Je, kuna uhitaji wa kuwa na jukwaa la misaada?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,782
JamiiForums
Moderator
Naomba mada hii msiipeleke kule jukwaa la malalamiko, ushauri na pongezi... Ni mada ya kuamsha mjadala juu ya kile kinachoendelea sasa hivi hapa Jamiiforums
Natangaza maslahi yangu kwenye hili... Sina tatizo na mtu anayeomba msaada... Na nimeshasaidia sana... Na mimi vilevile katika maisha yangu nimeshasaidiwa sana tu, tena na watu baki... Hivyo nisitafsiriwe vinginevyo
JamiiForums nadhani inaingia mwaka wake wa 12 tangu kuanzishwa kwake... Imepitia vipindi vingi... Vigumu na vyepesi... Lakini kubwa kuliko yote imeendelea kukua, kujulikana, kujitangaza vizuri na kuaminika zaidi kuliko mitandao mingine mikubwa....
Hili limevutia wengi kujiunga na huu mtandao.... Na halijatokea kwa bahati mbaya bali kujituma kwa uongozi, kusimamia sheria taratibu za jukwaa kwa ukamilifu wake...
Sasa basi hali ya uchumi wa nchi, ukosefu wa ajira, maisha magumu kumepelekea wengi kukimbilia JF kuomba misaada mbali mbali kuanzia karo za shule, nguo, chakula na mahitaji mengine muhimu
Wapo wafuatiliaji hivyo wakiona mmoja kasaidika na huja ama hushauriwa nao kuomba....
Ni katika makundi hayo waongo, wadanganyifu na matapeli pia hawakosekani... Mifano iko mingi tuu....

RAI YANGU
Je kutokana na ongezeko kubwa la wataka misaada.... Ni wakati muafaka sasa wa kuwa na jukwaa maalum kwa ajili ya hili jambo?
Je hii haitavutia wengi zaidi na kugeuza JF sehemu ya kuombea misaada?
Je ithibati na uhalisia wa wataka misaada vitahakikiwa na nani?
Je tunaweza kuwa na mawazo mbadala kwenye hili?

Ni mjadala wa wazi unaoweza kutoa suluhisho kwenye hili.. Karibuni
 
Mi naona lisiwepo maan kutajaa matapeli kibao kwenye hilo jukwaa
Jukwaa liwepo maana leo kila mtu analia na hawa watu kwenye suala ya kumsaidia mtu mtandaoni huwa wanakuja watu wote wawili mwenye shida kweli na tapeli na ugumu unakuja utamjuaje
 
Halina maana yoyote.

Misaada ipo ya aina nyingi, kwa atakayehitaji msaada wa aina fulani basi atapeleka ombi jukwaa husika.
 
Nimeona mkuu huu uzi ila jamaa alionekana mgumu wa kulipa kiatu cha samaki alisema kwenye reply zake
 
Mkuu hata mm hapa nilipo nahitaji msaada, ww hapo ulipo pia wahitaji msaada. Lkn shida yangu na yako haziwezi kuwa sawa siku zote.
Point yangu ili base kwenye hii reply yako
Halina maana yoyote.

Misaada ipo ya aina nyingi, kwa atakayehitaji msaada wa aina fulani basi atapeleka ombi jukwaa husika.
 
Wengi wanaaomba misaada sio wakweli wanapoteza imani ya wayoa misaada kwa wenye uhitaji wa ukweli hivyo itapelekea jukwaa la malalamiko kujaa post za kutapeliwa
Lakini pia si kila shida ni ya kukimbiza JF... Kuna mahitaji muhimu ya pesa ndefu kama karo na matibabu... Na haya wahusika huleta mpaka vielelezo.... Hili huwapa wahusika imani ya kuchangia lakini kuna mengine mmh....
 
Lakini pia si kila shida ni ya kukimbiza JF... Kuna mahitaji muhimu ya pesa ndefu kama karo na matibabu... Na haya wahusika huleta mpaka vielelezo.... Hili huwapa wahusika imani ya kuchangia lakini kuna mengine mmh....

Haya matatizo yanatofautiana uwezo kuna mtu anaweza kukwama kwa jambo ambalo wewe kwa uwezo wako ukahisi kama anatania vile..
 
Huyu jamaa kaleta hadi vielelezo kumbe tapeli ika kapiga pesa ndefu hapa

Uzi wake mwingine huu

Lakini pia si kila shida ni ya kukimbiza JF... Kuna mahitaji muhimu ya pesa ndefu kama karo na matibabu... Na haya wahusika huleta mpaka vielelezo.... Hili huwapa wahusika imani ya kuchangia lakini kuna mengine mmh....
 
Mie naomba liwepo ila sasa cha muhimu kama mtu atasema ana uhitaji wa kusaidiwa aweke details zake vzr tutafute watu wa eneo husika maana mm najua tumesambaa sana wajiridhishe kama ana shida watu wamsaidie
 
Huyu jamaa kaleta hadi vielelezo kumbe tapeli ika kapiga pesa ndefu hapa

Uzi wake mwingine huu

Mmh ulikuja kumgunduaje? Na huyo mtoto alikuwa wake kweli?
 
Back
Top Bottom