Je, Kuna Umuhimu wa Kufanya Uchaguzi wa Rais Ifikapo Oktoba 2020

Mk54

JF-Expert Member
Dec 29, 2016
1,997
3,932
Ni kwa kipindi kirefu sana tangu tuingie kwenye mfumo wa Vyama vingi. Sijawahi kuridhishwa na mfumo wa Uongozi unaoendeshwa na chama tawala.

Ni chama ambacho kila kinachofanywa ni kwa mujibu wa kisiasa; ni kipindi cha wakati huu utaona ujenzi wa barabara usio na kiwango unaendelea, viongozi wanatumbuliwa ili kuamsha hisia za wananchi (Hivi suala la Kangi Lugola limeishia wapi? Mmeshasahau?).

Ukusanyaji wa kodi umekuwa wa speed ili kuhakikisha project kubwa zinakamilika ikiwa ni pamoja na Miradi ya Chato.

Ni lazima ikamilike kipindi cha awamu ya 5; huenda Rais ajaye mwaka 2025 akaisimamisha baadhi ya miradi inayoonekana kwenda kinyume na Sheria za Manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 na Kanuni zake za mwaka 2013 pamoja na Marekebisho ya mwaka 2016.

Pamoja na haya yote, sidhani kama kuna Mtanzania yeyote mwenye akili timamu anayetamani Chama cha Mapinduzi kitoke Madarakani; hii haimaanishi kwamba CCM wanafanya vyema; Tanzania hatujawahi kupata Upinzani wenye tija na manufaa ya Taifa.

Tuliwaamini wapinzani katika kusimamia dafina na hazina ya Taifa letu, badala yake;

· Mpinzani anaomba kununua kesi ya Tanzania na Barrick ili Tanzania ishindwe na kuliingiza Taifa katika hasara

· Mpinzani anaandika barua kwenda nchi za Magharibi ili kusimamisha msaada wa fedha za elimu za ndugu zetu wa kike ambapo kijijini kwake kuna wasichana wengi wanakaa chini ya mawe

· Wapinzani ambao wanataka maridhiano ya kisiasa huku wanasambaza sumu kwa viongozi wa kidini na kulitia Taifa letu kwenye machafuko ya kiimani

· Wapinzani ambao wanachochea maandamano kupitia Mjane anayeishi nje ya nchi ili nchi yetu imwage damu na kuingia katika historia butu

· Upinzania ambao unaitia Taifa hasara ikiwa ni pamoja na kupokea Ruzuku ambazo ni kodi za wananchi huku wao wakienda kuzitumia kwa ajili ya matumbo yao

· Upinzani ambao hauna msimamo katika kauli zao badala yake wanapokea wala rushwa na kuwapa nafasi za juu kabisa; Je tukitoa hazina na dafina ya Taifa letu itakuwaje?

Hivyo, kuna haja ya vijana kati ya miaka 30-45 mjipange na kutengeneza Upinzani usiokuwa na Tamaa, Rushwa, Ukabila, Dini na Ngono na wenye nia Thabiti ya kuingia Magogoni ili kuleta muktadha chanya kwenye Taifa la Tanzania.

Kwa upinzani upi kwa mfano utakaomfanya Rais wa sasa asiweze kushinda Uchaguzi ujao?Kwa nini tunapoteza muda na fedha wakati majibu yapo Dhahiri.

Tunachangamoto nyingi katika Afya, Miundo mbinu, Ajira, Elimu, Kilimo na mfano wake; je ni kwanini hizi fedha zisielekezwe kwenye tija? Tunafanya uchaguzi mkuu kuridhisha wazungu au kwa manufaa yetu?

Mwisho, Sikubaliani na Magufuli Katika Ubabe Wake, Kujichukulia Yupo Juu Ya Nchi. Utasikia Akisema Nita-----Nitafanya Hivi au Vile. Tanzania Ni Taifa, Haufanyi Bali Tunafanya.

Serikali Ifikirie Namna ya Kuachana na Uchaguzi Mkuu na Gharama zote Ziende Kwenye Shughuli za Maendeleo ya Taifa Letu Adhimu

Thank you.
 
Demokrasia hakuna na ninafikiri itakuwa tu kama uchaguzi mdogo uliopita.
 
