JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 625
- 938
Umuhimu wa kunyonyesha kwa mama ni kama ifuatavyo:-
Mama anayenyonyesha huepukana na adha za uzazi na kurejea katika hali yake ya kawaida kwa haraka na kirahisi. Hii ni kutokana na Homoni za Oxytocin ambazo hutoka wakati wa kunyonyesha zinazosaidia kurudisha mji wa mimba katika hali yake ya awali na kusaidia kukoma kwa haraka kwa damu itokayo baada ya uzazi.
Tafiti zinaonesha kuwa wanawake walionyonyesha wana uwezekano mdogo sana wa kupata Saratani ya Ovari na ya Matiti.
Vilevile Mwanamke aliyenyonyesha ana uwezekano mdogo sana kupata uzito uliokithiri na magonjwa yatokanayo na matatizo ya moyo kama shinikizo la damu na mafuta mengi mwilini.
Lakini pia, unyonyeshaji unachelewesha kurejea kwa mzunguko wa hedhi kwa mama hivyo hutoa mda kati ya mimba moja na nyingine.