwi au hatakiwi kuyafanya hayo!?

Kumuandalia mke chakula, kufanya usafi wa nguo za mke na kuogesha watoto, kutandika kitanda, na kumpelekea mke maji ya kuoga bafuni si kazi yake pia?

Kina dada mnalionaje jambo hilo si katika haki zenu kufanyiwa haya yote!?
 
Wakuu ebu nisaidieni kuna umuhimu wowote kumwandalia chakule mumeo wakati housegirl/houseboy yupo na analipwa kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kuanzia usafi hadi chakula kinaenda vizuri?

Binafsi, sioni kama ni muhimu saana. Kama muda unaruhusu, yes 'mke anaweza' kumuandalia Mume chakula hata kama housegirl/houseboy yupo. Lakini kama muda hauruhusu, mfano mke pia ni muhangaikaji (kazi/kibarua/biashara) kama Mume, sidhani kama ni kosa chakula kikiandaliwa na housegirl/houseboy au Mume mwenyewe ajiandalie. Ikumbukwe hata huyu Mwanamke anatumia 'damu' na siyo 'kamashine' flani kasikochoka. So, wote Mume na Mke wana majukumu ya kuandaliana chakula pale inapobidi na kama wanao hao Maids,then why to pay a person for nothing.

I bet kama ni Mume wa kurun na housegirl, hata kama mke atampikia, kumfulia na kumuosha, kama ni mchafu ni mchafu tu, atarun na maid kama kawa.

Unless huyo Mume naye awe ameoa huyo Mke kwa kumtumikisha, otherwise sioni kwa nini mke mbali na kuhangaika huko na kule kama mumewe, then akifika nyumbani aanze tena sijui kupika na mengineyo, wakati mume sijui anaangalia TV or whatever, no way.
 
Kwa Ushauri tu, rejea katika mafundisho ya kidini (labda uwe mpagani), wanume wanaaswa kuwapenda wake zao, na wake wanatakiwa kutii...chakula cha mumeo au nguo zake za ndani kwa mfano usimwachie house girl kufanya, siyo mfumo dume wanao kushauri wengine bali ni ishara ya heshma na kutii na inaonesha mumeo ulimkubali kwa yote.ina maana kama h/girl asingekuwepo msingekula au kuvaa nguo safi?
wanaume pia kwa upendo wanafarijika sana wakiona mkewe akimjali hivi, na yeye siku zote atakupenda na kukuheshimu kama ni mtu mwenye akili timamu.....ukimwachia housegirl majukumu yote hayo hata yeye mwenyewe anakudharau kwanza anakuona tu kama mtu uliye kuja kwa ajili ya tendo la ndoa.ila kuna wakati ambao kwa mfano wote mpo ofcn mpaka late, jioni, hapa mnatakiwa kusaidiana kwa makubaliano lakini, sio lazima
 
Back
Top Bottom