Haipo Demokrasia au hatuna Upinzani wenye tija, Je unadhani kuna mpinzani yoyote mwenye hadhi ya kuingia Magogoni?
Kwanza umejiwekea ujinga au brain barrier kwamba hakuna anayeweza kwenda Ikulu including yourself.... Yaani tayari wewe akili yako umeishusha na kutegemea mwingine eti ainue maisha yako. Lakini cha ajabu ni kwamba toka uzaliwe mpaka leo ni wewe mwenyewe umekuwa unaendesha maisha yako na familia yako, kwa kutumia akili yako....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haipo Demokrasia au hatuna Upinzani wenye tija, Je unadhani kuna mpinzani yoyote mwenye hadhi ya kuingia Magogoni?
Jiwe mwenyewe hafai, wapo watu wengi mno wangetufaa sana ila demokrasia yetu haiwapi mazingira ya kuchomoza.
 
Kwanza umejiwekea ujinga au brain barrier kwamba hakuna anayeweza kwenda Ikulu including yourself.... Yaani tayari wewe akili yako umeishusha na kutegemea mwingine eti ainue maisha yako. Lakini cha ajabu ni kwamba toka uzaliwe mpaka leo ni wewe mwenyewe umekuwa unaendesha maisha yako na familia yako, kwa kutumia akili yako....

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwani mimi ni mpinzani au raia huru?
 
Usiwe kama popo, lazima ujipambanue unachokiamini ama upande unaoegemea, upinzani ama watawala.

Kuna mengi uliyoeleza ya hovyo ni kweli ni ya hovyo.

Lakini kila kitu kina upande wake wa pili wa shilingi, haujajihangaisha na kueleza mema yanayofanywa na awamu hii kupelekea hao waTz uliowasema wenye 'akili timamu' waendelee kuunga mkono juhudi.

Hilo la kusema uchaguzi uwepo ama usiwepo ni habari nyingine, maana jambo hilo lipo ndani ya katiba.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usiwe kama popo, lazima ujipambanue unachokiamini ama upande unaoegemea, upinzani ama watawala.

Kuna mengi uliyoeleza ya hovyo ni kweli ni ya hovyo.

Lakini kila kitu kina upande wake wa pili wa shilingi, haujajihangaisha na kueleza mema yanayofanywa na awamu hii kupelekea hao waTz uliowasema wenye 'akili timamu' waendelee kuunga mkono juhudi.

Hilo la kusema uchaguzi uwepo ama usiwepo ni habari nyingine, maana jambo hilo lipo ndani ya katiba.


Sent using Jamii Forums mobile app

1. Raisi ameongeza bajeti ya Dawa kutoka Bil 31 hadi Bil 270. Hili ni kwa mara ya kwanza kwa Tanzania
2. Mradi wa Reli ni jitihada za Rais
3 Kufufuliwa kwa Shirika la ndege
4. Ujenzi wa Daraja la Sarenda Bridge
5. Muelendelezo wa Interchange ya Ubungo
6. Barabara 8 za Kimara
7. Kuongeza ukusanyaji wa Mapato
8. Kuimarisha sheria ya Madini Na kupunguza upigaji wake
9.Kuondoa watumishi hewa zaid ya elf 20 kwa kipindi cha Mwaka mmoja tu; na kupunguza mishahara hewa
10 Kuongezeka kwa vituo vya kutolea huduma za Afya Tanzania. Hospital Na vituo vya kutolea huduma za Afya ni zaidi ya 7500, ukilinganisha na Mwaka 2010 Hadi 2014, idadi ya Vituo ilikuwa ni chini ya elf 4000 tu.

Maguful amefanya vyema ukilinganisha Na Rais yoyote kutokea. It is okay kutoelewa kwa Sasa; kila kitu kina hitaji Muda kueleweka Na hili pia Muda wake utafika.

Mapungufu yake yanavumilika.
 
Mimi sina muda kbs wa kupiga kura ili mtu apate kula kwa katiba yetu hii na tume yetu hii. Leo nimeangalia clip ya Bashiru akihojiwa Azam Tv wakati huo akiwa Dr. Analia na katiba na tume.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom